Asante kwa msaada wenu madr wa JF(Feedback)

Asante kwa msaada wenu madr wa JF(Feedback)

Bado Safari ni ndefu sana MadamG.miezi tisa kitaalam tunasema ni kama wiki 40 au siku 280.
Tunafurahia kusikia kwamba umekuwa mjamzito,ila bado mapema sana kutabiri chochote mpaka uvuke salama miezi mitatu ya mwanzo.
Ndiyo maana watu wengi huwa wanafanya siri mpaka wavuke miezi mitatu, kwa kuwa kuna changamoto nyingi katika miezi mitatu ya mwanzo.
Mara nyingi katika wiki 8 za mwanzo chochote kikienda wrong mimba huporomoka(abortion).
Jitahidi sana kula mboga za majani kwa wingi, matunda na protein.
Hizo chips hazilipi kabisa. unakosa virutubisho vingine muhimu.na je unazitengeneza mwenyewe au ni zile zinazochemshwa na mafuta ya kupozea transforma?
Maelekezo mengine umeshapewa na MziziMkavu.
Usipende kunywa dawa zozote bila maelekezo ya madaktari, na hasa dawa ambazo ni ANTI-Folate kama vile Fansidar, septrin, na zingine.Dawa hizi zinaingilia uumbaji wa mtoto kwa kuuzuia mwili usiweze kutumia FOLIC ACID na kusababisha ulemavu kama huu hapa:
M3500133-Newborn_child_with_spina_bifida.-SPL.jpg

kunywa maziwa kwa wingi ili upate calcium suppliments, daktari wako atakushauri kumeza folic acid na hasa kipindi hiki cha miezi mitatu ya mwanzo ili kuwe na ukamilifu kwenye uumbaji wa viungo vya mtoto.
Najua uko excited kujua mambo mengi kuhusu ujauzito.unapohitaji ushauri be free kutu-inbox nasi tuta-respond immediately.
 
Last edited by a moderator:
Watu8 na wewe ni Dr? anyway hongera kwa ushauri hadi madam amepata ujauzito. mimba ina wiki...... siwezi kutoa ushauri wowote atleast ifikishe mwezi lol! hukawii kusema una mimba mara wageni wakaja lol!

Nilidhani niko peke yangu kwenye doubts za udaktari wa watu8.
 
Last edited by a moderator:
big up Mzizi mkavu kwa ma point. Hongera mama K wetu MadamG.. Mungu akulinde wewe na kijacho.
 
Last edited by a moderator:
Bado Safari ni ndefu sana MadamG.miezi tisa kitaalam tunasema ni kama wiki 40 au siku 280.
Tunafurahia kusikia kwamba umekuwa mjamzito,ila bado mapema sana kutabiri chochote mpaka uvuke salama miezi mitatu ya mwanzo.
Ndiyo maana watu wengi huwa wanafanya siri mpaka wavuke miezi mitatu, kwa kuwa kuna changamoto nyingi katika miezi mitatu ya mwanzo.
Mara nyingi katika wiki 8 za mwanzo chochote kikienda wrong mimba huporomoka(abortion).
Jitahidi sana kula mboga za majani kwa wingi, matunda na protein.
Hizo chips hazilipi kabisa. unakosa virutubisho vingine muhimu.na je unazitengeneza mwenyewe au ni zile zinazochemshwa na mafuta ya kupozea transforma?
Maelekezo mengine umeshapewa na MziziMkavu.
Usipende kunywa dawa zozote bila maelekezo ya madaktari, na hasa dawa ambazo ni ANTI-Folate kama vile Fansidar, septrin, na zingine.Dawa hizi zinaingilia uumbaji wa mtoto kwa kuuzuia mwili usiweze kutumia FOLIC ACID na kusababisha ulemavu kama huu hapa:
M3500133-Newborn_child_with_spina_bifida.-SPL.jpg

kunywa maziwa kwa wingi ili upate calcium suppliments, daktari wako atakushauri kumeza folic acid na hasa kipindi hiki cha miezi mitatu ya mwanzo ili kuwe na ukamilifu kwenye uumbaji wa viungo vya mtoto.
Najua uko excited kujua mambo mengi kuhusu ujauzito.unapohitaji ushauri be free kutu-inbox nasi tuta-respond immediately.
nashukuru kwa ushauri
 
Kumuona Daktari

Daktari wako atapanga miadi kwa muda wa miezi tisa ili kuhakikisha wewe na mwanao mna rai. Mimba hukaa kwa muda wa wiki 40 (kutoka wakati wa hedhi ya mwisho) na hugawanywa kwa awamu tatu. Awamu ya kwanza huwa ya wiki 12, ya pili wiki 15 na ya tatu wiki 13.

Miadi hii ili kuhakikisha mimba iliyo na afya huwa:

  • Siku moja kwa miezi katika miezi ya kwanza sita.
  • Siku moja kila wiki mbili kutoka mwezi wa saba hadi wa nane (7-8)
  • Mara moja kwa wiki hadi wakati wa kujifungua.

Kufuata miadi hii huwa muhimu sana, hata kama wajihisi mzima, Hivyo, daktari wako anaweza kuchukua hatua kama wewe na mwanao mna matatizo.

Katika miadi ya kwanza na daktari wako, daktari atakuuliza kuhusu afya yako na historia ya familia yako na atakupima damu na mkojo pia. Kama una ugonjwa wowote kama, kupandwa na damu, shida za moyo na mishipa ama ugonjwa mwingine wowote, usisahau kumwambia daktati wako kama ni za kununua dukani). Haya ni mambo unayofaa kujulisha daktari wako kwani yanaweza kuadhiri mtoto wako, hivyo jaribu kumweleza wasiwasi.

Daktari wako atakufanyia uchunguzi kama wa urefu, uzito na viungo vilivyo karibu na nyonga. Baada ya miadi hii, unafaa kuwa na wazo la lini utajifungua.

Miada mingine huchukua muda mfupi lakini daktari atachunguza mwendo wa damu yako, mkojo na uzito. Uchunguzi mwingine ni kama wa kasoro za kuridhi au kasoro zinginezo. Ili kujua jinsi mwanao anakua, unaweza kufanyiwa uchunguzi awa ultrasound: Kumbuka kumwambia daktaari mabadiliki ambayo umapata/umeona kutoka wakati wa miadi ya awali. Pigia daktari wako simu kama umepata matatizo yoyote katikati ya miadi.


Unayafaa kujiepusha nayo


Usijiweke hatarini wakati wa mimba. Tumia wakati huu kufanya mabadiliko fulani maishani yako:

  • Acha kuvuta sigara* - uvutaji wa sigara wakati wa mimba huongezea hatari ya kuharibu mimba, kujifungua kabla ya wakati ufaao, kuzaa mtoto aliye na uzito mdogo isivyotarajiwa, SIDS na matatizo mengine.
  • Usinywe pombe – unywaji pombe wakati wa mimba huweza kusababisha kasoro ambazo haziwezi kuzuilika kama kupungukiwa na akili.
  • Usitumie dawa za kulevya – Bangi, Cocaine, Heroin, Speed, PCP na dawa zingine za kulevya zaweza kusababisha kuharibika kwa mimba, kuzaa kabla ya wakati ufaao na kasoro zingine. Mtoto anaweza pia kupata matatizo ya kusoma (kuelewa) na anaweza kuzaliwa akiwa mzoevu* kwa dawa hizi ongea na daktari wako kama wataka kuacha kutumia dawa hizi.
  • Punguza au acha kutumia kafeini ipatikanayo katika kahawa, chai, vinywaji ‘chocolate’ na dawa ziuzwazo dukani.
  • Usikule samaki, kuku au nyama nyingine ya mnyama kama haijaiva vizuri.
  • Jiepushe na kemikeli zenye sumu kama kuua za wadudu, rangi, vyuma kama lead na mercury.(Bidhaa nyingi za nyumbani zilo na tahadhari kwa walio na mimba) Bidhaa hizi kama hauna uhakika.
  • Jiepushe na ‘bafu ya pipa’ (tub) na ‘Saunas’ za maji moto. Hizi huongezea hatari ya kuharibika kwa mimba na kasoro zingine za uzazi.
  • Usioshe au kushika kisanduku cha paka wako. Hili linaweza kuambukiza maradhi yanayoweza kusababisha kasoro za uzazi. Pia valia vifuko vya mikono (gloves) unapofanya kazi shambani au mahali paka wako huwa Madam G
Ninakutakia kila la kheri mimba yako ikuwe kwa salama akuwe mtoto mwema mwenye kukusikiliza wewe mama yake inshallah.

Asante sana
 
Munamsahau Mupirocin amewapa formula nzuri sana ya namna ya kupata mimba coz mzizimkavu nakumbuka alikuwa amekosea hata formula na mupirocin akamrekebisha, sijui labda ulitumia njia ipi.
Lakini tunashukuru kwa feedback coz wapo wanawake wengi hata wasomi hawajui siku za kupata mimba, wanagegedana tu bila mpangilio
Hatujamsahau ndugu ndio maana ukisoma vizuri nimetaja na wengineo wote walionipa ushauri najua wapo wengi na nakumbuka chaleng yake ilijenga na mi nikaelewa zaidi
 
Kazi kweli kweli..mwenye mbuzi kashindwa kujua mbuzi ale nini ili anenepe...
majani mengine hayanenepeshi mpaka uwaone wataalamu au we mwenzetu ni mtaalamu wa kila sekta dr, mwl wewe?
ukiwa na mtoto wako unamsomesha mwenyewe kwasababu ni wako na ukiumwa unajitibu kwasababu ni ugonjwa wako, je kama unaumwa sikio na wewe udr wako umesomea jicho utajitibu tu kwasababu unaumwa wewe? siokila unachokijua na mwenzio anajua ndugu ila ongera coz umejitosheleza.
 
Watu8 na wewe ni Dr? anyway hongera kwa ushauri hadi madam amepata ujauzito. mimba ina wiki...... siwezi kutoa ushauri wowote atleast ifikishe mwezi lol! hukawii kusema una mimba mara wageni wakaja lol!
ha ha ha haaa. mimba ya wiki moja,loh!
 
Back
Top Bottom