Jee ni kweli Mohamed Iqbal Dar, mwenye asili ya kihindi, aliyekuwa akiishi Tanga, mnamo mwaka 1964 ndiye aliipa nchi yetu jina zuri la "Tanzania".
Kama ni kweli huyu mtu yuko wapi kwa sasa?
Na serikali yetu inaweka kumbu-kumbu gani za kihistoria kwa huyu mtu kwa vizazi vijavyo? ili vipate kujuwa nani aliipa nchi hii jina lake.
Au mchango wake hauna maana yeyote, ni jina tuu, kwa hiyo potelea mbali?
Nadhani hata vizazi vya sasa, ambavyo havipo mbali 1964 hatuna uhakika na ndio maana tunauliza.
Naomba anaejuwa kuhusu hilo atuelimishe.
================
UPDATE:
October 22, 2012