Wamepita Marais wengi hapa Tanzania lakini ni Rais Samia mtoto wa Ardhi ya Kizimkazi ndio ameutendea Haki Mkoa wa Mbeya kulingana na hadhi yake.
Ilikuwa ni Kilio Cha mda mrefu Kwa Wana Mbeya ambacho hakuna aliyekisikia isipokuwa huyu mwanamke Rais Samia.
Umefanya mambo mengi sana ya kuacha alama Mkoani Mbeya,miongoni mwayo ni
1. Ujenzi wa Barabara ya Tanzam njia 4
2. Ujenzi wa Mradi mkubwa wa Maji mto Kiwira
3. Ujenzi wa Barabara za lami za Mitaa km 15
4. Ukamilishaji wa uwanja wa ndege wa Songwe na kuanza kujenzi wa cold room
5. Kuanza ujenzi wa uwanja wa Maonesho ya Kilimo 8/8 kuwa wa Kimataifa
6. Pamoja na miradi hiyo mikubwa ila kubwa kuliko ni hili la Stendi kuu ya Mkoa
My Take
Mungu azidi kukupa hekima na maisha marefu uje utujengee na uwanja mkubwa wa mpira maana watu wa Mbeya ni wanamichezo mahiri.
Tutasimulia Wajukuu alikuwepo Samia aliipa heshima Mbeya 🙏🙏
Pia soma
Idadi ya miradi mikubwa inayotekelezwa na Rais Samia mkoani Mbeya