sasa huyu dada ndio aliona ndio njia mbadala ya kupunguzia machungu yake, na ndio kashanogewa hivyo so kifutacho ni kuishi na mume kwa ajili ya watoto, mume alichokuwa anakitafuta amekipata.....
They need something special that's why they do it.
Hapa mkuu linakuja swala la kwa vile yeye anafanya ngoja na mm nifanye sijui ukifanya kwa kulipiza kwa ubaya unamkomoa nani.
what about cheating for fun, as NN showed how it is done in the US
Well said mkuu
Kama mtu unafanya kwasababu fulani alifanya basi hapo ni confirmed kwamba UPUMBAVU UMEZIDI UJAZO.....mtu Unapofanya unatakiwa kufanya kwa utashi wako na sio kwasbabu partner kafanya
Anyway
Kumsaidia "shogake" MJ1, mwambie aendelee hadi mafuta yatakapoisha then atajua cha kufanya!!! Kwani hainiingii akilini mtu anataka kuacha halafu anshindwa, hapo ndio huwa sielewi, ukiamua kuacha unaacha.... ukiamua kuendelea unaendelea
Wapendwa WanaJF.
Natumaini wote mu wazima........naombeni msaada wa namna ya kushauri.
Ni rafiki yetu kifamilia, kwa muda mrefu yeye na mumewe wamekuwa kwenye migogoro ya hapa na pale ya kindoa. Kusema ukweli mumewe amekuwa akimis-behave kwa kipindi ikiwemo kucheat, physical abuse and the like. Mke akawa anaumia, anaconfront wanagombana.. After a while mgogoro ule ukapungua (ile frequency ya wao kuja kushtaki kwetu kesi zao ukapungua na mwisho kuisha kabisa- wadau tukakaa na kumshukuru MUNGU juu ya wokovu huu maana hali ilipokuwa inaelekea ilikuwa inatishia uhai wa ndoa ile).
Juzi kanijia huyo mke ananomba ushauri kama mwanamke mwenzie. Akatoa siri ya mafanikio 'amani' ya miujiza iliyotawala kwenye ndoa yake kwa kipindi kile. Alisema alikujaamua kuwa 'mpole' asimfuatilie mumewe wala asijihangaishe naye....alitafuta 'mshefa' wa pembeni naye akawa anajilia raha kwa nafasi!!!....sikuamini lakini kutokana na matatizo aliyokuwa nayo kipindi kile nadhani nilimwelewa ingawa sikuafiki.
Sasa anadai mumewe amejirekebisha sana na amebadilika na kuwa 'mume' tatizo liko kwake amejikuta amedevelop hisia kali za mapenzi kwa 'Mshefa' kuliko kwa mumewe na kila akijaribu kumuacha huyu jamaa anashindwa maana anasindwa kujicontrol kabisa. Not only that hata 'Mshefa' huyo hana dalili za kumsaidia 'kurudi' kwa mumewe kihisia kwani kila mara anakuwa kama anamblackmail vie kuwa anampenda na eti somehow huyu mwanamke amesababisha kutokuelewana flani kati yake yeye 'Mshefa' na mkewe nyumbani kwake. So kila mdada akijaribu kumuacha 'Mshefa' mshefa anakuja juu kimapenzi yaani anachochea vile.
Mdada anasema mumewe alishagundua juu ya cheatignyake lakini akamsamehe baada ya mke kukiri na kuapa kuacha. Ila sasa ndo anashindwa kihisia yuko kwa 'Mshefa' zaidi ya mumewe. Anaomba msaada afanyeje a'rudishe' mapenzi na hisia kwa mumewe??
Amekiri kuwa alifanya kosa na anajutia kutafuta 'faraja' nje ya ndoa.
Naombeni tumsaidie .....Nitawaacknowledge msijali
Kumsaidia "shogake" MJ1, mwambie aendelee hadi mafuta yatakapoisha then atajua cha kufanya!!! Kwani hainiingii akilini mtu anataka kuacha halafu anshindwa, hapo ndio huwa sielewi, ukiamua kuacha unaacha.... ukiamua kuendelea unaendelea
ndo maana mimi nimesema na ninasema tena dada hajaamua kuacha, na kama ni hivo sisi ni nani basi hata tumwambie aache kama nafsi yake haijakubali?!!
Nini sasa suruhisho la hii ndoa?
<br />Kama hajaamua kuacha basi aombe aolewe aone kama mshefa yupo tayari kubeba mizigo miwili kwa wakati mmoja.<br />
Wanawake ni wepesi sana kudanganyika na mianaume inayo kata kiu kwa muda tu
- Trick ya kwanza ni kummwaga huyo anayemwita mshefa, huyo ndo anayemwangamiza! Huo mvuto anaoupata kwa Mshefa ni sawa na faraja anayopata mgonjwa wa malaria anapokuwa juani. Anapata faraja huku anapandisha homa mwilini na kuwa mgonjwa zaidi. Huyo mshefa ni mgonjwa kama yeye (naye ana matatizo yake kwake ambayo siku moja yataisha).
- Hatua ya pili ni kuangalia heshima yake mwenyewe! Mapenzi ya mshefa wala si fulfilling, ni kuwa tu alikimbizwa huko na chuki na hasira kwa mmewe. Anashindwa kutoka sababu huyo bwana Mshefa anamng'ang'ania (bado anamhitaji kumtumia), siku atakapomchoka atamfanyia vibaya kuliko alivyofanyiwa na mmewe, kwani huyo hana responsibility yoyote kwake (atamflash kama toilet paper). Mapenzi mengi ya washefa huisha namna hiyo!! Kibaya ni hiyo guilty feeling itakayoendelea kumtesa maisha yake yote (Kinachotofautisha binadam na wanyama ni utambuzi wa mema na mabaya - rationality) - Hayo mabaya anayoyatenda, akijua ni mabaya, yanamuumiza yeye zaidi kuliko huyo anayedhani anamkomoa (akibeba ngoma itamtafuna - hata akimwambukiza na mme siku zote atajuta kuwa yeye ndo fisadi aliyeleta ngoma).
- Ajitoe fully kwa mme wake, hata kama hajisikii feelings mwanzoni. Ni kama kunywa dawa (yaani ni vigumu kunywa dawa ila matokeo yake ndo yanafanywa tulazimike kuinywa) - Atakavyoendelea kujitoa ndivyo feelings zitakaporudi na bond kuimarika zaidi. Akijitenga ameliwa, kwani feelings ndo zinaweza kupotea kabisaa na akajikuja anatumbukia kwa washefa wengine.
- Ajue kuwa yeye ni mgonjwa na hakuna dawa rahisi, yaani awe tayari kufanya maamuzi magumu ambayo mwanzoni yatamuumiza (Mfano kujishusha kwa mme wake - ataona anadhalilika, ila long term atapata heshima zaidi). Mapenzi ya washefa yanaleta faraja short term, tena faraja ya uongo. Long term ni maumivu na mateso moyoni, pengine na aibu juu!!
Nini sasa suruhisho la hii ndoa?
hivi mnajuaje kama huyu dada alifanya revenge au alifanya coz kama binadamu kamili anahitaji kitimiziwa hilo hitaji?
<br />
<br />
Dearest, binafsi nahisi naongeza mateso juu ya mateso. Ni either nijaribu kutimiza wajibu wangu kurejesha afya kwenye mahusiano yetu au nikayafanye hayo nikijua basi mkata wetu umeisha....
<br /><br />Haya mambo hayana formula mkuu, unaweza fanya vyote lakini bado tu, nafikiri tu dunia imeharibika, dhambi zimekuwa nyingi <br /><br />
hata yale mabaya tuyafanyayo hatuoni mabaya tena, tunaona kama ni haki yetu, visasi wengine, upweke sijui nini tufanye watu tuishi kwa amani
Hili sredi bado linaendelea?
Kama vipi nianze kulichakachua............ Sredi likiwa siriaz mwanzo mwisho linatakiwa lihamishiwe jukwaa la siasa.
MJ1 Msalimie shoga yako........BTW huyo mshefa wake unamjua?..........Navyowajua wanawake ntashangaa kama hajakuonyesha mtuwe kama kweli ni shoga yako kivile.....
.Habari zenu waungwana.......... nlikuwa napita tu, narudi jukwaa pendwa la maria roza.
bht nakubaliana na wewe kabisa kuwa uamuzi aliouchukua mke si sahihi lakini tukumbuke kuwa watu tunatofautiana jinsi ya kureact.nadhani the boss aliniuliza kitu nikamweleza ingekuwa mimi ningereact tofauti kabisa (ingekuwa mimi) lakini si wote wenye guts za kureact kama unavyofikiria wewe mpenzi. Kuna circumstances kibao, mwingiine anafikiria watoto wake (kama wana watoto); mwingine jamii tu inam-scare hata kufikiria uamuzi kama wa kukatisha mkataba wa ndoa. Kwa huyu dada inawezekana kabisa kuwa anafall kwenye mojawapo ya makundi haya ili mradi tu anao uwoga wa kuvunja ndoa. Najua wapo watakaoniuliza kama anaogopa kuvunja ndoa why akafanye kitendo ambacho ni dhahiri kinnawezapelekea kuivunja hiyo ndoa ambayo anajitetea kuiprotect ?? Well kuna post ambayo ameiweka mbu juu ya kutafuta faraja..........nadhani hii ilikuwa ni process
si kwamba ameamka, akavaa akatoka akaenda barabarani akasimama na kumpata mshefa la hasha. Si ajabu mshefa ni mtu wa karibu sana na familia yake, na pengine ni mtu ambaye yeye alianza kumweleza matatizo yake (kama rafiki either wa familia au rafiki tu) akawa anafarijiwa (si kimapenzi) hata ile kusikilizwa akilitoa dukuduku lake then in the process pengine ikafikia kulia, kubembelezwa, kukumbatiwa na mwisho kukissiwa na baadae kuliwazwa.
Yeye kama mwathirika kweli tutamhukumu kwa kushindwa kujizuia kipindi akiwa vulnerable?? Hebu tuangalie kwa upande huu pia jamani tuache kumnyooshea vidole mmama wa watu ambaye ameshagundua kosa sasa anataka kuweka sawa mambo.
mtm na fide ninaomba niwaulize swali la nyongeza: Suppose huyu mdada angekuja hapa akiomba ushauri wa manyanyaso na abuses anazozipata toka kwa mumewe; kunyimwa haki ya ndoa, kupigwa, mume kulala nje, mngemshaurije??