BABA SANIAH
JF-Expert Member
- Oct 20, 2013
- 4,606
- 5,922
Sasa Kama hakupendi unamlazimisha?Mara nyingi mawazo ya aina hii huwa ni ya vijana ambao hawajaoa na wanaishi kihuni , ila kwa aliye oa mke kihalali na wakaishi kwa kitambo kidogo na wakajaaliwa kupata familia, kuacha mke si jamboa jepesi jepesi tu kama unavyo lifikiria wewe ingawa hiyo haikufanyi usimuache mje mkorofi
Simon siro wapi ?Mama Samia Wadhibiti hawa watu na Mapema...Yaani Mtu anatuhumiwa kuchukua mke wa mtu na baadae anamuua mtu huyo huu upuuzi kabisa.
Mwenyewe nimekuwa na mashaka na aina ya huyo polisi asee.Askari wenye mafunzo ya kijeshi na wana bunduki wanashindwa vipi ku neutralize raia mwenye panga mpaka wampige risasi ya kifua?
Hii haiingii akilini kabisa kwa mtu mwenye kujielewa.
Basi sawa[emoji111]Sijajiapiza kwa sbb pia ni dhambi kwa imani yangu. Ila uamuzi ni wangu so nikisema nimesema na sifutiiii¹
Sometimes akili za wanawake tatizo alivurugwa akili na hawara ni habari ya muda tu polisi atakula Kona yy atabaki na makalio yakeIshapigwa chenga matata hapo Askari hana hatia.
Apumzike kwa amani, Paulina huo ni msalaba wake.
Sababu mke wa MTU hana gharama zaidi ya Nauli nakulipia guest tuMkuu na hali halisi ni kuwa hata kama polisi alikuwa anachepuka na huyo mke wa mtu ataanza kumkwepa sasa baada ya kuwa mjane. Sijui hili jambo huwa lina siri gani lakini mara nyingi mwanamke ''anapendeka'' anapokuwa kwenye ndoa lakini mara akiachika wanaume wanaanza kumpiga chenga.
Hamna kesi hapo umeelewa hiyo statement ya Polis wa ArushaKama ni kweli alikuwa anataka kuwakata na panga hapo ni wazi hiyo ni kesi ya mauaji pasipo kukuudia wakati mtu anashambuliwa
Kweli kuna kipindi hata uwe mtu mzima akili hufika mwisho mapenzi ya kuwekana ndani polis ujue ndoo kikomoSasa Kama hakupendi unamlazimisha?
Uwe kijana,uwe mtu mzima mapenzi yakisha Isha Basi Tena,wanawake hawajawahi kueleweka.
Kama hutaki unaacha.
Huyo polisi nae alievurugwa na hawara hana tatizo?Sometimes akili za wanawake tatizo alivurugwa akili na hawara ni habari ya muda tu polisi atakula Kona yy atabaki na makalio yake
Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Amini kwamba nimepiga juzi haijapatikana.ipo hewan mbona. Ccpinye unazngua
Nitumie yako pm mzeeAmini kwamba nimepiga juzi haijapatikana.
Kwa nini umehifadhi jina la muuaji we ni bure kabis shwainiPolisi wa kituo cha Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wanadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi kati ya mke wa marehemu na askari polisi.
Habari kutoka kwa ndugu na majirani wa marehemu zilisema kuwa tukio hilo limetokea aprill 12 mwaka huu majira ya saa 1.35 usiku katika mtaa wa sabasaba kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.
Vyanzo vilisema kuwa siku ya tukio ya marehemu alikuwana ugomvi na mke wake, Paulina Kiliani{37} na kumlalamikia mke wake kuwa sio mwaminifu katika ndoa akimtuhumu kuwa na mahusiano na askari polisi aliyefanya mauaji {jina linahifadhiwa} kuwa ndio mvunja ndoa yake.
Vyanzo vya habari viliendelea kusema kuwa siku ya mauaji marehemu na mke wake walikuwa na ugomvi mkubwa na kufikia hatua ya kupigana na mke alimpigia simu ya kiganjani askari polisi huyo na kumwelezea kupigwa kwake na mume wake na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio.
Habari zilisema kuwa baada ya marehemu kumwona askari yule yule anayemtuhumu kufanya mapenzi na mke wake akiwa wa kwanza kufika eneo la tukio,marehemu kwa hasira huku akiongea kwa jazba kuwa wewe ndio niliyekuwa nakutafuta ghafla aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua panga kwa nia ya kumtishia askari huyo akiwa na mwenzake ili aondoke eneo la tukio.
Vyanzo vilisema kuwa kabla ya marehemu kufanya tukio la kutaka kumkata Askari huyo,ghafla askari huyo alifyatua risasi na kumpiga marehemu kifuani kushoto na mguuni na kufariki dunia papo hapo.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo imesema kuwa NASIELI alijeruhiwa kwa risasi upande wa kushoto wa mguu na kwenye bega la mkono wa kushoto baada ya kukaidi amri halali ya askari Polisi ya kukamatwa na kutaka kumkata askari panga alilokuwa nalo mkononi mwake.
Kamanda aliendelea kueleza katika taarifa yake kuwa marehemu alikuwa amewafungia watoto wake na mtoto wa jirani yake ndani ya nyumba kwania ya kuwadhuru na baada ya kutoa taarifa askari waliamua kwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto lakini pia kumkamata mtuhumiwa.
Taarifa ilisema baada ya kufika eneo la tukio walianza kugonga mlango uliokuwa umefungwa ili kuokoa watoto waliokuwa hatarini wakati wanaokoa watoto hao nje ya nyumba hiyo walimwona mtuhumiwa huyo akiwa amejificha akiwa ameshika panga Mkononi huku akiwa fuata askari hao kwa lengo la kuwadhuru.
Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipoamua kumpiga risasi kwenye bega lake la kushoto hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kisha kupelekwa katika hospital ya wilaya ya Monduli na mtuhumiwa huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.
Ends...
=====
POLISI wa Kituo Kikuu cha Wilaya ya Monduli mkoani Arusha, anadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli katika mazingira yanayohusishwa na mapenzi. Majirani na ndugu wa marehemu wanadai kuwa, tukio hilo lilitokea Aprili 12 mwaka huu saa 1.35 usiku katika Mtaa wa Sabasaba, Kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.
Inadaiwa kuwa siku ya tukio, Nasieli alikuwa na ugomvi na mkewe, Paulina Kiliani (37), akimtuhumu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na polisi aliyedaiwa kuua (jina linahifadhiwa).
Kwa mujibu wa vyanzo, siku ya tukio Nasieli aligombana na mkewe hadi wakapigana na ndipo Paulina akampigia simu ya kiganjani polisi huyo kumpa taarifa kuwa amepigwa na mumewe.
Alielezwa kuwa, baada ya kupata taarifa hizo, askari huyo na mwenzake wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio. Inadaiwa kuwa baada ya Nasieli kumwona polisi anayemtuhumu kuwa na uhusiano na mkewe, alizidi kukasirika na kuongea kwa jazba kisha akaingia ndani kuchukua panga kwa lengo la kumdhuru askari polisi huyo.
Vyanzo vya habari vinadai kuwa kabla ya Nasieli kutimiza lengo lake, askari polisi huyo alimpiga risasi kifuani upande wa kushoto na mguuni na Nasieli akafa papo hapo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Justine Masejo, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema Nasieli alijeruhiwa kwa risasi mguu wa kushoto na kwenye bega la mkono wa kushoto.
Taarifa ya Kamanda Masejo ilieleza kuwa, raia huyo alikaidi amri ya polisi ya kutaka kumkamata na alitaka kumkata askari kwa panga alilokuwa nalo mkononi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Paulina ni mfanyabiashara na anaishi eneo la Sabasaba. Kamanda Masejo alieleza kuwa, awali mama huyo alifika Kituo cha Polisi akamtambulisha Nasieli kuwa ni mpenzi wake na kufungua kesi dhidi ya Nasieli ya kutolewa lugha ya matusi.
Alieleza kuwa, mchana wa siku ya tukio, mlalamikaji alirudi tena katika kituo cha Polisi akidai kuwa mpenzi wake alimpiga na kumsababishia majeraha kwenye kidole na sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kamanda Masejo alieleza kuwa, Nasieli pia aliwafungia wanawe na mtoto wa jirani ndani ya nyumba kwa nia ya na kuwadhuru na baada ya Polisi kupata taarifa walikwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto na kumkamata mtuhumiwa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, baada ya kufika eneo la tukio waligonga mlango uliokuwa umefungwa na wakati wanaokoa watoto, walimuona Nasieli akiwa amejificha akiwa na panga mkononi na akafuata askari kwa lengo la kuwadhuru.
Alieleza askari hao walimuamuru Nasieli asimame, lakini hakutii na aliendelea kuwafuata akiwa amenyanyua panga. Kwa mujibu wa kamanda huyo, askari hao walirudi nyuma mitaa kadhaa, lakini Nasieli aliendelea kuwafuata na askari walianza kukimbia, wakapotezana na mtuhumiwa akawa anamfukuza askari polisi mmoja.
Alisema askari polisi aliyekuwa akikimbizwa alipiga risasi mbili juu ili mtuhumiwa asimame, lakini alizidi kumfuata hivyo akampiga risasi mguu wa kushoto, lakini Nasieli alizidi kumsogelea askari ambaye kwa wakati huo alikuwa ameanguka.
Kiongozi huyo wa polisi alisema Nasieli alimfikia askari polisi na alitaka kumnyang’anya silaha aina ya SMG. Kamanda Masejo alieleza kuwa katika purukushani hiyo, polisi alimpiga risasi Nasieli kwenye bega la kushoto akavuja damu nyingi.
Kwa mujibu wa Polisi, Nasieli aliaga dunia wakati akipata tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Chanzo: Habari leo
Ukibaini mke si mwaminfu katika ndoa, uamuzi ni kukaa pembeni kuepusha msongamano. Vinginevyo utapata matatizo au kifo.Polisi wa kituo cha Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha wanadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi kati ya mke wa marehemu na askari polisi.
Habari kutoka kwa ndugu na majirani wa marehemu zilisema kuwa tukio hilo limetokea aprill 12 mwaka huu majira ya saa 1.35 usiku katika mtaa wa sabasaba kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.
Vyanzo vilisema kuwa siku ya tukio ya marehemu alikuwana ugomvi na mke wake, Paulina Kiliani{37} na kumlalamikia mke wake kuwa sio mwaminifu katika ndoa akimtuhumu kuwa na mahusiano na askari polisi aliyefanya mauaji {jina linahifadhiwa} kuwa ndio mvunja ndoa yake.
Vyanzo vya habari viliendelea kusema kuwa siku ya mauaji marehemu na mke wake walikuwa na ugomvi mkubwa na kufikia hatua ya kupigana na mke alimpigia simu ya kiganjani askari polisi huyo na kumwelezea kupigwa kwake na mume wake na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio.
Habari zilisema kuwa baada ya marehemu kumwona askari yule yule anayemtuhumu kufanya mapenzi na mke wake akiwa wa kwanza kufika eneo la tukio,marehemu kwa hasira huku akiongea kwa jazba kuwa wewe ndio niliyekuwa nakutafuta ghafla aliingia ndani ya nyumba yake na kuchukua panga kwa nia ya kumtishia askari huyo akiwa na mwenzake ili aondoke eneo la tukio.
Vyanzo vilisema kuwa kabla ya marehemu kufanya tukio la kutaka kumkata Askari huyo,ghafla askari huyo alifyatua risasi na kumpiga marehemu kifuani kushoto na mguuni na kufariki dunia papo hapo.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ambapo imesema kuwa NASIELI alijeruhiwa kwa risasi upande wa kushoto wa mguu na kwenye bega la mkono wa kushoto baada ya kukaidi amri halali ya askari Polisi ya kukamatwa na kutaka kumkata askari panga alilokuwa nalo mkononi mwake.
Kamanda aliendelea kueleza katika taarifa yake kuwa marehemu alikuwa amewafungia watoto wake na mtoto wa jirani yake ndani ya nyumba kwania ya kuwadhuru na baada ya kutoa taarifa askari waliamua kwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto lakini pia kumkamata mtuhumiwa.
Taarifa ilisema baada ya kufika eneo la tukio walianza kugonga mlango uliokuwa umefungwa ili kuokoa watoto waliokuwa hatarini wakati wanaokoa watoto hao nje ya nyumba hiyo walimwona mtuhumiwa huyo akiwa amejificha akiwa ameshika panga Mkononi huku akiwa fuata askari hao kwa lengo la kuwadhuru.
Alisema baada ya hali hiyo ndipo alipoamua kumpiga risasi kwenye bega lake la kushoto hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na kisha kupelekwa katika hospital ya wilaya ya Monduli na mtuhumiwa huyo alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.
Ends...
=====
POLISI wa Kituo Kikuu cha Wilaya ya Monduli mkoani Arusha, anadaiwa kumpiga risasi raia aliyetambuliwa kwa jina la Yohana Nasieli katika mazingira yanayohusishwa na mapenzi. Majirani na ndugu wa marehemu wanadai kuwa, tukio hilo lilitokea Aprili 12 mwaka huu saa 1.35 usiku katika Mtaa wa Sabasaba, Kata ya Monduli Tarafa ya Kisongo wilayani humo.
Inadaiwa kuwa siku ya tukio, Nasieli alikuwa na ugomvi na mkewe, Paulina Kiliani (37), akimtuhumu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na polisi aliyedaiwa kuua (jina linahifadhiwa).
Kwa mujibu wa vyanzo, siku ya tukio Nasieli aligombana na mkewe hadi wakapigana na ndipo Paulina akampigia simu ya kiganjani polisi huyo kumpa taarifa kuwa amepigwa na mumewe.
Alielezwa kuwa, baada ya kupata taarifa hizo, askari huyo na mwenzake wakiwa na silaha walikwenda eneo la tukio. Inadaiwa kuwa baada ya Nasieli kumwona polisi anayemtuhumu kuwa na uhusiano na mkewe, alizidi kukasirika na kuongea kwa jazba kisha akaingia ndani kuchukua panga kwa lengo la kumdhuru askari polisi huyo.
Vyanzo vya habari vinadai kuwa kabla ya Nasieli kutimiza lengo lake, askari polisi huyo alimpiga risasi kifuani upande wa kushoto na mguuni na Nasieli akafa papo hapo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Justine Masejo, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema Nasieli alijeruhiwa kwa risasi mguu wa kushoto na kwenye bega la mkono wa kushoto.
Taarifa ya Kamanda Masejo ilieleza kuwa, raia huyo alikaidi amri ya polisi ya kutaka kumkamata na alitaka kumkata askari kwa panga alilokuwa nalo mkononi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Paulina ni mfanyabiashara na anaishi eneo la Sabasaba. Kamanda Masejo alieleza kuwa, awali mama huyo alifika Kituo cha Polisi akamtambulisha Nasieli kuwa ni mpenzi wake na kufungua kesi dhidi ya Nasieli ya kutolewa lugha ya matusi.
Alieleza kuwa, mchana wa siku ya tukio, mlalamikaji alirudi tena katika kituo cha Polisi akidai kuwa mpenzi wake alimpiga na kumsababishia majeraha kwenye kidole na sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kamanda Masejo alieleza kuwa, Nasieli pia aliwafungia wanawe na mtoto wa jirani ndani ya nyumba kwa nia ya na kuwadhuru na baada ya Polisi kupata taarifa walikwenda eneo la tukio kwa nia ya kuwaokoa watoto na kumkamata mtuhumiwa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, baada ya kufika eneo la tukio waligonga mlango uliokuwa umefungwa na wakati wanaokoa watoto, walimuona Nasieli akiwa amejificha akiwa na panga mkononi na akafuata askari kwa lengo la kuwadhuru.
Alieleza askari hao walimuamuru Nasieli asimame, lakini hakutii na aliendelea kuwafuata akiwa amenyanyua panga. Kwa mujibu wa kamanda huyo, askari hao walirudi nyuma mitaa kadhaa, lakini Nasieli aliendelea kuwafuata na askari walianza kukimbia, wakapotezana na mtuhumiwa akawa anamfukuza askari polisi mmoja.
Alisema askari polisi aliyekuwa akikimbizwa alipiga risasi mbili juu ili mtuhumiwa asimame, lakini alizidi kumfuata hivyo akampiga risasi mguu wa kushoto, lakini Nasieli alizidi kumsogelea askari ambaye kwa wakati huo alikuwa ameanguka.
Kiongozi huyo wa polisi alisema Nasieli alimfikia askari polisi na alitaka kumnyang’anya silaha aina ya SMG. Kamanda Masejo alieleza kuwa katika purukushani hiyo, polisi alimpiga risasi Nasieli kwenye bega la kushoto akavuja damu nyingi.
Kwa mujibu wa Polisi, Nasieli aliaga dunia wakati akipata tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Chanzo: Habari leo
Askari na mwenza!!!?na askari huyo akiwa na mwenza wakiwa na silaha
Wanafunzi
Unafki at work ha ha Ila majitu myeusi tuna shida sanaWazee wa hashtag # Black nini nini siijui
Ova
Hehehe hii naona wako kimyaUnafki at work ha ha Ila majitu myeusi tuna shida sana
Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app