Askari wa barabarani wamuige askari wa Morocco kuongoza magari

Askari wa barabarani wamuige askari wa Morocco kuongoza magari

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Asubuhi na jioni ni muda ambao magari huwa mengi na askari wa usalama barabarani(Traffic) hujitahidi kupunguza adha hii kwa kuzipa kipaumbele barabara ambazo zina msongamano mkubwa zaidi wa magari.

Kinachotokea, mathalan upo kwenye barabara yenye magari pungufu, askari huyo ukakuzuia na ukawa mbele karibu na taa unaweza kulazimika kusubiri dakika 20 Traffic awajaze kwanza foleni ndio awaruhusu kwa pamoja, ratio yake ya kuruhusu ikawa dakika 20 kwenye msongamano kwa dakika 5 kusipo na msongamano(20:5), ukiwa kwenye msongamano unaweza kupita haraka zaidi na barabara iliyo nyeupe ukalaani traffic mpaka laana zikaisha.

Askari huyu wa Morocco pia anatoa muda mwingi zaidi kwa barabara yenye msongamano(Mwenge-Mjini) lakini anavunja kwenye makundi zile dakika nyingi kutowaweka watu, mfano badala ya kuwa 20:5 inakuwa 5:1. Kila baada ya dakika 5, anaziondoa gari chache zilizo kwenye barabara isiyo na kipaumbele, trafffic wengine unaombea uwe kwenye barabara yenye msongamano ili upite haraka kuliko kugandishwa kwenye barabara zisizo na magari mengi, yani anaweza kuita magari ambayo hayaonekani kutoka barabara kubwa.
 
Kabisa yupo yule mfupi mweusi hivi ana kakitambi ka kiaina, huwa ana wafikiria sana hata barabara nyingine mfano hii ya kutoka msasani kwenda Kinondoni, na kutoka kino kuja msasani japokuwa huwa hazina magari mengi sana ni mfano wa kuigwa kwa kweli.
 
Sijui umeandika nini!

Kazi ya traffic siyo kupunga mkono kuongoza magari!

Hii ishu ni dharula lakini huku kwetu eti ni ratiba kabisa trafiki offocer kupunga mikono magari!
Hii huonesha uprimitive tulionao!

Dunia iko kwenye automation lakini sisi kutwa tuko analog.

Ni matumizi mabaya ya askari ambao taifa limewekeza pesa na nguvu kusomesha! Halafu wanakuja kuota vibarango kwa kupigwa na jua wakati tungeweza set automation
 
kuna hawa wa mataa ya chang'ombe,sijui hata huwa wana shida gani by saa moja jion.

mnaotoka karume mnaweza subiri mpaka mkasahau.
 
Kabisa yupo yule mfupi mweusi hivi ana kakitambi ka kiaina, huwa ana wafikiria sana hata barabara nyingine mfano hii ya kutoka msasani kwenda Kinondoni, na kutoka kino kuja msasani japokuwa huwa hazina magari mengi sana ni mfano wa kuigwa kwa kweli.
Kuna siku aliruhusu magari na nilikuwa mbele kabisa, ghafla bodaboda akachomoka kutokea upande wa kinondoni, almanusura! ingekuwa ajali mbaya sana asubuhi asubuhi, akaniambia kwa sauti "Ungemgonga afe tu mbwa huyo"
 
Sijui umeandika nini!

Kazi ya traffic siyo kupunga mkono kuongoza magari!

Hii ishu ni dharula lakini huku kwetu eti ni ratiba kabisa trafiki offocer kupunga mikono magari!
Hii huonesha uprimitive tulionao!

Dunia iko kwenye automation lakini sisi kutwa tuko analog.

Ni matumizi mabaya ya askari ambao taifa limewekeza pesa na nguvu kusomesha! Halafu wanakuja kuota vibarango kwa kupigwa na jua wakati tungeweza set automation
Hujui ameandika nini ila bado umechangia kitu husika

duh wabongo nuksi
 
Asubuhi na jioni ni muda ambao magari huwa mengi na askari wa usalama barabarani(Traffic) hujitahidi kupunguza adha hii kwa kuzipa kipaumbele barabara ambazo zina msongamano mkubwa zaidi wa magari.

Kinachotokea, mathalan upo kwenye barabara yenye magari pungufu, askari huyo ukakuzuia na ukawa mbele karibu na taa unaweza kulazimika kusubiri dakika 20 Traffic awajaze kwanza foleni ndio awaruhusu kwa pamoja, ratio yake ya kuruhusu ikawa dakika 20 kwenye msongamano kwa dakika 5 kusipo na msongamano(20:5), ukiwa kwenye msongamano unaweza kupita haraka zaidi na barabara iliyo nyeupe ukalaani traffic mpaka laana zikaisha.

Askari huyu wa Morocco pia anatoa muda mwingi zaidi kwa barabara yenye msongamano(Mwenge-Mjini) lakini anavunja kwenye makundi zile dakika nyingi kutowaweka watu, mfano badala ya kuwa 20:5 inakuwa 5:1. Kila baada ya dakika 5, anaziondoa gari chache zilizo kwenye barabara isiyo na kipaumbele, trafffic wengine unaombea uwe kwenye barabara yenye msongamano ili upite haraka kuliko kugandishwa kwenye barabara zisizo na magari mengi.
si ni yule bonge palee!!yuko vzr sana aisee!!
 
Si hapa Ubungo tuna kajamaa kanavaa kofia ya pikipiki (helmet) muda wote. Akikusimamisha we andaa buku 10 hivi hivi hauchomoki.
 
Sijui umeandika nini!

Kazi ya traffic siyo kupunga mkono kuongoza magari!

Hii ishu ni dharula lakini huku kwetu eti ni ratiba kabisa trafiki offocer kupunga mikono magari!
Hii huonesha uprimitive tulionao!

Dunia iko kwenye automation lakini sisi kutwa tuko analog.

Ni matumizi mabaya ya askari ambao taifa limewekeza pesa na nguvu kusomesha! Halafu wanakuja kuota vibarango kwa kupigwa na jua wakati tungeweza set automation
ume nena vyema kabisa,najiuliza ata mm kwa nn traffic anaongoza magari wakati kuna trafic light zingetakiwa kufanya kazi iyoo?
ushauri wangu traffic angetakiwa awe kama observer kuangalia kama sheria zina fuatwa.
#traffic akiwa road follen asipo kuwepo hamna folen.
 
ume nena vyema kabisa,najiuliza ata mm kwa nn traffic anaongoza magari wakati kuna trafic light zingetakiwa kufanya kazi iyoo?
ushauri wangu traffic angetakiwa awe kama observer kuangalia kama sheria zina fuatwa.
#traffic akiwa road follen asipo kuwepo hamna folen.
Nakumbukuka miaka ya nyuma baada ya maneno kama haya haya kuwa mengi, siku moja traffic hawakutokea barabarani siku hiyo, ilikuwa ni balaa.

What they do! Traffic wako barabara zote mjini, wanawasiliana changamoto za foleni zilizopo na ku-act accordingly, taa inaweza kuruhusu upande ambao hauna gari hata moja na kuendeleza foleni upande wenye foleni..
 
Nakumbukuka miaka ya nyuma baada ya maneno kama haya haya kuwa mengi, siku moja traffic hawakutokea barabarani siku hiyo, ilikuwa ni balaa.

What they do! Traffic wako barabara zote mjini, wanawasiliana changamoto za foleni zilizopo na ku-act accordingly, taa inaweza kuruhusu upande ambao hauna gari hata moja na kuendeleza foleni upande wenye foleni..
Hizo ni programm tu, ni jambo la kuongeza mda upande wa magari mengi!
Ishu ya kuprogram taa tu hiyo
 
Kabisa yupo yule mfupi mweusi hivi ana kakitambi ka kiaina,
Kuna wakati tuliambiwa sifa ya polisi ni urefu na kutokuwa na kitambi ili awe na uwezo wa kutupa hatua ndefu na kumdhibiti mhalifu kwa tanganyika jeki, sasa huyu aliingiiaje huko
 
Askari huyu wa Morocco pia anatoa muda mwingi zaidi kwa barabara yenye msongamano(Mwenge-Mjini) lakini anavunja kwenye makundi zile dakika nyingi kutowaweka watu, mfano badala ya kuwa 20:5 inakuwa 5:1. Kila baada ya dakika 5, anaziondoa gari chache zilizo kwenye barabara isiyo na kipaumbele
Kwa askari wetu hii akili alipewa na mtu mwenye upana sana wa kufikiri kama wewe hivi, inahitaji kufikiri mambo zaidi ya kawaida ili uje na matokeo hayo.

Nashauri Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani amchukue huyo akawafundishe wengine ili:
  1. Kuondoa adha ya foleni sugu kama Mwenge
  2. Kuondoa dhana ya hesabu kuwa somo gumu huku ttukilitumia kila siku bila kujijua
  3. Kuondoa ujuaji kwa askari wanaojiona wana nguvu sana wawappo kwenye mataa
 
Back
Top Bottom