Askofu Bagonza: Vita ya Kagera VS Corona

Askofu Bagonza: Vita ya Kagera VS Corona

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
VITA YA KAGERA Vs CORONA

Wakati wa vita ya Kagera, Baba wa Taifa akiwa Rais wa Tanzania, alilazimika kufanya mabadiliko ya uongozi wa Mkoa wa Ziwa Magharibi. Mkoa huu ulikuwa katika eneo la msitari wa mbele vitani. Alimuondoa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa na kumteua mwingine anayendana na mabadiliko na hali halisi ardhini.

Mkuu wa mkoa aliyekuwepo alikimbilia kuhamisha familia yake na kutumia muda mwingi kuangalia usalama wake na wa familia yake.

Sasa tuko vitani na KIRUSI cha CORONA. Vita haina macho lakini kanuni za vita hazibadiliki.

Nasihi, nashauri, kanuni za vita zifuatwe. Uongozi wa makamanda ni muhimu kuliko ubora wa silaha.

Hekima ya Wanyambo inasema, "unaweza kumpenda sana binti yako lakini huwezi kuondoka naye kwenda kuolewa alikoolewa".

Tuko vitani DSM, kamanda asiyepunguza majeruhi wa vita, hatufai, hamfai jemedari Mkuu na anafaa kwa kuwasaidia maadui wetu.

Tusichelewe kama tulivyochelewa kusoma alama za nyakati. Hata kichaa ana jambo la kutufundisha.

Mchelea mwana kulia, hulia mwenyewe. Anayekataa kuambiwa jambo, hawezi kukataa kuona madhara ya kukataa kwake jambo hilo au kukataa kuona madhara ya jambo lenyewe.
 
Huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam unayetaka aondolewe hapo alipo nadhani utasubiri sana mdau kwani wewe siyo wa kwanza kulitaka hilo.
 
Ni vigumu kuelewa falsafa usipoituliza akili nayo ikakubali kutulia. Endelea kutafakari. Kwa mbali unakaribia kuelewa anachokimaanisha Baba Askofu..
Huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam unayetaka aondolewe hapo alipo nadhani utasubiri sana Mdau kwani Wewe siyo wa Kwanza kulitaka hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam unayetaka aondolewe hapo alipo nadhani utasubiri sana Mdau kwani Wewe siyo wa Kwanza kulitaka hilo.
Ametumia mkoa na vita ya kagera kama mfano Anazungumzia makamanda wa vita na uwezo wao wa kukabiliana na adui.

Pia anaongelea Zana ya ushindi wa vita kuwa ni pamoja na kuwa na majeruhi wachache na vifo. Kamanda anayeangamiza watu kwa umbumbu wake hatufai na hatakama hutupendi madhara ya umbumbu wa kamanda yataonekana
 
Kwahiyo akija mkuu wa mkoa mwengine Corona itaisha au yeye ndio itakuwa dawa ya Corona au? inabidi dunia ibadilishe viongozi wote maana wameshindwa kuidhibiti Corona

Sent from Tapatalk
 
Ametumia mkoa na vita ya kagera kama mfano Anazungumzia makamanda wa vita na uwezo wao wa kukabiliana na adui. Pia anaongelea Zana ya ushindi wa vita kuwa ni pamoja na kuwa na majeruhi wachache na vifo. Kamanda anayeangamiza watu kwa umbumbu wake hatufai na hatakama hutupendi madhara ya umbumbu wa kamanda yataonekana
Mkuu msamehe siunajua tena akili za lumumba.
 
Mavi
VITA YA KAGERA Vs CORONA

Wakati wa vita ya Kagera, Baba wa Taifa akiwa Rais wa Tanzania, alilazimika kufanya mabadiliko ya uongozi wa Mkoa wa Ziwa Magharibi. Mkoa huu ulikuwa katika eneo la msitari wa mbele vitani. Alimuondoa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa na kumteua mwingine anayendana na mabadiliko na hali halisi ardhini.

Mkuu wa mkoa aliyekuwepo alikimbilia kuhamisha familia yake na kutumia muda mwingi kuangalia usalama wake na wa familia yake.

Sasa tuko vitani na KIRUSI cha CORONA. Vita haina macho lakini kanuni za vita hazibadiliki.

Nasihi, nashauri, kanuni za vita zifuatwe. Uongozi wa makamanda ni muhimu kuliko ubora wa silaha.

Hekima ya Wanyambo inasema, "unaweza kumpenda sana binti yako lakini huwezi kuondoka naye kwenda kuolewa alikoolewa".

Tuko vitani DsM, kamanda asiyepunguza majeruhi wa vita, hatufai, hamfai jemedari Mkuu na anafaa kwa kuwasaidia maadui wetu.

Tusichelewe kama tulivyochelewa kusoma alama za nyakati. Hata kichaa ana jambo la kutufundisha.

Mchelea mwana kulia, hulia mwenyewe. Anayekataa kuambiwa jambo, hawezi kukataa kuona madhara ya kukataa kwake jambo hilo au kukataa kuona madhara ya jambo lenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yani ukiwa na akili za kibavicha ni tabu tupu, kwa akili ya askofu anafikiri kwamba dunia yote imeshindwa kudhibiti corona sababu ya ubovu wa makamanda au wa wakuu wa mikoa.?

Angekuwa na akili angalau angeongelea hili suala kiimani zaidi, kwamba Mungu anataka tufanye nini katika nyakati kama hizi au hiki janga lina maanisha nini kiimani.

Lakini nae kaja na mipasho ileile ya kiufipa. Tabu tupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yani ukiwa na akili za kibavicha ni tabu tupu, kwa akili ya askofu anafikiri kwamba dunia yote imeshindwa kudhibiti corona sababu ya ubovu wa makamanda au wa wakuu wa mikoa.?

Angekuwa na akili angalau angeongelea hili suala kiimani zaidi, kwamba Mungu anataka tufanye nini katika nyakati kama hizi au hiki janga lina maanisha nini kiimani.

Lakini nae kaja na mipasho ileile ya kiufipa. Tabu tupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kama hujaelewa ni kukaa kimya kuliko kuropoka utafikiri umekula kipolo kilicho chacha,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jina Askofu/ Padri/ Shekhe na majina mengine yanayowakilisha mjumbe wa Mungu, ni majina makubwa Sana, yanaheshima ya kipekee, Ni majina yanayopatikana Kwa sifa ya kubeba mamlaka nyingine, ili kulinda hadhi ya jina Hilo na kuondoa ukakasi na kuwapa watu Uhuru wa kuchambua mada mfu zinazoletwa na viongozi wa Dini, ni Bora wajisajiri hapa Kwa majina Yao halisi au majina feki, hii itawapa nafasi hata wafuasi wao kuchambua hoja zao

Maana kunahoja zingine zinaletwa hapa na viongozi wetu wa dini ni dhaifu na zinamaudhui ya kisiasa Wakati mamlaka walizozivaa hazina ushirika na siasa, Wala kuonesha upendeleo Kwa Baadhi ya makundi

Kwani, ikiwa Dunia itashindwa kuunganisha watu,moja Kwa moja inakuwa hata wao wanahusika kuibomoa jamii Kwa sababu ya kule kuegemea upande

Wakati umefika wa kila mtu asitumie cheo chake kuleta hofu ya watu kujadiri kile mtu anawasilisha hapa, Wajisajiri Kwa majina Yao, kama ni Jambo la kushauri watumie hivyo vyeo vyao, na nafasi ya kushauri hawa watu, wanaruhusiwa kuingia popote pale kupeleka Ushauri wao,

Vinginevyo vinavyofanyika hapa ni siasa Tu hakuna lingine,

Mtu ukizungumzia vita, mkuu wa nchi anaweza kutangaza vita hata akiwa kijijini kwetu kule Kimokela kule, na vita vtapiganwa

Raisi, mahali popote aweza kwenda na akafanya kituo na mipango yote ikaanza kufanyika Kutokea hapo alipo,

Je kwani akiwa Tu Dar-es-salaam ndio mipango mizuri ya kivita itafanikiwa!!

Baba Askofu, Kwanza ni lazima kutofautisha vita vya Kagera, vita ambavyo unapigana huku ukimuona adui.

Baba Askofu, nilidhani Kwa upande wenu kama watumishi wa Mungu,na Kwa vile vita hivi ni vya Kiroho, basi nyinyi ndio muwe maamiri Jeshi wa vita hivi, maana Biblia ninayoisoma Mimi, inaniambia, vita vya kiroho hupiganwa katika ulimwengu huo huo wa Kiroho, inakuwaje ninyi ndio mnaanza kulalamikia huu ulimwengu usioona chochote?
 
Back
Top Bottom