ARUSHA: Wawili wanaswa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin gramu 70.77

ARUSHA: Wawili wanaswa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin gramu 70.77

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia mfanyabiashara Abdi Hamis (27) mkazi wa Ngarenaro na Ally Said (25) dereva na mkazi wa Olasiti baada ya kukamatwa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin gramu 70.77 kwa kutumia gari Na. T 949 DQA lenye tela Na. T. 253 CXR.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Justine Masejo amesema uchunguzi wa awali wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa watuhumiwa hao wamekuwa wakijihusisha na biashara hiyo haramu kwa muda mrefu na walikuwa wakifuatiliwa.

Aidha jeshi bado linaendelea kuwashikilia watuhumiwa hao pamoja na gari hilo mpaka upelelezi utakapokamilika.

Heroin.jpg
 
Muda mrefu ndio mkamate gramu najua mtawafunga maisha hao machalii still sio solution!
 
Hizo gram 70 itakuwa walikuwa wanajidunga wenyewe tu wakiwa safarini
 
Bila kuwa na side hustle tutakula wali bila mafuta au chai bila sukari. Kila kitu bei juu. Tufanyaje ss
 
Yaani Hilo Benz ndiyo lilikuwa linasafirisha gramu 70.77? siyo kilo 70 ni gramu 70 ambayo ni sawa na ganda la kiberiti?

Sasa sijui wanalishikia kwa ajili ya nini..??? nadhani hio kesi hao Dereva na tingo wake wanaweza kuwa na majibu sahihi... Endapo tu Mmiliki atathibitisha kuwa hauhisiki na huo unga..

Ila Askari wa SIrro sasa ndio wataona pa kupatia hela za kujengea hapo
 
Trafiki walijuaje kwamba kulikuwepo na unga? Isije ikawa mambo ya tii Sheria bila shurutiii
 
Back
Top Bottom