Askari 8 wanashikiliwa Morogoro kwa tuhuma za Mauaji ya Ally Zona

Askari 8 wanashikiliwa Morogoro kwa tuhuma za Mauaji ya Ally Zona

Mlyafinono

Senior Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
177
Reaction score
47
-Habari zilizotufikia punde ni kwamba askari wanane (8) wamekamatwa mkoani Morogoro kwa tuhuma za mauaji ya Muuza magazeti Ali Zona wakati wa maandamano ya Chadema yaliyofanyika mwezi uliopita mjini humo.

-Mjini Iringa mtuhumiwa wa mauaji ya Daudi Mwangosi hakuweza kufikishwa mahakamani leo kama ilivyokuwa imepangwa.

-IGP Mwema bado yupo Iringa anahaha kuzungumza na viongozi wa dini kusaidiwa kupoza mambo katika jamii kuhusu tukio la kuuawa kwa mwandishi wa habari Daudi Mwangosi, tukio ambalo limeonekana kugusa hisia kali miongoni mwa wanajamii mkoani humo.
 
Hivi kwani wauaji si wanaonekana katika picha zote za still na video. Sasa inakuwaje bado hawajapanda kizimbani? Mbona ya Kanumba Lulu alipanda mahakamani immediately wakati hata haijulikana alisukuma mtu au vipi? sasa this glaring action and event sasa mnasema nini polissmmmmmm nyie?
 
Kwanini wanawakamata hao kabla ya TUME huru kuundwa, wakati Nape alisema Tundu Lisu ni muongo amedanganya umma kuwa POLISICCM ndiyo waliofanya mauaji. Wanatafuta mbinu ya kuwavisha watu makosa, wakati kama kungekuwa na TUME huru tungejua kwa undani kwamba hawa askari walipewa maagizo gani, na nani, na kwaajili ya nini?
 
Enyi Makamanda wenzetu CHADEMA,

kama mlikua hamna taarifa ya yale yanayoendelea nyuma ya pazi hadi hivi sasa ukweli wa mambo ni kwamba SERIKALI YA RAIS KIKWETE hadi hivi sasa
imebanwa to the maximum (unaweza ukarudia hilo fungu la maneno mara 10 ukipenda) kufuatia huu mlolongo mrefu wa UKATILI WA JESHI LA POLISI DHIDI YA RAIA NA CHADEMA ...

... hot hot zaidi ziko njiani huku baadhi ya vingunge wana-CCM wakitupiana mpira kushoto kulia. Kaeni mkao wa kula juu ya haya.

Hilo ndilo neno la leo huku tukimwambia Mze Wasira, Nchimbi pamoja na Mwema kwamba mbele ya kitu 'HAKI YETU' katu haturudi nyuma hatubanduki hata kwa mizinga!

Mabadiliko ya kweli yaja tena hayazuiliki hata kwa dawa!!
 



Asanteni Kamati Kuu CHADEMA walau kwa kuitikia sauti ya na majonzi ya umma wa Tanzania na kutoa dira kwa Taifa, kukemea na kuainisha mambo gani yafanyike ili kutokomesha UKATILI WA JESHI LA POLISI dhidi ya raia na mauaji yasiokwisha kila kona ya nchi.

Hakika bado tunaomba sana mambo yasiishie tu hapo kwenye ma-tamko bali zaidi wananchi tunaasubiri kuona CHADEMA kinavyofwatilia utekelezaji wa kila agizo la Kamati Kuu taifa kwa faida yetu sisi walalahoi huku vijijini.

Elimu ya uraia kwa umma wa Tanzania sasa ndio iongezewe kasi maraduru ili kila kijiji kiweze kufikiwa ki-undani zaidi na zaidi.

KOVU LA UKATILI WA JESHI LA POLISI DHIDI YA RAIA NCHINI:
WATANZANIA TUNAJIBU GANI KWA 'MACHOZI YA LAANA NA KILIO CHA HAKI YA MWANAMAMA WINFRIDA JOHN' WA KIJIJI CHA NYOLOLO MKOANI IRINGA ???


Kamanda Winfrida John, kada wa CHADEMA kijiji cha Nyololo, bila shaka wewe ni mwana mama mtu mdogo tu hapo kijijini Nyololo ambaye pengine hata mbunge wa eneo hilo huenda asikufahamu kitu achilia mbali wakuu wa wilaya na mkoa huko Mufindi na Iringa kwa mpangilio huo, ila kwa wachache sana tena wenye jicho la mwewe angani huenda lako hili la kipekee mno likawa limewagusa nao pia.

Naam, kabla sijaandika mengi juu yako na kile kilichonigusa mno kwako kwanza niombe kwamba tafadhali Mama Winfrida futa machozi yako, yale ya akinamama wengine wengi zaidi hapo Nyololo na kwamba katu usiendelee kutuhuzunisha zaidi sisi WaTanzania wenzako kwa uchungu wote huo; machozi yako hadharani ya KULILIA HAKI na kutuhoji sote kama taifa tukupe jibu UHURU WAKO WA MAONI, NA KUJUMUIKA ulikopotelea;

Ni kweli kwamba siku hiyo 'SIMBA MLA WANYONGE WANAAOLILIA HAAKI' alipomnyakua makuchani Mtanzania wa 22 (Daudi Mwangosi) afiaye mikononi mwa dola kwa visingizio mbalimbali za kisiasa tangu mwaka huu, bila shaka watu wengi tu hapo Nyololo, Itete na hata vijiji vingine vya mbali sana nao walilia ila wewe hapo chozi laako linageuka kuwa chozi la dhahabu si kwa kuwa tu ulikua kwenye eneo la tukio baali zaidi ni kwamba ni mmoja kati ya wenyeji waliotembelewa naa CHAADEMA kwa shughuli ya ufunguzi wa ofisi mahali haapo.

Hakika ni kutokana na udhahabu huo wa chozi lako tena ukiwaa ni mwanamama tu mnaohitajika kuimarishwa zaidi kushiriki katika siasa na uongozi wa taifa, inanifanya nisiamini tu kwamba hivi karibuni huenda ukawa ni mtu wa kutafutwa sana japo sauti na vyombo vingi vya nyumbani hapa na vile vya kimataifa kama vile BBC, VoA, Deuche Welle ...

... bali zaidi najikutaa pia nikiwa sina wasi wasi kwamba Mama Hellen Kijo Bisimba naye amekusikia popote alipo, naamini kwamba msururu wako wa maswali ya msingi sana uliyoyauliza siku hii hata Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani umemuacha hana amani moyoni;

Ndio, kwa mtaji w kilio chako kikiwakilicha KILIO CHA HAKI kwetu sisi WaTanzania kwa ujumla wetu bila shaka ni wazi kwamba tayari umetuma ujumbe mzito kiasi cha kuwalazimisha hata magwiji wa habari nchiki akina Mzee Jenerali Ulimwengu, Fred Masako, Mzee Mwanakijiji, pamoja na Pasco wa JF.

Nasema kwa kilio cha mwanamama 'kiumbe dhaifu' katika jamii yetu hii inayoendekeza ufalme wa akina-baba tu kwamba vile vile utakua umewakuna akina Mama Nkya, Ayub Ryoba, Muhingo Rweyemamu pamoja na wengine kibao, waondoke kwenye viyoyozi maofisini na kuanza kupiga kiguu na njia wao wenyewe bila kumuagiza mwandishi yeyote wa chini, kwenda kukutafutia majibu sahihi na murua zaidi kiasi cha kuweza kukufuta machozi wewe na vizazi vijavyo;

Mama Winifrida, kwa kilio hiki hapo kijijini Nyololo ni wazi kwamba tayari umewakilisha sauti dhaifu za akina mama wote na watoto Tanzania ambao kweli
siku Daudi Mwangosi alipogeuka RUNDO LA NYAMA hapo kijijini kwenu(kwa hisani ya maagizo ya serikali ya CCM) - wenzetu mmeonekana kuteseka mno kukimbia ovyo na vichanga kuokoa maisha huku mkidhalilishwa na mgeni wenu CHADEMA ambaye ndiye kwanza mlikua mnamkaribisha rasmi hapo kijijini kwenu kwa kumpa eneo akafungulie ofisi yake (kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi) lakini ukarimu wenu wote ukahitimishwa na kilio cha historia yote Nyololo kugeuka ghafla kuwa uwanja wa mauji kama Syria.

Naam, nielewavyo mimi ni kwamba mama yetu Winfrida, hadi hapo ni kwamba tayari umewaamrisha wanaharakati kama Kijana mwenzetu Kibodya, Tundu Lissu, Deus Mallya, Prof Shivji, John Tendwa, pamoja na Mhe Augustino Mrema.

Wengine zaidi ambao wapende wasipende machozi yako ya haki bila shaka yako mabegani mwao ni pamoja na Prof Palamagamba Kabudi, Madam Spika wa Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, Mama Makinda, Prof Safari, Prof Maina, Prof Baregu, Dr Kitila Mkumbo, Dr Azaveli.

Ndio, nasema hawa waheshimiwa wote wanao wajibu kwako usiokwepeka kutoa jawabu kamili tena lisilocha maswali, kila mmoja kwa wakati wake, wakwambie kwamba kwenye katiba mpya wao wanategemea kuona Jeshi la Polisi la aina gani ili Winfrida John wa miaka hiyo ijayo wao wasije wakajikuta wakilia kilio kile kile kilichokumuaga machozi hapo Nyololo.

WaTanznia wote bila kujali itikadi za kidini na kisiasa, je tunalo jibu gani kwa mama huyu Winfrida John wa kijiji cha Nyololo ikiwa ni kielelezo cha kilio cha akina mama wengine wengi zaidi wasiokua na majina katika jamii yetu hii wangali nao wanao wachozi yasiokauka kulilia haki kama vile kule Igunga, Arumeru Mashariki, mauji ya Pemba, Arusha, Tarime, Mbeya ...?


 
Last edited by a moderator:
-Habari zilizotufikia punde ni kwamba askari wanane (8) wamekamatwa mkoani Morogoro kwa tuhuma za mauaji ya Muuza magazeti Ali Zona wakati wa maandamano ya Chadema yaliyofanyika mwezi uliopita mjini humo.

-Mjini Iringa mtuhumiwa wa mauaji ya Daudi Mwangosi hakuweza kufikishwa mahakamani leo kama ilivyokuwa imepangwa.

-IGP Mwema bado yupo Iringa anahaha kuzungumza na viongozi wa dini kusaidiwa kupoza mambo katika jamii kuhusu tukio la kuuawa kwa mwandishi wa habari Daudi Mwangosi, tukio ambalo limeonekana kugusa hisia kali miongoni mwa wanajamii mkoani humo.

Mbona jana hujatuambia nini kimezunguzwa katika kikao cha wauaji wa watanzania wanaotumia unifomu za polisi? Hivi huyo Shemeji wa Vasco ndio mtuhumiwa nambari wani
 
Kumbe ile ishu ya UNDEFINE FLYING OBJECT (UFO) ilitokea kwa polisi. Ile Ilikua ni mbinu dhaifu.
 
Jamani yule Senso wa Polisi makao makuu yu wapi na majibu yake ya kufikirika kwenye njozi??tunamtaka atupe tena majibu ya kilichoomuua Mwangosi!!
 
kama kweli tunashukuru kwamba hatua zimeanza chukuliwa, lakini tatizo ni ajira zisizo fuata uweledi, watoto watukutu ndio wanao ajiriwa polisi
 
Wakuu hivi huyo muzungu kwenye picha ni nani? Kweli hili chama ni balaa limedhihirisha ni la wote hakuna ubaguzi wa aina yoyote iwe dini, rangi, jinsia, wala nini. Viva Chadema.
 



Asanteni Kamati Kuu CHADEMA walau kwa kuitikia sauti ya na majonzi ya umma wa Tanzania na kutoa dira kwa Taifa, kukemea na kuainisha mambo gani yafanyike ili kutokomesha UKATILI WA JESHI LA POLISI dhidi ya raia na mauaji yasiokwisha kila kona ya nchi.

Hakika bado tunaomba sana mambo yasiishie tu hapo kwenye ma-tamko bali zaidi wananchi tunaasubiri kuona CHADEMA kinavyofwatilia utekelezaji wa kila agizo la Kamati Kuu taifa kwa faida yetu sisi walalahoi huku vijijini.

Elimu ya uraia kwa umma wa Tanzania sasa ndio iongezewe kasi maraduru ili kila kijiji kiweze kufikiwa ki-undani zaidi na zaidi.

Mkuu, nimetamani sana kujua yaliyomkuta dada yetu huyo. Bahati mbaya natumia simu. Please help!
 
Hilo ni igizo lingine. Hakuna la maana. Cha kujiuliza hapa ni kwamba iweje washtakiwe wakati tume haijamaliza kazi! Ikija na majibu tofauti? Its another silly season! Au series kama Isidingo.
 
Enyi Makamanda wenzetu CHADEMA,

kama mlikua hamna taarifa ya yale yanayoendelea nyuma ya pazi hadi hivi sasa ukweli wa mambo ni kwamba SERIKALI YA RAIS KIKWETE hadi hivi sasa
imebanwa to the maximum (unaweza ukarudia hilo fungu la maneno mara 10 ukipenda) kufuatia huu mlolongo mrefu wa UKATILI WA JESHI LA POLISI DHIDI YA RAIA NA CHADEMA ...

... hot hot zaidi ziko njiani huku baadhi ya vingunge wana-CCM wakitupiana mpira kushoto kulia. Kaeni mkao wa kula juu ya haya.

Hilo ndilo neno la leo huku tukimwambia Mze Wasira, Nchimbi pamoja na Mwema kwamba mbele ya kitu 'HAKI YETU' katu haturudi nyuma hatubanduki hata kwa mizinga!

Mabadiliko ya kweli yaja tena hayazuiliki hata kwa dawa!!
Hakuna kurudi nyuma,JUSTICE MUST PREVAIL!Na huu ndo uwe mwisho wa udhalimu.Kama kwenye process hiyo ukombozi utapatikana,basi na iwe hivyo.
 
Hapana,askari wanaonewa,wao hutekeleza maagizo tu na ndicho walichoapa.Wauaji ni wale wanaotoa maagizo haya.Hawa ndio wanaostahili kukamatwa na kukatwa shingo zao.Inauma sana machozi yanitoka
 
Mbona jana hujatuambia nini kimezunguzwa katika kikao cha wauaji wa watanzania wanaotumia unifomu za polisi? Hivi huyo Shemeji wa Vasco ndio mtuhumiwa nambari wani

Kweli somo la historia ni adimu tena kwa watu wengi tz. I wish'you'could hv little of knowledge of what is so called wind of change; its sweeping tz now and its accelarated by people like you who do not turns blind'eye'from reality. chadema wameua wapi for heaven sake point out. Shame on you!
 
Mbona wanawaacha wahusika halisi Mwema na Nchimbi na kuwaonea hawa wanaopokea amri zao tu na hawatakiwi kuzipinga!
 
Back
Top Bottom