Hapa Sokwe hujafikiria kama binaadamu....malalamiko yako hayana msingi wowote.
Na unaposema Asha alimsaidia mtu baki akamuacha ndugu yake...hiki ni kioja, huyo Mungu unayemshtakia kwake yeye hajui kama kuna ndugu baki na ndugu ndani...kwake ndugu ni ndugu, hebu ujifanyie tathmini kama kweli unamjua Mwenyezi Mungu.
Kesho Misanya Bingi mambo yake yasipoenda sawa utambwatukia Mzee Mengi kwa kuwa tu Misanya alifanya kazi IPP ? je ni Amigo peke yake ndiye aliyekwishafanya kazi kwa Asha ?....na wengine je hawana stahili hizo ? huyo Asha atayaweza wapi ? badala kuilaumu serikali yako kukosa hizo huduma bora unahamishia hasira kwa Asha.
Unavyosema Asha ni mbaya wewe tunakujua wapi tuone kuwa ni mwema unayepaswa kumuona Asha ni mwema ? nijuavyo mbaya pia humuona mwema mbaya kwa maslahi na tafsiri zake binafsi...kama wewe ni Singa singa na Asha ni Kafulila basi Asha atakuwa mbaya tu kwako, hatuna msaada kwa hilo ewe Sokwe.
Kama unasema Asha ni ndugu wa Marehemu ni dhahiri kuwa wewe usiye ndugu hujui Marehemu alikuwa anaugua nini, hujui daktari aliongea nini na ndugu wa marehemu kuhusu ugonjwa wa Marehemu...sasa hebu kafanye homework zako vizuri uje tena ueleweke unataka kusema nini.