Askofu anamiliki HAMMER ya 250million!

Status
Not open for further replies.
Suala siyo utajiri - kumtumikia Mungu hakumaanishi kuwa Maskini hata kidogo. Mungu aliahidi kwamba wote wamchao Bwana atawabariki na watakuwa vichwa wala si mikia.

Cha kujiuliza hapa ni kwa waumini wenyewe wanaotoa hizo fedha kwamba wanajua wanayemtolea? Tatizo ni kwamba watu wengi hawasomi Neno la Mungu wanangojea hao Maaskofu wawachagulie mistari ya kuwasomea. Na kwa sababu wanajua wanachokifanya wanatafuta mistari yenye utisho tu (k.m. usipotoa utalaaniwa). Na watu wengi wamegundua kwamba ukiwa na uwezo wa kuwashawishi watu wakakukubali wewe umeukata,kwa sababu zaka wanazotoa hakuna mtu anayeuliza isipokuwa ni Askofu tu. AKILI NI MALI.
 


tobe honest wewe umesema ukweli.. bnadamu we are so quick to judge... tunasahau kama hao wachungaji pia ni binadamu.. petro pia alimkana yesu na eafuasi wake wengine wote walimkimbia.. lakini walitubu..
mungu wetu ni mwenye huruma..
 
Natamani kuwa Askofu.....!

Kuna rafiki mmoja nimekutana nae amesema anaanzisha kanisa lake. Dah nilivyo kumbuka hii ya Hammer nikamwambia usinitose tupo pamoja kusaidiana kuchunga kondoo.
 
hata mm lakwangu linatoka mbinguni.. Katoliki

very good but ndugu yangu kumbuka kwa Mungu hakuna jina la dini. Soma
Yakobo 1:27 "Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao na kujilinda na dunia pasipo mawaa." Ubarikiwe!
 
Kuna rafiki mmoja nimekutana nae amesema anaanzisha kanisa lake. Dah nilivyo kumbuka hii ya Hammer nikamwambia usinitose tupo pamoja kusaidiana kuchunga kondoo.

sasa wewe utanunua nini??? wenzio tayari wameshanunua hammer
 
sasa wewe utanunua nini??? wenzio tayari wameshanunua hammer

Mi nimemwambia nitachangia mabati kwanza ili jengo la kanisa lisimame kisha tuanze kuvuna kondoo.
 
wajinga ndio waliwao......wanaojiita wachungaji wote wezi na matapeli tu.
wewe jamaa unaongea upuuzi mtupu, na umetumwa na shetani.angalia, watumishi wengine hao ukiwagusa, unakuwa unagusa mboni ya jicho la Mungu, unaweza ukajikuta unalaaniwa milele, imeandikwa "washindanao na Bwana watapondwa kabisa, Mungu akiwa upande wetu hakuna aliye juu yetu", hivyo ukianza kushindana na mtu wa Mungu, unashindana na Mungu mwenyewe na utapondwa kabisa hakika.

kama wana magari mazuri, waache, unajuaje kama Mungu ndo amewaambia wafanye hivo, ulitaka wavae kandambili zilizotoboka kama mashehe wenu? Mungu anasema mtenda kazi astahili posho lake, akifanyia kanisani, kuna share imewekwa kabisa itakayoenda moja kwa moja kwenye account yako. kama umekuwa na waumini wengi, ina maana share itakuwa kubwa, na unaweza kuitumia vyovyote upendavyo, kuhusu waumini, hakuna hata anayelalamika, huyo anayelalamika ni mnafiki mtumishi wa shetani na hajaokokoka na mwisho wake u karibu. WACHUNGAJI WENGINE wanapewa tu magari hayo. kuna mmoja ana makanisa Japan, yule wa Ubungo, gari alipewa na wajapani, makanisa ya kule yalimnunulia, kama ndo mnamsema yeye, kwasababu yeye ndo mwenye hio gari. ILE GARI ALIPEWA JAPAN, ana branch ya makanisa Korea, Japan na china, na anazungu dunia nzima kama beny hinn, watu wanaopona wanawapa magari na chochote anachotaka. fumba mdomo wako.
 
mimi naombeni kitengo cha kufundisha dini shule za sekondari(zanaki na jangwani)
 

Mtumishi wa Mungu bila shaka unaupako.....kama angekuwa anafanya kazi za kitumishi angeliuza na mali akagawia maskini. Kumbuka Yesu alikuwa na Kanzu moja tu!
 
Kumbuka Yesu alikuwa na Kanzu moja tu!

Hivi huyu mtumishi wa Mungu akiuza Hammer na kununua Starlet awe anatembelea atapungukiwa na nn? Na hizo pesa azipeleke Kilosa kwenye mafuriko.
 

mbona unaonekana kuwa mkali na uko radhi kutukana? Ni vyema ukajenga hoja kama ulivyoanza mwanzoni na si kuimalizia kwa hasira. kama ulivyofanya mpendwa. una uhakika ana makanisa japani na huko kwingine ulikotaja??
ni vigumu kuamini kwa mtu wa kawaida asiye mshirika katika kanisa hilo. Na wana JF wengi si washirika katika kanisa lenu.
Lakini vyo vyote viwanyo kuendesha gari hata la thamani ya dola bil kumi kama ni mpango wa Mungu, mtu yeyote ataendesha tu.
 
Hivi huyu mtumishi wa Mungu akiuza Hammer na kununua Starlet awe anatembelea atapungukiwa na nn? Na hizo pesa azipeleke Kilosa kwenye mafuriko.
hehehehe!
umenipiga NGUMI ya kustukiza hapo mpwaaz
 
hivi huyu mtumishi wa mungu akiuza hammer na kununua starlet awe anatembelea atapungukiwa na nn? Na hizo pesa azipeleke kilosa kwenye mafuriko.

ufisadi una sura nyingi sana
 
mi nimemwambia nitachangia mabati kwanza ili jengo la kanisa lisimame kisha tuanze kuvuna kondoo.
mpaka uwe na bati, fikiria hata banda la makuti tu!!!! Hujasikia?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…