mkuu kwanza hongera sana kwa kuwa na ardhi kubwa , ni hivi we mtu wako muhimu hapa ni surveyor ambaye ameshafanya kazi kama hii ...ukipita mwenyewe utaumia tena vibaya , huyu surveyor kama jamaa walivyosema hapo juu lazima ana mtu wake wizarani , step ya kwanza ni kujua mipango ya serikali kwa eneo hilo kwa hiyo watakuja huku kuchukua vipimo vyao kupeleka wizarani , baada ya hapo sasa ndio wakate hizo plots alafu urudi tena wizarani kwa approval alafu ndo nafikiri stage ya mwisho project yako inaweza fanyika na wewe ukauza I guess ndio mpango wenyewe , vizuri unapouza washirikishe manispaa , so kama plot ya mil 5 mnaweza sema hata mil 6 etc manispaa ndio itangaze kwa wanaotaka viwanja ....hamna sehemu yenye urasimu bongo kama ardhi lakini komaa hii kitu inawezekana kabisa ila andaa hela ndefu kufanikisha .....