Arusha: Mama wa miaka 50 akutwa na bangi gunia 3

Arusha: Mama wa miaka 50 akutwa na bangi gunia 3

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mtuhumiwa mmoja pekee, Kanael Akyoo (50), ametiwa mbaroni na kikosi maalum cha kupambana na dawa za kulevya, akidaiwa kukutwa na magunia matatu na viroba tisa vya bangi nyumbani kwake.

Julai 6 mwaka huu, Rais John Magufuli aliagiza kuondolewa kazini na kushushwa vyeo kwa aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arumeru (OCD), Ofisa Usalama wa Wilaya hiyo (DSO), Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya hiyo (OC CID) na maofisa wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaohusika, baada ya kushindwa kudhibiti dawa hizo hadi Kaimu Kamishna wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya alipokwenda wilayani huko kufanya operesheni.

Jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Florence Khambi, alisema bangi hiyo ilikamatwa katika Kitongoji cha Karafia kilichoko eneo la Kisimiri Chini wilayani Arumeru.

Kwa mujibu wa Khambi, operesheni hiyo iliongozwa na Kamishna Jenerali wa DCEA, James Kaji, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Arusha.

Alisema kuwa katika ukaguzi wa awali kwenye maeneo ya mashamba ya kitongoji hicho walifanikiwa kukamata magunia 116 ya bangi.
Alisema pamoja hayo, pia walikamata viroba tisa vya bangi, gunia 1 la mbegu na misokoto 714 ya bangi.

Alisema kuwa katika operesheni hiyo, pia walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja Kanael Akyoo (50), mwanamke mkazi wa Karafia Kisimiri Chini akiwa na magunia matatu na viroba 9 vya bangi vikiwa vimehifadhiwa ndani ya nyumba yake.

“Juhudi za intelijensia ya taasisi hizo zilifanikisha kumkamta mtuhumiwa huyo na kwa kweli ni jambo jema, maana unapokamata kitu bila mtu inafikirisha," alisema.

Alibainisha kuwa magunia mengine 113 yalikamatwa katika nyumba zaidi ya 20 za wakazi wa eneo hilo ambapo watuhumiwa waliokuwa wakiyamiliki, walikimbia makazi yao.

Alisema kuwa mtuhumiwa Akyoo anatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya mchakato wa upelelezi kukamilika.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na tukio hilo, alisema kuwa kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya udhibiti wa dawa za kulevya, wameendelea kupambana na biashara hiyo haramu wilayani huko na hivi karibuni walifanikiwa kukamata watu watano wakituhumiwa kujihusisha na biashara hiyo na tayari wameshafikishwa mahakamani.

Alisema kuwa jana walipanga kufanya ziara ya kikazi katika maeneo ya Kitongoji cha Karafia na vijiji vingine wilayani humo ili kutoa elimu na kubadili fikra za wananchi kuhusu kilimo cha bangi ambacho alidai wananchi wa huko wanaona ndiyo kipato cha kuendeshea maisha yao.

“Tutaambatana na wataalamu wa elimu za kilimo biashara, tuna programu ya kuelimisha kilimo cha pareto ambacho hustawi sehemu za baridi ambacho kina kipato zaidi ya kilimo na biashara haramu dawa za kulevya aina ya bangi. Kilo moja ya pareto ni Sh. 1,600 hadi 2,000.

Kwa hiyo, kwenye gunia moja ni pesa nzuri kabisa na watabadilisha maisha yao na kuepuka bangi ambayo kila siku inawakutanisha na mkono wa dola," alisema Muro.

Chanzo: Nipashe
 
Hakuna serikali iliyowahi kumshinda mkulima wa bangi haswa wa kike,polisi mwachieni mama wa watu haraka iwezekanavyo la sivyo kimbunga cha Jah rastafarian,ever living,ever faithful,ever sure hakitawaacha salama.FIREEE BURN BABYLON.
 
Mtuhumiwa mmoja pekee, Kanael Akyoo (50), ametiwa mbaroni na kikosi maalum cha kupambana na dawa za kulevya, akidaiwa kukutwa na magunia matatu na viroba tisa vya bangi nyumbani kwake.

Julai 6 mwaka huu, Rais John Magufuli aliagiza kuondolewa kazini na kushushwa vyeo kwa aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arumeru (OCD), Ofisa Usalama wa Wilaya hiyo (DSO), Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya hiyo (OC CID) na maofisa wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaohusika, baada ya kushindwa kudhibiti dawa hizo hadi Kaimu Kamishna wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya alipokwenda wilayani huko kufanya operesheni.

Jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Florence Khambi, alisema bangi hiyo ilikamatwa katika Kitongoji cha Karafia kilichoko eneo la Kisimiri Chini wilayani Arumeru.

Kwa mujibu wa Khambi, operesheni hiyo iliongozwa na Kamishna Jenerali wa DCEA, James Kaji, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Arusha.

Alisema kuwa katika ukaguzi wa awali kwenye maeneo ya mashamba ya kitongoji hicho walifanikiwa kukamata magunia 116 ya bangi.
Alisema pamoja hayo, pia walikamata viroba tisa vya bangi, gunia 1 la mbegu na misokoto 714 ya bangi.

Alisema kuwa katika operesheni hiyo, pia walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja Kanael Akyoo (50), mwanamke mkazi wa Karafia Kisimiri Chini akiwa na magunia matatu na viroba 9 vya bangi vikiwa vimehifadhiwa ndani ya nyumba yake.

“Juhudi za intelijensia ya taasisi hizo zilifanikisha kumkamta mtuhumiwa huyo na kwa kweli ni jambo jema, maana unapokamata kitu bila mtu inafikirisha," alisema.

Alibainisha kuwa magunia mengine 113 yalikamatwa katika nyumba zaidi ya 20 za wakazi wa eneo hilo ambapo watuhumiwa waliokuwa wakiyamiliki, walikimbia makazi yao.

Alisema kuwa mtuhumiwa Akyoo anatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya mchakato wa upelelezi kukamilika.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na tukio hilo, alisema kuwa kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya udhibiti wa dawa za kulevya, wameendelea kupambana na biashara hiyo haramu wilayani huko na hivi karibuni walifanikiwa kukamata watu watano wakituhumiwa kujihusisha na biashara hiyo na tayari wameshafikishwa mahakamani.

Alisema kuwa jana walipanga kufanya ziara ya kikazi katika maeneo ya Kitongoji cha Karafia na vijiji vingine wilayani humo ili kutoa elimu na kubadili fikra za wananchi kuhusu kilimo cha bangi ambacho alidai wananchi wa huko wanaona ndiyo kipato cha kuendeshea maisha yao.

“Tutaambatana na wataalamu wa elimu za kilimo biashara, tuna programu ya kuelimisha kilimo cha pareto ambacho hustawi sehemu za baridi ambacho kina kipato zaidi ya kilimo na biashara haramu dawa za kulevya aina ya bangi. Kilo moja ya pareto ni Sh. 1,600 hadi 2,000.

Kwa hiyo, kwenye gunia moja ni pesa nzuri kabisa na watabadilisha maisha yao na kuepuka bangi ambayo kila siku inawakutanisha na mkono wa dola," alisema Muro.

Chanzo: Nipashe
Wamama wa ngalelooo
 
Wakati makampuni makubwa na baadhi ya nchi wakiruhusu iwe huru kwa matumizi huku shithole country wanakimbizana na wakulima na wavutaji....

Huu utakuwa umaskini wa akili...
 
Bangi na gongo ni biashara nzuri sana sana hasa kwa sisi watumishi wakati huu mungu usio na ongezeko la mshahara ndoo ya lita ishirini unapata zaidi ya laki na thenini bangi ndoo ndogo hukosi laki tatu hivi ila inategemea soko wakati wa msako bei hupanda Mara dufu
 
Bangi na gongo ni biashara nzuri sana sana hasa kwa sisi watumishi wakati huu mungu usio na ongezeko la mshahara ndoo ya lita ishirini unapata zaidi ya laki na thenini bangi ndoo ndogo hukosi laki tatu hivi ila inategemea soko wakati wa msako bei hupanda Mara dufu
Kuna Mwalimu mkuu mmoja huko Ngara aliwahi kudakwa kwa kukutwa na bangi,lkn alitoboa.
 
Mtuhumiwa mmoja pekee, Kanael Akyoo (50), ametiwa mbaroni na kikosi maalum cha kupambana na dawa za kulevya, akidaiwa kukutwa na magunia matatu na viroba tisa vya bangi nyumbani kwake.

Julai 6 mwaka huu, Rais John Magufuli aliagiza kuondolewa kazini na kushushwa vyeo kwa aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Arumeru (OCD), Ofisa Usalama wa Wilaya hiyo (DSO), Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya hiyo (OC CID) na maofisa wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaohusika, baada ya kushindwa kudhibiti dawa hizo hadi Kaimu Kamishna wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya alipokwenda wilayani huko kufanya operesheni.

Jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Florence Khambi, alisema bangi hiyo ilikamatwa katika Kitongoji cha Karafia kilichoko eneo la Kisimiri Chini wilayani Arumeru.

Kwa mujibu wa Khambi, operesheni hiyo iliongozwa na Kamishna Jenerali wa DCEA, James Kaji, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Arusha.

Alisema kuwa katika ukaguzi wa awali kwenye maeneo ya mashamba ya kitongoji hicho walifanikiwa kukamata magunia 116 ya bangi.
Alisema pamoja hayo, pia walikamata viroba tisa vya bangi, gunia 1 la mbegu na misokoto 714 ya bangi.

Alisema kuwa katika operesheni hiyo, pia walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja Kanael Akyoo (50), mwanamke mkazi wa Karafia Kisimiri Chini akiwa na magunia matatu na viroba 9 vya bangi vikiwa vimehifadhiwa ndani ya nyumba yake.

“Juhudi za intelijensia ya taasisi hizo zilifanikisha kumkamta mtuhumiwa huyo na kwa kweli ni jambo jema, maana unapokamata kitu bila mtu inafikirisha," alisema.

Alibainisha kuwa magunia mengine 113 yalikamatwa katika nyumba zaidi ya 20 za wakazi wa eneo hilo ambapo watuhumiwa waliokuwa wakiyamiliki, walikimbia makazi yao.

Alisema kuwa mtuhumiwa Akyoo anatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni baada ya mchakato wa upelelezi kukamilika.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na tukio hilo, alisema kuwa kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya udhibiti wa dawa za kulevya, wameendelea kupambana na biashara hiyo haramu wilayani huko na hivi karibuni walifanikiwa kukamata watu watano wakituhumiwa kujihusisha na biashara hiyo na tayari wameshafikishwa mahakamani.

Alisema kuwa jana walipanga kufanya ziara ya kikazi katika maeneo ya Kitongoji cha Karafia na vijiji vingine wilayani humo ili kutoa elimu na kubadili fikra za wananchi kuhusu kilimo cha bangi ambacho alidai wananchi wa huko wanaona ndiyo kipato cha kuendeshea maisha yao.

“Tutaambatana na wataalamu wa elimu za kilimo biashara, tuna programu ya kuelimisha kilimo cha pareto ambacho hustawi sehemu za baridi ambacho kina kipato zaidi ya kilimo na biashara haramu dawa za kulevya aina ya bangi. Kilo moja ya pareto ni Sh. 1,600 hadi 2,000.

Kwa hiyo, kwenye gunia moja ni pesa nzuri kabisa na watabadilisha maisha yao na kuepuka bangi ambayo kila siku inawakutanisha na mkono wa dola," alisema Muro.

Chanzo: Nipashe
Arusha ni mkoa wa kipekee wakina mama na wa dada ndo mapusha wa bangi pia na vibibi
 
Leo asubuhi nimeona askari akitoa furushi la bangi kutoka kwenye mkoba wake bila woga ijapo hanifahamu.

Nimegundua hii biashara inafanywa na baadhi ya askari pia
 
Back
Top Bottom