Asante sana Trump kwa kuliweka hili wazi wazi kwamba katika vita yoyote anatanguliza maslahi ya Marekani

Asante sana Trump kwa kuliweka hili wazi wazi kwamba katika vita yoyote anatanguliza maslahi ya Marekani

eliakeem

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2009
Posts
17,214
Reaction score
15,853
Miaka mingi iliyopita, watu wengi walifikiri kwamba MArekani anapigana vita ili kulinda amani, demokrasia au kuwaokoa watu/nchi fulani kutoka katika ukandamizaji. Ilijipambanua kwamba yenyewe haitangulizi masirahi yake, badala yake inapambania utu, ubinadamu, haki na mali za wale wote wanaoonewa.

Sasa kinachoendelea Ukraine ni tofauti kabisa. Ukweli ni kwamba iliingia kuisaidia Ukraine siyo kuilinda dhidi ya uvamizi wa Urusi, bali kama muwekezaji yeyote ambaye aliona fursa ilioko mbeleni. Kwamba vita inayoendelea katika taifa hilo, siku za usoni itakuwa ni neema kwa Marekani.

Imekuwa kweli. Sasa marekani kwa uwazi kabisa anamdai Ukraine kwamba waingie mkataba wa makubaliano ya kuwa Marekani itanufaika na madini muhimu yanayopatikana humo. Haya yote yalikuwa yanafanyika miaka mingi sana huko nyumba.

Lakini yalikuwa hayawi wazi kama ilivyo sasa. Ndiyo maana nasema na kurudia tena, TUNAKUSHUKURU SANA TRUMP KWA KUYAWEKA HAYA WAZI.

SASA TUNAJUA FIKA KABISA KWAMBA HAKUNA KITU CHA BURE HAPA CHINI YA JUA.


1740560674190.png


 
Zamani hatukujua kwamba huyu mwamba marekani anajipambania maslahi yake anavyojihusisha na vita katika maeneo mbalimbali ulimwenguni. Tunamshukuru Trump mzee wa ukweli na uwazi ambaye hana chembe ya unafiki, kwa kuliweka hili bayana. Sasa ni rasmi kila tunapomuona marekani anang"ang"ana kujiingiza kwenye mizozo ni kwa sababu za kiuchumi.

CC: Yoda usirudie tena kumuita Trump mpuuzi. Unafikiri bila yeye mambo haya aliyoyaweka wazi tungeyajulia wapi?
 
Zamani hatukujua kwamba huyu mwamba marekani anajipambania maslahi yake anavyojihusisha na vita katika maeneo mbalimbali ulimwenguni. Tunamshukuru Trump mzee wa ukweli na uwazi ambaye hana chembe ya unafiki, kwa kuliweka hili bayana. Sasa ni rasmi kila tunapomuona marekani anang"ang"ana kujiingiza kwenye mizozo ni kwa sababu za kiuchumi.

CC: Yoda usirudie tena kumuita Trump mpuuzi. Unafikiri bila yeye mambo haya aliyoyaweka wazi tungeyajulia wapi?
waafrika wengi waliimbishwa mimbo ya ugaidi na demokrasia bila ya kujua mwenzao yupo kwenye kuangalia maslahi yake na siyo kuwatetea wao kama walibya walivyodanganywa
 
Kila nchi duniani lazima itangulize maslahi yake binafsi kwanza.

Sasa nashangaa waafrika wanao walaumu Marekani kuiba rasilimali za watu wengine.

Ukiwa mjinga na mpumbavu lazima rasilimali zako ziibwe maana umeshindwa kuzilinda na kuzitumia.

MAKE AMERICA GREAT AGAIN.

MAKE EUROPE GREAT AGAIN.

POOR AFRICA.
 
waafrika wengi waliimbishwa mimbo ya ugaidi na demokrasia bila ya kujua mwenzao yupo kwenye kuangalia maslahi yake na siyo kuwatetea wao kama walibya walivyodanganywa

Inasikitisha sana, miaka yote tulikuwa tukilielewa jambo hili kwa mbaali sana. Lakini sasa Trump Kaweka kila kitu hadharani
 
Kila nchi duniani lazima itangulize maslahi yake binafsi kwanza.

Sasa nashangaa waafrika wanao walaumu Marekani kuiba rasilimali za watu wengine.

Ukiwa mjinga na mpumbavu lazima rasilimali zako ziibwe maana umeshindwa kuzilinda na kuzitumia.

MAKE AMERICA GREAT AGAIN.

MAKE EUROPE GREAT AGAIN.

POOR AFRICA.

Katika kipindi ambacho Afrika inabidi ijitambue ndiyo sasa. Lakini cha kusikitisha bado hatujielewi
 
Ninashawishika kuamini kuwa vita ya Urusi na Ukraine ulikuwa mpango wa Us na Urusi
 
Marekani kusema inatanguliza maslahi yake ni neno pana sana japo wengi mmelichukulia kwenye mrengo wa kiuchumi au mali zaidi.

Maslahi ya marekani ni pamoja na usalama wa raia wake na washirika wake muhimu. Na hakuna nchi ambayo haipiganii maskahi ukiacha vichwa maji wa Afrika.
Ukitaka kujua hilo angalia waliyo nyuma ya vita ya Sudan na Somalia.
Hata hivyo kauli hiyo haiondoi ukweli kwamba vikundi kama ISIS, Hizbollah, Hamas n.k ni magaidi.
ISis ni magaodi haswa na wenye akili wote wanajua ni tawi la mossad kasoro watu kama wewe ambao wanasubiri kauli ya trump
 
Miaka mingi iliyopita, watu wengi walifikiri kwamba MArekani anapigana vita ili kulinda amani, demokrasia au kuwaokoa watu/nchi fulani kutoka katika ukandamizaji. Ilijipambanua kwamba yenyewe haitangulizi masirahi yake, badala yake inapambania utu, ubinadamu, haki na mali za wale wote wanaoonewa.

Sasa kinachoendelea Ukraine ni tofauti kabisa. Ukweli ni kwamba iliingia kuisaidia Ukraine siyo kuilinda dhidi ya uvamizi wa Urusi, bali kama muwekezaji yeyote ambaye aliona fursa ilioko mbeleni. Kwamba vita inayoendelea katika taifa hilo, siku za usoni itakuwa ni neema kwa Marekani.

Imekuwa kweli. Sasa marekani kwa uwazi kabisa anamdai Ukraine kwamba waingie mkataba wa makubaliano ya kuwa Marekani itanufaika na madini muhimu yanayopatikana humo. Haya yote yalikuwa yanafanyika miaka mingi sana huko nyumba.

Lakini yalikuwa hayawi wazi kama ilivyo sasa. Ndiyo maana nasema na kurudia tena, TUNAKUSHUKURU SANA TRUMP KWA KUYAWEKA HAYA WAZI.

SASA TUNAJUA FIKA KABISA KWAMBA HAKUNA KITU CHA BURE HAPA CHINI YA JUA.


View attachment 3250217

Mkuu hakuna kipya wala cha ajabu alichosema Trump zaidi ya kuanika jazba zake na kutafuta umaarufu kwa watu duni (ignorant & gullible).

Halafu sio waafrika wote ni mazuzu. Mtu yeyote “aliyeenda shule” lazima afahamu kuwa nchi hutekeleza sera zao za mambo ya nje kwa maslahi yao.

Kuna wakati maslahi ya nchi huingiliana. Kwa mfano, Marekani inaweza kusaidia mapambano dhidi ya HIV/AIDS dunia nzima ili kupunguza maambukizi kwa raia wao wanaokula bata na watu wa dunia nzima ndani na nje ya US.

Katika tawala nyingine za US, hili la madini ya Ukraine lingejadiliwa kimya kimya na maelewano ya kiuwekezaji na kibiashara yangefikiwa kwa manufaa ya wote. Wanafanya hivyo dunia nzima na hayasikiki na wengi. Trump ni populist.

Trump anapayuka kila kitu ili kusikika na watu wa Marekani kuwa anawaletea faida. Bila shaka hatawaeleza undani wa dili hilo. Kwamba Marekani itawekeza kiasi gani, Ukraine watakuwa na mgao upi na Kwamba Marekani itawajibika kiasi gani katika ulinzi wa Ukraine.

Vile vile kama kawaida ya Trump, atajaribu kulazimisha makampuni yenye maslahi yake binafsi na mabilionea wenzake kina Musk yapewe kipaumbele kinyume cha sheria, kanuni na taratibu.

Kule sio kama Afrika ambako wanajichotea tu na kuacha mashimo na umasikini uliokithiri. Majadiliano (negotiations) ni serious business.
 
Miaka mingi iliyopita, watu wengi walifikiri kwamba MArekani anapigana vita ili kulinda amani, demokrasia au kuwaokoa watu/nchi fulani kutoka katika ukandamizaji. Ilijipambanua kwamba yenyewe haitangulizi masirahi yake, badala yake inapambania utu, ubinadamu, haki na mali za wale wote wanaoonewa.

Sasa kinachoendelea Ukraine ni tofauti kabisa. Ukweli ni kwamba iliingia kuisaidia Ukraine siyo kuilinda dhidi ya uvamizi wa Urusi, bali kama muwekezaji yeyote ambaye aliona fursa ilioko mbeleni. Kwamba vita inayoendelea katika taifa hilo, siku za usoni itakuwa ni neema kwa Marekani.

Imekuwa kweli. Sasa marekani kwa uwazi kabisa anamdai Ukraine kwamba waingie mkataba wa makubaliano ya kuwa Marekani itanufaika na madini muhimu yanayopatikana humo. Haya yote yalikuwa yanafanyika miaka mingi sana huko nyumba.

Lakini yalikuwa hayawi wazi kama ilivyo sasa. Ndiyo maana nasema na kurudia tena, TUNAKUSHUKURU SANA TRUMP KWA KUYAWEKA HAYA WAZI.

SASA TUNAJUA FIKA KABISA KWAMBA HAKUNA KITU CHA BURE HAPA CHINI YA JUA.


View attachment 3250217

Hivi angeendelea Biden haya tunayoyashuhudia kwa sasa yangetokea kweli?
 
Walichokifanya kwenye biashara kinaitwa Pivoting,
Original mission ilikua kuporomosha uchumi wa Urusi kwa kuitupa kwenye war of attrition walio i back up kwa ma billions ya dollars ya silaha za kijeshi, intelligence na vikwazo vya kiuchumi

Lengo ni kuchochoea mapinduzi Urusi ambayo yangemtoa V Putin madarakani na kuweka kibaraka wao, kwasababu waliamini uchumi wa Urusi unge collapse, wali overestimate nguvu yao ya kiuchumi wakasau Urusi ni mwanachma wa BRICS na BRICS wana account 37% ya Global economy (in PPP) ukilinganisha na G7 yenye 35%, plus BRICS ni 60%+ ya total world population, kwa maneno mengine BRICS ni matajiri kuliko Marekani na mashoga zake.

Baada ya kushindwa wameanza kubadili strategy, kwanza resources za Ukraine kwa ajili ya magari ya zezeta Elon Musk ambayo hayana uwezo tena wa ku compete na BYD bila direct colonialism

Pia fatilia maisha na maoni ya wananchi wa kawaida wa Marekani, maisha yao ni mazuri kwenye Hollywood na ya hovyo kwenye uhalisia, Trump na rais yoyote yule wa Marekani, ni mwakilishi tu wa daraja matajiri wachache Wamarekani wanaomiliki majority ya pato Marekani
Kwa mujibu wa takwimu zao wenyewe, Nusu ya Wamarekani wanamiliki 3% tu ya uchumi wa Marekani
Ni li nchi la mabeberu ambalo halina tena chembe yoyote ya maadili
 
Hili si la kuuliza. Kama yalivyokuwa mataifa na Dola kubwa zaidi ya US huko nyuma kanuni ni zile zile, hakuna cha wote, ni cha kwangu kwanza.
 
Hivi angeendelea Biden haya tunayoyashuhudia kwa sasa yangetokea kweli?

Kwa wale mababa wa unafiki na utapeli, hili lingekuwa tunalidhania tu. Tusingelijua kwa uwazi kama kwa huyu mwamba Trump ambaye hafichi mambo
 
Back
Top Bottom