ARUSHA: Wafanyakazi Naura Hotel na Impala waandamana kwa Mabango kuilalamikia Mahakama

ARUSHA: Wafanyakazi Naura Hotel na Impala waandamana kwa Mabango kuilalamikia Mahakama

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2016
Posts
753
Reaction score
1,812
Wafanyakazi zaidi ya 200 wa hotel za Naura Spring na Impala za jijini Arusha wameandamana katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakilalamikia mwenendo mbaya wa mashauri yao ya madai yaliyopo mahakamani unaolenga kuchelewesha haki ya kulipwa Madai yao yanayofikia kiasi cha sh,milioni 700.

Wafanyakazi hao waliokuwa na mabango yenye jumbe mbalimbali walitinga ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Arusha majira ya saa Tisa alasiri wakitokea katika mahakama Kuu Kanda ya Arusha Masijala ndogo ya kazi kusikiliza shauri lao la madai ambapo wakimtuhumu mahakama hiyo kujaa Rushwa na kushindwa kuwatendea haki.

Hata hivyo baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa shauri hilo lililopo mbele ya Jaji Mohamed Gwai ambaye aliahiridha Kesi hiyo hadi June 28 na Mei 20 mwaka.huu, wafanyabiashara hao walihamasishana na kuandamana kuelekea ofisi ya mkuu wa Mkoa wa ARUSHA.

IMG_20210510_140006_257.jpg
 
'Wafanyakazi zaidi ya 200 wa hotel za Naura Spring na Impala za jijini Arusha wameandamana'.

'wafanyabiashara hao walihamasishana na kuandamana kuelekea ofisi ya mkuu wa Mkoa wa ARUSHA.'

Wafanyakazi vs wafanyabiashara.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kwamba mkuu wa mkoa ataikomandi mahakama au?
 
Kwa nini lkn hawa watu wanazungushwa?

Mbona muda mrefu kwa nini?

Wapeni haki zao acheni kuwachelewesha.
 
Kwani DC Muro anasemaje?
Muro ni wa Arumeru sio Manispaa ya Arusha mjini ilipo Naura Spring, kwahiyo hausiki na hili

Kifupi ni kuwa migogoro ni mikubwa katika hoteli zote za Marehemu Mrema na watoto wake hawaelewani tena, wanadaiwa sana na wamefulia

Balaa tupu, ni kama tu kwa Mzee Mollel (Black toto)
 
Back
Top Bottom