Asilimia 88 ya vijana (umri 30 - 35) hutegemea wazazi na mashemeji

M24 Headquarters-Kigali

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2012
Posts
8,199
Reaction score
8,186
Katika kutathimini namna ambavyo kama taifa linapaswa kuwekeza kwenye elimu ya biashara (ujasiriamali) na ubunifu badala ya vijana kutegemea ajira za serikali, uchunguzi uliofanywa katika miji ya Dar es Salaam, Morogoro, Tanga, Mwanza & Kagera umegundua 88% ya vijana kati ya umri wa miaka 30 na 35 bado hutegemea kwa matumizi yao yote toka kwa wazazi ama Mashemeji zao.

Hii si dalili nzuri tunapoelekea kwenye nchi ya viwanda na kutimiza dira ya Taifa ya maendeleo ya 2025 (Tanzania Vision 2025). Vijana amkeni fanyeni kazi, biashara, kilimo, acheni kubweteka na ku-bet kutwa nzima, kushangilia mipira ya ulaya na siasa za Marekani huku hamna namna ya kuingiza kipato binafsi zaid ya kutegemea mashemeji na wazazi kuwapa pesa ya matumizi.
====
*vijana acheni uvivuuuu
 

Attachments

  • f0d73c2d05a24b6d844ca6fba86bd3b6.jpg
    70.3 KB · Views: 2
Kweli kabisa... tena vijana wengi wa namna hii ni mashabiki wa Yanga. Kazi kushangilia Simba ikifungwa.

Fanyeni kazi vijana!!
 
mimi nimeamua kumfanya shemeji (kwa siri) NYUMBA NDOGO. Yaani kuliko nikatafute kicheche mtaani bora nile humo humo ndani kwa gharama nafuu na pia katika kutimiza ile dhana ya EMPOWERMENT.
** nahusudu utaratibu wa dini fulani (jina kapuni) wa kuruhusu kuoa zaid ya mke mmoja hata kama ni ndugu.
 
Msalimie shemeji yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…