Uchaguzi 2020 Askofu Bagonza: Makundi yetu kuelekea Uchaguzi Mkuu

Uchaguzi 2020 Askofu Bagonza: Makundi yetu kuelekea Uchaguzi Mkuu

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
VIONGOZI WA DINI
(Makundi Yetu)

Kama haitapendeza nisamehewe. Katika mchakato kuelekea Uchaguzi Mkuu, tumegawanyika makundi kadhaa:

1. Mitano Kwanza na Mitano tena. Kundi hili linaelekeza wapiga kura wachague mmojawapo kwa kutumia busara .

2. Mitano Kwanza tu. Kundi hili lina upande wa waziwazi. Linavumilia, halivumiliwi.

3. Mitano tena. Kundi hili lina upande wa waziwazi. Linavumiliwa, halivumilii.

4. Kimya kizito. Jambo lao wanalijua wenyewe. Hawataki wajulikane na hawataki kumwelekeza yeyote.

5. Tuombee Amani. Wanakerwa na kelele za kudai haki.

6. Tuombee haki na usewa. Kundi hili linakerwa na kelele za kudai amani TU.

Mgawanyiko huu unaashiria na kuweka mbele yetu jambo moja muhimu. Tunahitaji Tanzania ishinde; siyo mitano kwanza wala mitano tena. Roho ya visasi ishindwe na kiu ya damu ardhini ikome, na badala yake ardhi inywe maji isinywe damu.

Mungu Ibariki Tanzania
Ijalie kiu ya haki na njaa ya ukweli.
AMINA.
 
Huyu askofu athibitishe kwanza uraia wake aache uchochezi nchi ikiingia machafuko atakimbilia kwao Uganda
 
Tunahoji uraia wa Bagonza, mbona mitume wa kwenye Biblia hamna Mtanzania hata mmoja lakini hamjawahi kuwakosoa na maneno yao mnayaita matakatifu? Au ndio kusema nabii hakubaliki kwao?
Its too low
 
Back
Top Bottom