Asanteni kwa mawazo yenu

Kwanza kabisa naweza hisi kwa nini mumeo ni mwenda nje. (upeo wako wa kufiri, kutambua na kupambanua mambo uko chini ya kiwango). hata maamuzi unayofanya ni kishetani zaidi kuliko maandiko matakatifu. Omba Mungu akupe hekima macho yako yaone mbali kwa imani.

Pole sana kwa kukosa busara.
 
<br /> <br /kosa la 3. kila mwaka unazaa hii ni hatar kwa afya yako na ya watoto. Tumia uzaz wa mpango
 
ndiyo wanajua yote lakini hawawezikuniingilia coz nilifanya ndoa kwa siri hata wao kujua kwa hiari yangu ndo mana leo yamenikuta&lt;br /&gt;<br /> &lt;br /&gt;
<br /> <br /kosa la 4. uliolewa bila ridhaa ya wazazi wako.
 
<br />
Khaaa! Sasa unachosubiri ni kutolewa roho au? Afu jamani swala la kuzaa au kutokuzaa mbona lipo ndani ya uwezo wako? Hivi kweli unashindwa kuzuia mimba? Mwanaume gani huyo wa kumzalia kila mwaka?..vinginevyo unamsingizia... Mambo mengine marahisi tu unayafanya kuwa magumu kwa mapenzi yako.. Penda unapopendwa mama, unachovumilia hasa ni nini hapo?..waeleze ndugu zako hali halisi ya ndoa yako, naamin watakusaidia hata kama ulifunga ndoa bila kuwajulisha watakusamehe.. Huyo mwanaume hana utu na usitegemee atabadilika.. Endelea kumzalia kila mwaka afu cha moto utakiona... Amini kuwa peke yako unaweza na utaweza kweli. Mtangulize mungu kwenye kila jambo na utafanikiwa... Jiamini, Amka, Unaweza!
 
kwa kweli ndugu zanguni mie ni mke wapili na kataka mwenyewe kunioa na pili mie msafi na nawaweka vizuri wanangu na mwenyewe niko fit slim na mzuri na kuhusu job siwezi coz mwanaume mwenyewe hataki nifanye kazi nikitoka nje pia hata dukani navaa ninja hata nyumbani wakija wanaume rafiki zake siruhusiwi kutoka nje ya chumba na tatu mie mwenyewe sasa sitaki kuzaa nataka niwekeshe kijiti cha mkono sijui nzuri manake mie niko ndani tu kama jela na mie namwachia mungu tu atampa lake mie sina la kumwambia basi tu roho inaniuma sana naungulika mwenzenu nipo naishi tu kama mjane mume wa jina huyu hata matumizi hanipi vizuri kunipa mimi anakuwa bahili niko miaka sita nae but mpaka leo sina akiba yoyote niponipo tu na lingine mwenyewe ameshaniambia baada ya mwaka mie niondoke zangu niishi navyojua mwenyewe kwa kweli mie naona ameshaoa au anataka kumuoa huyo mwanamke aliye nae dah mtihani huu mungu atanisaidia my destiny counts....
 
Nakupa pole saaana kwa matatizo na mikasa inayokukuta ndani ya ndoa yk, najua ni kiasi gani unaumia ukizingatia unampenda sana mumeo na yeye anakufanyia vituko na kukwambia lugha za kejeli na dharau, nyamaza ndgu yangu usilie tena km ni makosa ulishafanya na haya ni matokeo ya makosa, futa machozi na uwatazame wanao kwani watoto hao ndio wa muhimu kuliko mwanadamu yyt kwako. Ishi kwa ajili ya wanao na umtangulize mungu kwenye mambo yako, mwombe mungu akupe wepesi pia waombe wazaz na ndgu msamaha. Usilipe ubaya kwa ubaya piga moyo konde na mungu atakusaidia.
 
Maelezo yako yanakera, yanatia hasira na hayana maana kabisa. Naungana na aliyesema mumeo amekuona huna akili... Si uondoke hata leo sasahv? Unasubiri huo mwaka ili iweje??? Nna hakika hata mumeo anajuta kukuoa manake daaah! Unakera sio siri... Hata kama huna akili ya darasani na ya kuzaliwa pia umekosa jamani? Hebu acha kujifaoya unamwachia Mungu.. Fanya maamuzi na Mungu atakusimamia..
 
<br />
<br />
mama weeee! Sweetlady kapandisha mzuka.
 
Dada, mimi nakushauri ukamuona 'marriage councillor' au psychotherapist yeyote akusaidie. Hapa chuo kikuu wapo wataalamu watakusaidia, maana kwa kweli unatia huruma!
 
<br /> <br / ww pia ni mwanamke haya na makubwa zaid yanaweza kukukuta hvyo usimkashifu dada wa wa2 kumbuka yk kwnye wakat mgumu. Binafs nahisi ww huna akili ya kufikiri hata tone na km ungekua nayo usingesema tn kwa kujishebedua kw "maamuz yake ni ya kishetani ZAIDI KULIKO maandiko matakatifu" HUNA AKILI WALA HUJITAMBUI
 
sweetlady kuondoka rahisi dear lakini sharti lake unajua huyu bwana anasema watoto atawachukua na watoto wangu wote wa kike maskini nimewazaa kwa tabu na mama angu na ndugu zangu wote wamenisamehe mama angu ananiambia niachane nae ni mnyama huyu mara nyingi tu nimetolewa humu ndani nafukuzwa bila viatu kisa ukimtell kama y unarudi alfajiri
 
kweli dear mie siwezi kumfanyia ubaya nipo navumilia kwa ajili ya wanangu <br />
<br />
 
<br /> <br / anakupa masharti ya kuacha watoto wako ye nani?kwani hajui mtoto akizaliwa analindwa na sheria? Na Sheria iko wazi juu ya umri mtoto anaotakiwa aish chini ya uangalizi wa mama yake hvyo asikubabaishe nenda kwenye vyombo vya sheria watakusaidia.
 
kwanza huyu mtu nikimwambia kuhusu sheria anasema nenda tutafight na watoto atapata yeye dah yaani dunia naona chungu kwa tension brain inaacha kufanya kazi sasa siwezi kusahau nilikuwa na miezi minane mimba alinipiga sana mpaka mdomo ulivimba kama anavyopigwa mwiza alinipiga teke la nyuma mpaka haja ndogo ilinitoka dah halafu kunifanyia yote hayo akaniambia mie nakuacha wakati kosa analo yeye hamna mwanamke atakae vumilia kila siku mume kurudi alfajiri mie mpaka naona alama za makucha kwenye mwili wake ya mwanamke anavyoenda kukutana nae hivi nani ataweza kuvumilia halafu hana mda hata dk mbili aseme akae na mie aongee au ale chakula na mimi hamna niko alone tu na pia watoto hana mda nao yeye anawapenda sana marafiki zake ambao ndo malaya kishenzi watoto wakiumwa nihangaike mimi hata nikiwa niko hospitali nikienda kujifungua mume anakuwa hayupo mpaka napojifungua ndo anakuja kumwona mtoto
 
kwa kweli yapo mengi aliyonifanyia na bado ananifanyia sasa hata humu ndani hashindi siku zingine analala nje hata kula chakula hali even mwezi huu pia iko siku alirudi asubuhi ndo leo wiki ya tatu haongei na mimi niko niko tu but na mie nampuuza nishajua yupo na mwingine huyo na namwachia afanye tu nasubiria wanangu wakue kidogo nitamwachilia mbali niangalie maisha yangu
 
pole sana dada unayejiita usiye na bahati (unlucky)!

mi naona hapo ndipo penye kosa kubwa. hivi ni bahati gani unayoamni kuwa huna na unafikiri ungekuwa nayo mambo yako yangeenda vizuri?

napenda kukuambia kwa uwazi kuwa duniani hakuna bahati, ila kuna BARAKA NA FURSA. baraka hutoka kwa Mungu na ni matokeo ya kumcha Mungu na neema na rehema zake kwetu wanadamu. fursa hutokana na circumstances au mazingiza. ikishindwa kusoma mazingira yako na kuzibaini fursa zilizomo na kuzifanyia kazi, hutafanikiwa katika jambo lolote na ndio matokeo ya kujiita usiye na bahati na kumbe ulishindwa kuzibaini fursa na kuzitumia. hapa huwa tunaomba uzima tu, manake hata mtu asiye mcha Mungu akituma vizuri fursa zinazojitokeza hufanikiwa pengine hata kuzidi baadhi ya wacha Mungu!

kwa case yako, nakuona humchi Mungu sawasawa (rejea maelezo yako mwenyewe jinsi ulivyoelewa na jinsi unavyoyakabili majaribu kwenye ndoa yako). lakini hata kama humchi Mungu lakini unazo fursa amabazo ukiamua kuzitumia zinaweza kukusaidia. unasema huna uhuru, lakini umeweza kupata access ya internet na kusajili ID hapa, umeleta mada na unafuatilia mjadala na kujibu hoja! je hapo huoni fursa? je fursa hii ya kuwa connected umeitumiaje?

umeshauriwa na wengi kujitafutia cha kufanya, unasema mumeo hakuruhusu kutoka, hivi unajua wanawake wengine wanapambanaje na maisha? mbona akina mama wana mbinu nyingi sana, we unabadilishana nao mawazo juu ya nini ufanye, au we kwa kuwa umeolewa, basi unataka maisha yakuendee vyema kupitia mume? ukiona hayako unavyotarajia unasema huna bahati na kila ukipata fursa unaitumia kulalamikia tabia ya mwenzio? nyanyuka sasa (hata kama ni wakati akiwa kazini) jichanganye na akina mama wenzio walio karibu mshauriane kuhusu namna ya kukabiliana na maisha. usiwafuate wanaoendesha ma-VX, ma Rav-4 nk, bali wafuate wajane, aliotalikiwa na wengine wanaojua kukabili maisha katika hali kama hizo,hao ndio watakaokupa msaada kwa sasa. waulize taratibu, wao wanawezaje kushinda na kuishi kwa amani?

pia nakushauri, ufute kabisa mawazo ya kutoka nje ya ndoa au kugawana naye watoto kwa namna yoyote ile. usiogope kuhusu kuwa atawachukua, hayo mambo huamriwa na vyombo vya sheria na si mwanaume. uamini kuwa huyo ndiye mumeo wa kufa na kuzikana na usiache hata siku moja kuiombea familia yako na ujitahidi kuongea naye kwa hekima kubwa na upole hasa ukimwomba mjadili na kupanga maisha pamoja. hata kama ana dharau na mkali anakupiga mara kwa mara, hakikisha moyoni mwake unaweka chapa ya neno la hekima na upendo ili siku akirudiwa na fahamu zake, ajue ubaya wa hayo anayokutenda. usipoacha alama ya wema, hekima na subira moyoni mwake, hata kesho akirudi kwenye hali ya kukuheshimu, hataona alipokosea. hiii ndiyo maana Bwana wetu Yesu akatuambia TUUSHINDE UBAYA KWA WEMA!

mwisho nakupa pole kwa hayo unayopitia, fahamu kuwa Mungu anakupenda sana na mbele yako amekuwekea baraka na fursa, ukizitumia kwa hekima na shukrani, yeye ni mwaminifu hatakuacha katika majaribu yako.

tulihimidi jina la Bwana kila wakati
 
asanteni nimevunja ukimya na kila siku namwambia kuhusu hivi vitu mie mwenyewe sipendi ugomvi napenda niishi vyema nae milele lakini bwana mwenyewe anahangaika nje na kuhusu intanet niko kwenye simu natumia na mungu namuomba kila siku na huyu bwana hataki kuambiwa ukimwambia kosa lake unapata kipigo anasema mie mwanaume hata niwe na wanawake mia we haikuhusu we uko hapa unakula unalala na unavaa inakutosha usiningilie mie kama huwezi kuvumilia ondoka na anasema kwanza umenipa nini zaidi ya watoto,watoto hata nje naweza kupata,kwa kweli mie nimetoka nae mbali sana huyu bwana alikuwa hana chochote tumechuma wote pamoja nimehangaika nae kwenye kufanya kazi na hamna hata siku nichukue hata shs mia bila ruksa leo mungu kampa mie ananiona kama mavi anasema nyie wanawake wa tanzania malaya sana huyu bwana ni mtu wa nje but anaishi hapa mie mpole sana ndo mana leo naonewa dah
 
nampenda sana mume wangu hata mwanaume mwingine simwangalii nakuwa sina time nao hata mtu akinitongoza namwambia mume wangu niko honest but still ndo hivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…