Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
ASKARI WAZULU KATIKA JESHI LA WAJERUMANI 1890s - 1914
Kwa miaka mingi bila mafanikio nimekuwa nikitafuta picha ambayo inaonyesha askari mamluki waliokwenda kuchukuliwa Mozambique na Hermann von Wissmann kuja German Ostafrika kama Tanganyika ilivyokuwa ikijulikana kuja kupigana na Bushiri Al Harith na Mtwa Mkwawa.
Leo nimeipata picha hiyo hapo chini kutoka kumbukumbu za Tom von Prince afisa katika jeshi la Wajerumani aliyeshiriki katika vita hivi na nimeiweka hapa sote tuione.
(Huyu Tom Prince ndiye Mjerumani aliyemsaidia Chief Merere dhidi ya Mkwawa.
Kalenga Museum kuna barua aliyoandika Mtwa Mkwawa kwa hati za Kiarabu na ndani ya barua hii Mkwawa anaeleza usaliti wa Chief Merere wa Usangu.
Mkwawa alisilimishwa Abushiri bin Salim akawa Muislam na jina alilochagua ni Abdallah na Abushiri ndiye aliyemfunza kusoma na kuandika).
Pamoja na picha hii ya hawa askari Wazulu naweka maelezo kidogo:
''Efffendi Plantan, Sykes Mbuwane na mamluki wengine wa Kizulu walikuja Tanganyika katika meli ya kivita ya Wajerumani ikitokea Laurenco Marques iliyotia nanga Pangani mwaka 1894.
Wazulu hawa walitokea Inhambane, Msumbiji iliyokuwa ikitawaliwa na Wareno.
Kijiji chao kilikuwa kinajulikana kama Kwa Likunyi. Mjerumani alIyewaleta toka huko alikuwa na sifa ya kuwa mwanajeshi na mvumbuzi, Harmine von Wissman.
Wazulu wenyewe walikuwa wakiwaeleza watoto wao kuwa:
‘’Wajerumani waliweka mkataba na Mohosh, Chifu wa Inhambane nchini Msumbiji, kuwa watu wake watakwenda na Wajerumani hadi Tanganyika kupigana, wakakubliana kuwa ardhi yoyote watakayoteka watagawana sawasawa kati ya Wazulu na Wajerumani.
Wajerumani waliwachukua Wazulu katika meli hadi Pangani chini ya uongozi wa Mohosh, shujaa wa vita ambaye baadae alikuja kujulikana kwa jina la Effendi Plantan.’’
Kutoka kitabu cha Abdul Sykes (1998)
Huyu Affande Plantan ndiye baba yao Thomas Saudtz Plantan, Schneider Abdillah Plantan na Ramadhani Mashado Plantan na hawa wote walizaliwa Mozambique walikuja German Ostafrika wakiwa wakubwa.
Mtoto wa mwisho kuingia nchini alikuwa Mashado Plantan mwaka wa 1905.
Affande Plantan ndiye babu yake Bi. Maunda Plantan, mwalimu wa shule na mtangazaji wa kwanza mwanamke Sauti ya Dar es Salaam ilipoanzishwa mwaka wa 1952 na alikuwa English Service.
Kitu kitakachokushtua kwa haraka ukizungumza na Bi. Maunda ni ule ulimi wake katika kuzungumza Kiingereza.
Hali kadhalika baba yake mzazi Thomas Plantan alikuwa akizungumza Kijerumani fasaha kabisa na wakiizungumza lughs hii wakati wa utawala wa Waingereza.
Nimepata kuweka video ya Thomas Plantan akizungumza Kijerumani katika kumbukumbu ya kifo cha Paul von Lettow Vorbeck ambae alikuwa Mkuu wa Majeshi ya Ujerumani Tanganyika Vita Vya Kwanza Vya Dunia (1914 - 1918).
Ukoo wa Plantan una historia kubwa katika siasa za African Association, TAA, Al Jamiatul Islamiyya na TANU.
Schneider Plantan yeye alikuwa Secretary wa Daawat Islamiyya taasisi ya Kiislam iliyokuwa ikiongozwa na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir na ndiye aliyeongoza mapinduzi baridi kumtoa kaka yake, Thomas Plantan katika uongozi wa TAA na kuingiza uongozi wa vijana Abdul Sykes na Dr. Kyaruzi mwaka wa 1950.
Mashado Plantan alikuwa muhariri wa gazeti lake mwenyewe Zuhura.
Picha: Askari Wazulu, kitabu chenye kumbukumbu ya Tom von Prince na barua ya Mkwawa kwa Chief Merere.
Kwa miaka mingi bila mafanikio nimekuwa nikitafuta picha ambayo inaonyesha askari mamluki waliokwenda kuchukuliwa Mozambique na Hermann von Wissmann kuja German Ostafrika kama Tanganyika ilivyokuwa ikijulikana kuja kupigana na Bushiri Al Harith na Mtwa Mkwawa.
Leo nimeipata picha hiyo hapo chini kutoka kumbukumbu za Tom von Prince afisa katika jeshi la Wajerumani aliyeshiriki katika vita hivi na nimeiweka hapa sote tuione.
(Huyu Tom Prince ndiye Mjerumani aliyemsaidia Chief Merere dhidi ya Mkwawa.
Kalenga Museum kuna barua aliyoandika Mtwa Mkwawa kwa hati za Kiarabu na ndani ya barua hii Mkwawa anaeleza usaliti wa Chief Merere wa Usangu.
Mkwawa alisilimishwa Abushiri bin Salim akawa Muislam na jina alilochagua ni Abdallah na Abushiri ndiye aliyemfunza kusoma na kuandika).
Pamoja na picha hii ya hawa askari Wazulu naweka maelezo kidogo:
''Efffendi Plantan, Sykes Mbuwane na mamluki wengine wa Kizulu walikuja Tanganyika katika meli ya kivita ya Wajerumani ikitokea Laurenco Marques iliyotia nanga Pangani mwaka 1894.
Wazulu hawa walitokea Inhambane, Msumbiji iliyokuwa ikitawaliwa na Wareno.
Kijiji chao kilikuwa kinajulikana kama Kwa Likunyi. Mjerumani alIyewaleta toka huko alikuwa na sifa ya kuwa mwanajeshi na mvumbuzi, Harmine von Wissman.
Wazulu wenyewe walikuwa wakiwaeleza watoto wao kuwa:
‘’Wajerumani waliweka mkataba na Mohosh, Chifu wa Inhambane nchini Msumbiji, kuwa watu wake watakwenda na Wajerumani hadi Tanganyika kupigana, wakakubliana kuwa ardhi yoyote watakayoteka watagawana sawasawa kati ya Wazulu na Wajerumani.
Wajerumani waliwachukua Wazulu katika meli hadi Pangani chini ya uongozi wa Mohosh, shujaa wa vita ambaye baadae alikuja kujulikana kwa jina la Effendi Plantan.’’
Kutoka kitabu cha Abdul Sykes (1998)
Huyu Affande Plantan ndiye baba yao Thomas Saudtz Plantan, Schneider Abdillah Plantan na Ramadhani Mashado Plantan na hawa wote walizaliwa Mozambique walikuja German Ostafrika wakiwa wakubwa.
Mtoto wa mwisho kuingia nchini alikuwa Mashado Plantan mwaka wa 1905.
Affande Plantan ndiye babu yake Bi. Maunda Plantan, mwalimu wa shule na mtangazaji wa kwanza mwanamke Sauti ya Dar es Salaam ilipoanzishwa mwaka wa 1952 na alikuwa English Service.
Kitu kitakachokushtua kwa haraka ukizungumza na Bi. Maunda ni ule ulimi wake katika kuzungumza Kiingereza.
Hali kadhalika baba yake mzazi Thomas Plantan alikuwa akizungumza Kijerumani fasaha kabisa na wakiizungumza lughs hii wakati wa utawala wa Waingereza.
Nimepata kuweka video ya Thomas Plantan akizungumza Kijerumani katika kumbukumbu ya kifo cha Paul von Lettow Vorbeck ambae alikuwa Mkuu wa Majeshi ya Ujerumani Tanganyika Vita Vya Kwanza Vya Dunia (1914 - 1918).
Ukoo wa Plantan una historia kubwa katika siasa za African Association, TAA, Al Jamiatul Islamiyya na TANU.
Schneider Plantan yeye alikuwa Secretary wa Daawat Islamiyya taasisi ya Kiislam iliyokuwa ikiongozwa na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir na ndiye aliyeongoza mapinduzi baridi kumtoa kaka yake, Thomas Plantan katika uongozi wa TAA na kuingiza uongozi wa vijana Abdul Sykes na Dr. Kyaruzi mwaka wa 1950.
Mashado Plantan alikuwa muhariri wa gazeti lake mwenyewe Zuhura.
Picha: Askari Wazulu, kitabu chenye kumbukumbu ya Tom von Prince na barua ya Mkwawa kwa Chief Merere.