Ashikiliwa na Jeshi la Polisi Morogoro kwa tuhuma za wizi wa misalaba 14

Ashikiliwa na Jeshi la Polisi Morogoro kwa tuhuma za wizi wa misalaba 14

mshale21

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2021
Posts
2,126
Reaction score
5,068
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola.

Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Morogoro ACP Alex Mkama amesema, jeshi hilo lilipokea malalamiko kuwepo kwa wizi wa misalaba ndipo walipofanya msako na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye ni fundi seremala ambaye anatumia misalaba hiyo kama vyuma chakavu.
 
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola...
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola.[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji2][emoji2] maisha magumu sana hali sio poa kbsa kitaa wahuni wamepinda mdog mdogo wataanza kufukua makaburi waibe majeneza

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Mara ya pili kukamatwa mtu kule kola , hata Kama vyuma, kazoea wizi, na kukosa hofu ya mungu.
 
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola...
Mwaka 2015 wezi/majambazi walilipua kwa mabomu kaburi lililojengwa kwa marumaru kule Afrika Kusini katika Jimbo la North-West ili kuiba Dhahabu aliyozikwa nayo marehemu.
 
Mwanaume mmoja Mkazi wa Kichangani Manispaa ya Morogoro Meshack Azikam (23) amekamatwa kwa tuhuma za wizi wa misalaba 14.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Alex Mkama amesema Mtuhumiwa huyo alikamatwa aking'oa msalaba katika makaburi ya Kola Manispaa ya Morogoro na baada ya kumfanyia upekuzi nyumbani kwake walikuta misalaba mingine 13 .

Ayo tv imeongea na Msimamizi wa makaburi hayo ya Kola, Abdalah Salum ambaye amesema changamoto hiyo imekuwa kubwa katika eneo hilo na mara nyingi wizi unafanyika majira ya alfajiri na jioni ambapo licha ya kuiba misalaba pia limeibuka wimbi wa wizi wa matofali na marumaru.

"Tumeshawakamata wezi mara nne kwa nyakati tofauti na wengine tumewapeleka Polisi wengine tumewafikisha Mahakamani na misalaba mingine ipo hapa tumekuta imeng'olewa na kutelekezwa katika makaburi hayo tunaomba Ndugu waje wachukue wakarudishie kwenye makaburi ya Ndugu zao"

Chanzo: Millard Ayo
 
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola...
CCM mpo? Mnakoipeleka nchi sipo! Mama kafanya hiki na kile, hakuna tija katika uchumi wa mtu mmoja mmoja!!
 
Makaburi tu ya kinondoni uwizi upo ila wanaiba mishumaa na maua
Ila siku hizi wafiwa wakipeleka maua
Huwa wanayanyofoanyofoa

Ova
 
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola.

Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Morogoro ACP Alex Mkama amesema, jeshi hilo lilipokea malalamiko kuwepo kwa wizi wa misalaba ndipo walipofanya msako na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye ni fundi seremala ambaye anatumia misalaba hiyo kama vyuma chakavu.
Mimi ndugu yangu kazikwa makaburi ya kola na waliiba msalaba na kung’oa kila kitu kilichowekwa ktk kaburi Yaani nilijua nimekwenda kaburi tofauti

Ova
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Mtu mmoja anaefahamika kwa jina la Meshack Azikam (23) mkazi wa mtaa Kichangani Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani humo kwa kosa la kuiba misalaba 14 katika makaburi ya Kola.[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
Miaka ya nyuma 90 kuna mjomba wangu alikuwaga baharia, alikufaga
Walimzika na cheni dhahabu,bracelet pia,si unajuwa mabaharia zamani tena kwa sifa,
Ilikuwa kwa kopa pale...
Ahh wahuni walimfukua aise walikomba kila kitu

Ova
 
Endapo akipatikana na hatia afungwe jela naye aliwe kiboga tumechoka kuona watu wangese wamejaa kwenye jamii zetu.
 
Makaburi tu ya kinondoni uwizi upo ila wanaiba mishumaa na maua
Ila siku hizi wafiwa wakipeleka maua
Huwa wanayanyofoanyofoa

Ova

Wanayaunguza kabisa na mishumaa, Yaani maua yanakuwa uchafu juu ya kaburi Kwa kuchomwa moto na yote hii kisa wasiibe, Yaani ni shida Tupu, pale kinondoni niliacha mishumaa ktk kaburi la Baba yangu Yaani ile mishumaa ya kuwaka Kwa siku Tatu Lakini baada ya mazishi siku inayofuatia nilikwenda pale na nilikuta mishumaa yote imepotea wameiba aisee

Ova and out
 
Wanayaunguza kabisa na mishumaa, Yaani maua yanakuwa uchafu juu ya kaburi Kwa kuchomwa moto na yote hii kisa wasiibe, Yaani ni shida Tupu, pale kinondoni niliacha mishumaa ktk kaburi la Baba yangu Yaani ile mishumaa ya kuwaka Kwa siku Tatu Lakini baada ya mazishi siku inayofuatia nilikwenda pale na nilikuta mishumaa yote imepotea wameiba aisee

Ova and out
Wabongo nuksi sana

Mara nyingi wezi huwa mateja

Ova
 
Back
Top Bottom