Asikilizwe Huyu Mzee tunaposema uchaguzi wa mwaka 2020 haukuwa uchaguzi bali ni uhuni muwe mnatuelewa!!

Konny Joseph

Senior Member
Joined
Aug 28, 2016
Posts
118
Reaction score
199
Your browser is not able to display this video.


Tumekuwa tunatumia nguvu nyingi kusifu na kuficha madhaifu ya Magufuli, ila Mungu kwa rehema zake amekuwa anayafichua kwa namna anayoitaka yeye.

Wazee hawa wanadhihirisha dhulma kubwa iliyofanywa na Magufuli katika uchaguzi wa mwaka 2020, ambao wahafidhina wa chama tawala wanalazimisha kuficha ukweli huo.

Natumai kadiri siku zinavyokwenda mbele yataibuka maovu mengi yaliyofanywa na mwanakwenda zake ili wale wanaotetea wafedheheke!!
 
Uchaguzi huru, wa wazi na wa haki, utafanyika humu nchini kwa mujibu wa katiba, sheria, kanuni na taratibu za nchi. Na sio kulingana na maoni, mtazamo, matakwa, malalamiko au maelekezo ya mtu fulani mahala fulani. No, haipo hivyo 🐒

Mtazamo na maoni ya mtu, yasikilizwe na kuheshimiwa, kuongeza ufahamu, tahadhari, maboresho baadae, na uelewa wa masula ya uchaguzi na si vinginevyo🐒

Ni vuzuri zaidi, kujiandaa na kujipanga vizur kushiriki chaguzi zijazo kikamilifu, kwa hiari bila shuruti au mihemko, ili utulivu na Amani ya Mama Tanzania iendelee kutamalaki bila hamaki kwa waTanzania wote 🐒
 
NJia waloitumia kwenda mtoni kuchota maji ndio hiyo hiyo watakayoirudia wakitoka mtoni.

Mbao za mti pori na mti shamba zote ni mbao.
 
Hao wazee wanaudumavi tu wa akili, yaani wanamuona huyo mbunge kama kama ndiyo mwokozi wao wakati ukweli anawasilikiza tu kuwapiga siasa.
 
Mwendazake!
 
Nyie ngojeni muone mtakavyopigwa tena 2025. Wenzenu washaanza kupita kwa wananchi mapema. Ile kazi alopiga JPM si ya kitoto, hakutegemea tena pesa ya matajiri kupiga kampeni, wananchi waliona na wakajibu kwenye sanduku!! Kama mliibiwa basi fursa ilikuwepo kwenda mahakamani, vyombo hivi hivi mlikuwa mkienda na mlikuwa mnashinda kesi, utasikia "Kibatala aibwaga Serikali mahakamani, uchaguzi kurudiwa" hamjiulizi, mliibiwa nchi nzima? Mlikuwa mmesinzia?
Tatizo nyinyi hampo mashinani, vyama vipo makao makuu tu na kupiga blah blah na kupiga pesa za ruzuku na misaada. Wananchi hawana cha kukupimeni.
Pesa haiendi chini kujenga vyama vyenu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…