Askari wa Mikumi hawakagui magari bali wanakusanya hela wazi wazi bila woga

Kamgomoli

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2018
Posts
1,896
Reaction score
4,058
Askari (traffic) wa kituo cha ukaguzi wa magari eneo la Mikumi hawakagui magari bali wanachokifanya ni kukusanya hela tu! Kila basi wakilisimamisha trafic anaenda moja kwa moja kwa dereva anachukua 5000 kisha anaruhusu gari kuondoka.

"Bus" likikaribia tu konda anashika hela mkononi trafic anakuja anapewa hela yake na kuondoka bila woga. Au serikali iseme km imewaruhusu kufanya haya maana TAKUKURU ni km wamefumba macho.
 
 
Nakumbuka waliruhusiwa kuchukua pesa ya kubrashia viatu kipindi cha Jiwe.
 
Maeneo mengi bus wana kiasi chao na hizi gari zinazopiga safari za ndani wakipigwa faini ni ile wanasema amevunja mwiko au mkaidi na faini nyingi za trafik ni za magari ya watu binafsi hata mkipigwa tochi wao wanaimaliza kwa Ten wewe unaefatia utalipishwa faini ya elfu therathini hata utoe machozi wao wanaonyeshwa tuu na kutoa rushwa na kutembea Rushwa kwa hawa jamaa imekua ni jambo la kawaida sana...
 
Hela ya kununua kiwi nayo unaita rushwa ?
 
Mama Jana Kamwambia Wazi IGP Mpya Hafurahishwi Na Police Huko Njiani Ni Kama Hawana Mafunzo
Hapo Jeshi Lijipime Lenyewe Bila Kutafuta Huruma
Wamejizoesha Vibaya Sana
 
Yule utopolo alishawapa ruhusa wajipimie. Sasa unategemea nini!?
 
Wale ni kama kikoba yaani ni kama wamesajiliwa kisheria wanakera sana.
 
Yakikaguliwa kwa mujibu wa sheria hakuna litakalotembea barabarani...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…