Askari Mstaafu: Sijalipwa stahiki zangu, Polisi wamenipa Siku 7 nikabidhi nyumba la sivyo vitu vyangu vitatolewa nje

Askari Mstaafu: Sijalipwa stahiki zangu, Polisi wamenipa Siku 7 nikabidhi nyumba la sivyo vitu vyangu vitatolewa nje

Kwanini hajaiomba CCM imsaidie kama alivyokuwa anaisaidia kupitisha masanduku ya kura feki ndio watumie mbinu hizo hizo kumnusuru.
 
Aibu hii jmn hizo pesa watu walishakula kuzitoa sasa ni mtihani shame on you!Aibu sana hii hamjali haki za wastaafu bila kusahau nyinyi wenyewe mtastaafu!
 
Ubaya ubwela! Ndivyo unavyoweza kusema. Ukiwatendea watu ubaya kwa kudhulumu haki zao za msingi au kuwaumiza kifizikia (physically) ipo siku nawe utapata msukomsuko kama huo hapa duniani hadi akili zitakukaa sawa. Kanuni ya tatu ya mwendo ya Newton inafanya kazi hapa duniani kila siku. "For every action, there is equal and opposite reaction". Baada ya huu ufunguzi, naomba sasa nijielekeze kwenye hoja.

Nafikiri nyote mnawakumbuka polisi hawa hapa waliohusika kuwapiga wafuasi wa CUF waliokuwa wakiandamana kihalali na kwa mujibu wa sheria. Tazama jinsi wanavyowapiga raia kwa virungu na kiuonevu kisa tu wanamiliki silaha na nguvu walizopewa na serikali ya CCM.


Kwa kudhihirisha kuwa malipo ya ubaya ni hapahapa duniani, polisi huyu anayelia hapa chini alikuwa ni miongoni mwa polisi waliohusika kuwapiga hao raia. Lakini leo hii baada ya kustaafu utumishi wa polisi na kunyimwa pesa za nauli na serikali hiyohiyo ya CCM aliyokuwa akiisaidia kuwapiga raia virungu, leo hii anakuja hapa kulialia akitaka aonewe huruma na raia aliokuwa akiwavunja miguu kwa virungu wakati akiwa ndani ya utawala wa polisi. Ubaya ubwela! Aliyokuwa akiwatendea raia wenzake leo hii yanamgeukia. Na haohao raia aliokuwa akiwavunja miguu na migongo, ndio anataka wamuonee huruma. Thubutu!


MAONI YANGU
Upolisi ni kazi ya laana. Usithubutu kuingia kwenye upolisi. Ni afadhali ukose kazi upige debe kwenye daladala wakuite teja au uokote makopo wakuite chizi kuliko kuajiriwa kuwa polisi. Nakuombea kwa Mungu akuwezeshe upate kazi kwenye kada nyingine mbali na upolisi au ukikosa kazi, ufanye kazi ya binafsi yenye staha na kipato kikubwa kuliko kazi ya polisi. Amina.
 
Hela ya mzigo na hela ya safari haizidi 5M,

Anakusubiria hizo ndo zimsaidie ila hela ya kustaaafu more than 30M hazikumsaidia.

Kukaa kambini ni ujinga, kunalemaza watu, wanasahau kujitafutia makazi yao ya kudumu.
 
Mzee John Samwel Swai(61) mstaafu wa Jeshi la Polisi amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumsaidia asiondolewe katika kambi anayoishi kwani bado hajalipwa fedha za mizigo pamoja na fedha za likizo ambazo anapaswa kulipwa.

.Mzee huyo alistaafu mwaka 2020 baada ya kutumikia jeshi la polisi kuanzia mwaka 1983 amedai kupewa barua na Mkuu wa Kambi za Polisi inayomtaka kuhama ndani ya siku saba kuanzia Februari 04 mpaka leo Februari 10 na endapo asipohama vitu vyake vitatolewa nje.

Kupitia barua aliyopewa tarehe nne mwezi huu imesema “Umeariwa kukabidhi nyumba tajwa hapo juu, kwani umeshastaafu kazi toka 2020.

Oc Barracks amekuamuru kukabidhi nyumba tajwa hapo juu kwa kuwa umestaafu kazi. Umepewa siku 07 kuanzia leo tarehe 04/02/2025 hadi 10/02/2025 uwe tayari umekabidhi nyumba hiyo, Kushindwa kutekeleza amri hii, vitu vyako vitatolewa nje, hivyo unaamriwa kuviondoa mwenyewe kabla ya kutolewa”

Mzee Swai amewaomba wasaidizi wa Rais ambao Jeshi la Polisi lipo chini yao akiwemo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini(IGP), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kumsaidia wakati huo serikali ikiendelea kushuhulikia malipo yao.

Jambo TV imefanya jitihda za kumtafuta Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini DCP David Misime kwa njia ya simu lakini jitihada hazikuzaa matunda.
Mbaya zaidi huenda walimtendesha dhambi hata ya kuua au kujeruhi kwa bunduki zao.
 
Hakuna uhusiano na laana ya mtu na kazi yke
Mbona wapo police wengi tu wapo fresh baada ya kustaafu
 
Kazi ambayo siwezi fanya bora nife njaa ni ugambo jiji kazi ya uporaji vitu vya watu wenye marejesho ya kausha damu
 
Ngoja anyooke maana wakiwa bado kazini huwa wanaona dunia yote ni ya kwao,sina huruma na hao watu kabisa hata kama nikakuta wamepata ajali bado wanapumua namaliza kazi
 
Hili ni funzo kwetu ambao umri wa kustaaf haujagota
 
Nyumba aipate wapi wakati amestaafu akiwa koplo na amepata kiinua mgongo milioni 20 zinatosha kujenga nyumba mkuu?

1983-2020=37 unawezaje kukosa kujenga Nyumba ya kujisitiri?
 
Back
Top Bottom