Asec Mimosas imeomba mechi ya marudiano na Simba ifanyike kwa Mkapa

1) Asec bado hajafuzu ila ana mazingira mazuri ya kufuzu,
Endapo atafungwa mechi dhidi ya Simba na huku Wydad akishinda dhidi ya Galaxy basi msimamo utakuwa
Asec 10
Simba 8
Wydad 7

Mechi ya mwisho ni Wydad vs Asec kule Morocco na endapo Wydad watashinda goli 2 bila huku Simba naye akishinda dhidi ya Galaxy basi Asec ataaga mashindano kwasababu watalingana point na Wydad ila H2H itamtoa.

2) Asec wanatokea Ivory coast na ndio wanao host AFCON mwaka huu, hivyo swala la uwanja Ivory coast hakuna shaka, na swala la usalama pia hakuna shaka pia
3) Asec Mimosa ndio klabu kubwa Ivory coast hivyo swala la mashabiki kule wa kuujaza uwanja kwao hakuna shaka kabisa.

4) kitendo cha kukidhi vigezo hivyo vitatu juu, kama wataamua kuja kuchezea Tanzania mchezo wao, basi moja kwa moja watafikiriwa katika upangaji wa matokeo
 
HHahahahahaha.ina maana kuna mnao amini hii habari ?
 
Umemaliza kila kitu
 
Mkubwa kundi liko hivi
Asec point 10
Simba point 5
Galaxy point 4
Waydad point 3

Sasa hiyo ya waydad akishinda anakuwa na point 7 hiyo moja inatoka wapi??
Waydad akishinda mechi zake zote zilizobaki atakuwa na jumla ya point 9
Kwa maana hiyo mwenye uhakika wa kumzidi point asec ni simba tu tena na yeye ashinde mechi zake zote zilizosalia hivyo kumfanya amalize akiwa kiongozi wa kundi kwa alama 11.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…