Are spies made or born?

infantry soldier askari wa miguu mambo gan ya ajabu hayo??[emoji23] [emoji23]
mkuu, tunafutana tongotongo kwa hizi mambo za "lip reading" ...... mimi sijui kabisa kama kuna professions za namna hii hapa duniani. kweli ushamba ni mziggo
 
mkuu, tunafutana tongotongo kwa hizi mambo za "lip reading" ...... mimi sijui kabisa kama kuna professions za namna hii hapa duniani. kweli ushamba ni mziggo
mtafute mtu mwambie aseme "BIBI" na "PIPI" bila kutoa sauti akiwa mbali uone ilivo shida kutofautisha unatakiwa uangalie movement za lips zake na akili yako iwe sharp
 
François Gaston de Lévis
 
De levis Kaja kwa sasa wachangiaj wa mwisho mlianza kupoteza maana michanngo ya awali ikikuwa imeshiba mkisoma mabandiko ya. Awali
Mi nikaja nikarekebisha kuhusiana na akili na matumizi kimahitaji.
De levis kafafanua hoja za kujibu kichwa cha thread tena kwa mifano ya anayoita kwa mwanaye na classmate wake.
Baba yke pia inaonyesha
ALL WE BORN AS SPIES LACK OF TIME AND ENOUGH SPACE LEAD US INTO ZERO RECOGNITION.

Calmness of heart and mind inaletwa na muda na nafasi pekee ya kupumzika au kazi changamfu.
Yote ya yote right person anatengenezwa kwa malezi yake mwenyewe au ya watu wengine.
Meditation ni dawa kwa watu hawa wanaoamin juu ya nguvu za fikra au matumiz makubwa ya.akili.


Tafuteni uzi wa meditation humu jf mjishibishe vema mpractise then mtaona faida za hiyo kitu ambayo inasaidia sana kazi hii.
Watu wengi wanaoudumu humo wanakuwa private room kwao kwa ajili ya shughuli hiyo na utunzaji wa rasilimali saidia ambazo mara nyingi husaidia kurefresh na kuifanya akili mpya na angavu baada ya muda.

N.b. kujua mambo haya kunahitaji self efforts na selfinvestments kwa ko wewe na kizazi chako.
Na ndio maana waswahili wanasema mtoto wa nyoka ni nyoka
Na samaki mkunje angali mbichi, akiauka akunjiki atakuchoma miba.
Karibuni uswahilini
 
Bila shaka wote mu wazima wa afya, kama heading inavyojielezea hapo juu ni swali nililokuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sasa kama uwezo wa hawa watu huwa ni wa mafunzo au wanazaliwa wakiwa tayari na hizi attributes?

Ninawasilisha.
Russian spy Andrei Bezrukov said:
"Intelligence is not like a thriller novel or action film. If you behaved like James Bond, you wouldn’t last more than half a day"
 
Bila shaka wote mu wazima wa afya, kama heading inavyojielezea hapo juu ni swali nililokuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sasa kama uwezo wa hawa watu huwa ni wa mafunzo au wanazaliwa wakiwa tayari na hizi attributes?

Ninawasilisha.
big man Infantry Soldier, spies are both, born then made and molded to fit the specific trade requirements. for instance, the KGB spy machinery had so many spy school across the ussr. some of those school were located kwenye top secret military installations katikati ya misitu minene ambapo recruits walikuwa wanapelekwa huko usiku wa manane wakiwa wamefungwa vitambaa vyeusi usoni wasijue wanaenda wapi, mpaka kufikia mida ya sasa kumi na moja alfajiri panaanza kupambazuka ndio wanaanza kufika kambini na kutolewa vitambaa wasijue wapo sehemu gani hata washindwe kurudi walipotoka..........

hawa jamaa wa kgb walikuwa na spy school zingine located at the city center. hivi unaweza kuamini spy school inaweza kuwa katikati ya jiji kama vile moscow ama tuseme kariakoo kwa namna palivyo busy kiasi kile??? kwa mfano shule yao moja ya kijasusi ilikuwa kati kati ya jiji moja huko poland ilikuwa ipo ghorofa tano chini kabisa ya jengo refu la ghorofa 20, huko juu zilikuwa ni shopping malls, super markets kubwa za kufa mtu, garage za magari kukiwa na kelele na ubize wa kila namna, kumbe chini kabisa ghorofa 5 kuna team kubwa ya watu wanafundishwa mautundu ya ajabu ya kijasusi..............
 
nadhani ni katik thread hii niliwahi kutaja sifa za mtu anaefaa kuwa jasusi..nitazirejea kwa kifupi..
1. jasusi lazima awe na kumbu kumbu..hii ni sifa muhimu sana lazima akili yake iwe ina rekodi kila jambo na kila hatua anayopitia na kwa usahihi..kuanzia asubuhi ambo yoote unayofanya/unakpita unarekodi kisha jioni unaandika report ya kika kitu bila kuacha..na pia ukiulizw ajambo lililotokea wiki mbili zilizopita ulikumbuke kwa usahihi na kwa mapaa yake..kuna watu hawana kumbu kumbu yaani hat kushika namba5 za simu hawezi..binafsi sina jina la mtu yeyote kwene simu yangu bali namba tu na ninajua namba hii ni ya nani na hata kuitaja..niliifundisha akili katika hilo..so kumbu kumbu ni sifa muhimu
2.. lazima jasusi afikiri kuwa mantiki (logic)...lazima ujiulize kwa nini hik kiko hivi na ninaweza vipi kukibadilisha katika muonekano huu na kikawa kitu kingine, kufikiri kwa logic ni muhimu sana, na katika kufikiri lazima ujiulize , why, who, where, what etc...ukiwa mtu wa kukurupuka lazima uumie..
3.lazima awe mtu wa kuchunguza (observation)..haijalishi mahali alipo lazima achunguze mazingira na nini kinaendelea..ukiingia ndani ya nyumba lazima uichunguze kwa mda mfupi na kwa umahiri mkubwa ujue ina milango migapi, madirisha, nk nk..akili lazima iwe inarekodi..na lazima uangalie escape route iwapo kutatokea shida..mlango lioingia sio wa kuutegema sana..
4..jasusi lazima ajue kubadilika kulingana na mazingira au eneo alilopo..awajue watu wanaomzunguka wanataka nini na ni wa aina gani..jasusi laizma ajue kucheza na hisia za watu(sifa muhimu sana hii)
5..jasusi lazima ajue kusikiliza milango yote 7 ya fahamu(sio 5 ni 7)..katika ubongo wa mwanandam kuna maelekezo mengisana yanayomuonya mtu juu ya jambo flan.(wengine wanaita machale) machale haya humuonya mtu juu ya hatari iliyo mbele so ni lazima jasusi ajue namna ya kusukiliz amilango yake yote na kuchukua hata inayostahili kama yu katika hatari

hapo ni baadhi ya sifa anazopaswa kuwa nazo jasusi..sasa ukiangalia sifa hizo hakuna hata moja hapo ianayofundishwa darasani zote ni za kuzaliwa...na kwa kweli wote tunazaliwa tukiwa pure isipokuwa tunajaza uchafu mwingi kwenye ubongo na kuharibu nguvu ya akili...hata katika maisha ya mtu wa kawaida tu sifa hizo hapo juu ni muhimu sana..huwezi kuyatawala mazingira kama huna utulivu wa akali.... The mind is a good servant but a terrible master...lazim akili yako uitawala na uitume ifanya jemabo flani sio yenyewe ikutme wewe kufanya jambo flani..
sasa ukiw ana sifa hizo hapo juu na zingine ambazo sijazitaja kisha ukaingizwa darasana na kunolewa sawa sawa lazima ufnay mambo makubwa..

ndugu zangu mambo haya huwa hayaji hivi hivi ni lazima ujitume katika kuhakikisha akili yako inakuwa sawa mda wote na u-keep low profile,upayukaji hauhusiki, majigambo,nk...ukiishi kama mastaa wa movie hwezi chukua round ktik game hii...
kwenda kwenye vyuo vya mafunzo haya ,,,huko unaongezewa mbinu mfano za kutumia silaha za aina zote, namna ya kujihami, namna ya kugoma kuhojiwa iwapo utakamatwa....
mazingira ya ujasusi yamezungukwa na hatari, ukiwa, upweke na kivuli so nilazima jasusi ajifunze mbinu zoe za awali za kazi hii (tradecraft)...

kwa hiyo naweza kusema kuwa watu hawa sifa kubwa ni zile za kuzaliwa kisha wanaingizwa darasan/vyuoni ili kupewa mafunzo kufit mahitaji yaliyopo...

nimalize kwa kunukuu maneno ya mwalimu wangu:
1 when you control your thoughts, you control your mind, when you cotrol your mind you control your life; and once you reach a stage of being in total contolof your life you become the master f your own destine.

2..Alwys life favors the prepared mind
3.. in life there is no mistakes but lessons...sometime pain can be a good teacher

NB: mwambieni Invisible auweke uzii huu sticky maana kuna mda nautafuta siupati
 

Uchambuzi mzuri..!!
 
NB: mwambieni Invisible auweke uzii huu sticky maana kuna mda nautafuta siupati
Mkuu wangu de'levis habari za masiku.

hapo kwenye kuitafuta thread hii halafu huipati,bila shaka kile kigezo kimoja wapo ulichosisitiza sana kuhusu spy kutunza kumbukumbu kinahusika.

ili kuondoa usumbufu wa kuitafuta thread ambayo ulishawai kukomenti nyakati za nyuma,yafuatayo inabidi uyakumbuke:

1:kumbuka maneno yaliyomo ndani ya thread au title yake then I-type google ili isachiwe.

2:kumbuka sub section forum(jukwaa) ambalo mada hiyo iliwekwa.mfano jamii intelligence, siasa nk.
 
mkuu de'levis, umemwaga nondo za kutisha sana katika andiko lako hapo juu. mimi naweza kusema ya kwamba tatizo letu sisi vijana ni kuwa huwa hatupendi kupitwa na jambo na ndio sababu mama inayopelekea watu kukosa kabisa utulivu wa akili (mental tranquility). unakuta kijana mmoja ni mtu wa pombe kali, ana mademu nane, jana usiku ameshindwa kula kisa arsenal amefungwa, etc, na mambo mengine kadha wa kadha yasiyokuwa na tija katika kujenga maisha yake ya kila siku au hata katika kumuongezea uwezo flani katika maisha yake achilia mbali kuja kuwa jasusi hapo baadaye.

swali langu: hivi, kwa hapa tanzania kuna watu/vijana kweli waliozaliwa wana sifa za namna hiyo kama ulivyoziainisha hapo juu???
 
hahahaaaaaaaaa, you made me laugh man
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…