Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
Historia ya dunia inasema kuwa binadamu wa kwanza aliishi barani Afrika na mifupa yake iligundulika Afrika tena katika nchi ya TANZANIA
.Na dunia nzima inajua kuwa mtu wa kwanza aliishi hapa Tanzania.wakati huo huo historia inadai kuwa sehemu ya kwanza kwa binadamu kustaharabika na kuendelea kisayansi ulianzia hapa hapa Afrika tena huko Afrika kaskazini katika nchi ya Misri.
Hivyo basi mwisho wa siku utakuja kugundua kuwa bara la Afrika lina historia ndefu sana. Lakini wewe kama mwafrika unapaswa ujue kuwa, Kuna tofauti kubwa kati ya maneno haya, Mwafrika, Uafrika na bara la Afrika. Wakati tukifikiria tofauti ya maneno haya, hebu tuone asili ya neno Afrika. Lakini kabla ya kuapata historia ya neno Afrika, kuna mambo machache ya kufahamu.
Twende kazi sasa
Kwanza Afrika ni bara la pili kwa ukubwa wa kilomita za mraba 30,221,532, lenye idadi ya watu zaidi ya 3.1 bilioni. kwa sasa bara hili lina nchi zisizopungua 56.
Kijiografia bara hili limezungukwa na bahari kubwa, kwa mfano bahari ya Hindi na Atlantiki. Na bara hili linagawika ktika sehemu kuu nne yaani Afrika kaskazini, Afrika mashariki, Afrika kusini na Afrika magharibi.
Historia ya neno Afrika inaongozwa na nadharia mbalimbali moja wapo ni nadharia ya Kabila la Waafr(Afri tribe). WaAfri ni kabila ambalo lilikuwepo kwa miaka mingi huko Afrika kaskazini. Na historia inasema kuwa waafrika hao walikuwa na vita na watu wa ulaya muda mrefu sana kuanzia miaka ya 400-100KK au KM. Na moja ya kubwa ilikuwa vita vya Punic(260-140)KK au KM ambavyo vilihusisha mapigano kati ya wacarthege(watunisia kwa sasa) na waroma.Waroma walipofika katika mji wa carthage walikuta watu( kabila la Waafri ambao kwa wakatii huo hawakujulikana waliitwaje kwa sababu za kukosekana kwa maandishi). inasemekana kuwa sababu za Waroma kuwaita Waafri ni namna ya Uongeaji wao na muonekano wao hasa hasa rangi.
Historia inaeleza zaidi kuwa, waroma kwa Lugha yao walitamka AFRICUS, wakimaanisha (the land of afri) yaani Ardhi ya waafri. na kwa kuwa hiyo ndiyo sehemu yao ya kwanza kufika, na ndio sehemu za mwanzo miji kuendelea. wakaandika habari zote juu ya Waafri na ardhi yao(yaani bara la Afrika). Kuanzia hapo maeneo hayo yalifaamika kama Africus. Na kutokana na miingiliano ya watu mbalimbali , watu wengi (hasa hasa Waarabu) walishindwa kutamka Africus na kujikuta wakitamka Afrika. Na hapo ndipo asili la neno Afrika lilitokea. jambo la kusisitiza ni kwamba, hii ni nadharia tu ambayo ilianzishwa kwa lengo la kutoa ufafanuzi. na kuna nadharia zingine pia. na zaidi waafrika tunapaswa kufahamu kuwa, asili ya mambo mengi duniani imetokana aidha mitazamo ya wageni kwa utani au mambo yao au mitazamo ya wenyeji na mtindo wao wa maisha.
Ni mimi MJUKUU WA CHIFU a.k.a kiboko ya The bold
.Na dunia nzima inajua kuwa mtu wa kwanza aliishi hapa Tanzania.wakati huo huo historia inadai kuwa sehemu ya kwanza kwa binadamu kustaharabika na kuendelea kisayansi ulianzia hapa hapa Afrika tena huko Afrika kaskazini katika nchi ya Misri.
Hivyo basi mwisho wa siku utakuja kugundua kuwa bara la Afrika lina historia ndefu sana. Lakini wewe kama mwafrika unapaswa ujue kuwa, Kuna tofauti kubwa kati ya maneno haya, Mwafrika, Uafrika na bara la Afrika. Wakati tukifikiria tofauti ya maneno haya, hebu tuone asili ya neno Afrika. Lakini kabla ya kuapata historia ya neno Afrika, kuna mambo machache ya kufahamu.
Twende kazi sasa
Kwanza Afrika ni bara la pili kwa ukubwa wa kilomita za mraba 30,221,532, lenye idadi ya watu zaidi ya 3.1 bilioni. kwa sasa bara hili lina nchi zisizopungua 56.
Kijiografia bara hili limezungukwa na bahari kubwa, kwa mfano bahari ya Hindi na Atlantiki. Na bara hili linagawika ktika sehemu kuu nne yaani Afrika kaskazini, Afrika mashariki, Afrika kusini na Afrika magharibi.
Historia ya neno Afrika inaongozwa na nadharia mbalimbali moja wapo ni nadharia ya Kabila la Waafr(Afri tribe). WaAfri ni kabila ambalo lilikuwepo kwa miaka mingi huko Afrika kaskazini. Na historia inasema kuwa waafrika hao walikuwa na vita na watu wa ulaya muda mrefu sana kuanzia miaka ya 400-100KK au KM. Na moja ya kubwa ilikuwa vita vya Punic(260-140)KK au KM ambavyo vilihusisha mapigano kati ya wacarthege(watunisia kwa sasa) na waroma.Waroma walipofika katika mji wa carthage walikuta watu( kabila la Waafri ambao kwa wakatii huo hawakujulikana waliitwaje kwa sababu za kukosekana kwa maandishi). inasemekana kuwa sababu za Waroma kuwaita Waafri ni namna ya Uongeaji wao na muonekano wao hasa hasa rangi.
Historia inaeleza zaidi kuwa, waroma kwa Lugha yao walitamka AFRICUS, wakimaanisha (the land of afri) yaani Ardhi ya waafri. na kwa kuwa hiyo ndiyo sehemu yao ya kwanza kufika, na ndio sehemu za mwanzo miji kuendelea. wakaandika habari zote juu ya Waafri na ardhi yao(yaani bara la Afrika). Kuanzia hapo maeneo hayo yalifaamika kama Africus. Na kutokana na miingiliano ya watu mbalimbali , watu wengi (hasa hasa Waarabu) walishindwa kutamka Africus na kujikuta wakitamka Afrika. Na hapo ndipo asili la neno Afrika lilitokea. jambo la kusisitiza ni kwamba, hii ni nadharia tu ambayo ilianzishwa kwa lengo la kutoa ufafanuzi. na kuna nadharia zingine pia. na zaidi waafrika tunapaswa kufahamu kuwa, asili ya mambo mengi duniani imetokana aidha mitazamo ya wageni kwa utani au mambo yao au mitazamo ya wenyeji na mtindo wao wa maisha.
Ni mimi MJUKUU WA CHIFU a.k.a kiboko ya The bold