Askofu Bagonza: Yawezekana tulikuwa na Bunge bila Spika. Tunakoelekea tunaweza kuwa na Spika bila bunge

Askofu Bagonza: Yawezekana tulikuwa na Bunge bila Spika. Tunakoelekea tunaweza kuwa na Spika bila bunge

Kina Lema na wafuasi wao wanashangilia kama mazuzu bila kujua kama bunge ndio limepigwa nyundo mazima!

[emoji23][emoji23][emoji23]Nchi hii mataahira yapo kila kona
Limepigwa nyundo na nani.
 
"MAMA TUVUSHE ILI TUKUVUSHE. Kama una mashaka, Kuna MWAMBA mzoefu wa kuvusha, anaweza kusaidia."
Mwisho wa kunukuu
 
Na Hangaya huku kina Lema na misukule yao wakishangilia wakidhani wanamkomoa spika
Duh! wewe unamuona Lema tu unashangaza Kwahiyo UVCCM waliokuwa wanashinikiza ajiuzulu wao wamehuzunika?

Ndugai amevuna alichopanda.
 
Kina Lema na wafuasi wao wanashangilia kama mazuzu bila kujua kama bunge ndio limepigwa nyundo mazima!

[emoji23][emoji23][emoji23]Nchi hii mataahira yapo kila kona
Kimea,acha roho mbaya Lema nae ana haki ya kufurahi lau kwa mwaka mara moja.Hata miye acha nifurahi kwani mchimba kisima kadumbukia mwenyewe
 
... kwa Katiba hii, hakuna aliye salama hata Mama baada ya kuondoka madarakani hatakuwa na usalama siku "mwehu" akikamata madaraka kwa Katiba hii inayotoa mamlaka ya kiungu kwa mtawala! Katiba hii ni hatari mno kwa usalama wa taifa hususan kadiri makundi yanavyozidi kujiunda na kumea! Wenye busara na wastuke no matter wana itikadi gani.
Umenena maono makubwa sana. Acha waendelee kushupaza shingo
 
MAMA TUVUSHE, TUKUVUSHE

Yawezekana tulikuwa na Bunge bila Spika. Tunakoelekea tunaweza kuwa na Spika bila bunge. Bila ushabiki wala uzembe, tuangalie yafuatayo kwa makini:

1. Ukubwa wa CCM si mtaji, ni hatari. Bila upinzani imara, CCM ni sawa na chatu aliyefugwa ndani chungu cha mfinyanzi. Akikosa chakula atamla mfugaji.

2. Mihimili mitatu ya kufikirika ni hatari kwa nchi. Mmoja juu ya mingine ni kitanzi cha amani yetu.Tatizo Wanaofunikwa wanapenda.

3. Isiwe sheria wakuu wa mihimili kualikana kila wakati na kila mahali. Tunadhoofisha uadilifu wa mihimili yote. Kujipendekeza kumestawishwa kupitia huko.

4. Tuharamishe kujipendekeza kama tulivyoharamisha kukashifu Viongozi.

5. Mgombea binafsi anaweza kuwa Spika mzuri ili kuokoa uadilifu wa bunge. Kama mahakama isivyo na mahakimu/majaji wenye vyama na Spika asiwe na chama.

6. Afya ya Taifa ni mshikamano wa dini mbalimbali, makabila, jinsia, na itikadi mbalimbali. Mshindi anayechukua vyote ni sumu kwa amani yetu. Bora upinzani wa nje kuliko wa ndani.

7. Mjadala wa Haja ya kuwa na Katiba Mpya usitishwe. Huu ni wakati wa kutekeleza si kujadili.

8. Tangu uhuru tumetawaliwa na chama kimoja awamu tofauti. Kila awamu ina mambo yake. Zipo zilizotawanya na kurarua. Namlilia Mungu ili hii ya (6 au ya 5) iwe ya kuunganisha na kuponya majeraha. Anayesita zamu yake yaja.

9. Sakata la Ndugai (Ndugaigate) limefunua aibu yetu. Mfumo dume uko imara lakini pia bibi mwenye ndizi mbivu hakosi wajukuu wa kutuma mtoni. Waliojituma hongera, mliotumwa kuna siku mtatumwa kutafuta vitanzi vyenu.

10. MUNGU YUPO na ANATUONA. Si kila kitu tulichofanya 2020 kilibarikiwa na Mungu! Tukubali aturekebishe kwa sababu tumemtaja sana tangu 2020 na tumeshika misahafu tukaapa kwa jina lake. ZINGATIA HILI: Pasipo na haki huwa hayupo.

MAMA TUVUSHE ILI TUKUVUSHE. Kama una mashaka, Kuna MWAMBA mzoefu wa kuvusha, anaweza kusaidia.
Mheshimiwa Rais apate hili andiko kama lilivyo kwani twajua ni msomaji sana wa mitandao ya kijamii na JF ni sahihi kwake kujua hali ilivyo mitaani na vijiweni.
ulichosema ni kamili.
 
... sawa ila waombe Mungu waendelee kutawala wao; wasije wakajichanganya wakampa nafasi "mwehu" ataingiza taifa matatizoni. Tutaumia wote!
Mwehu ndiye aliyeondoka na ameishatuingiza kama Taifa matatizoni ndani nje, hatatokea mwingine kama yeye kwani Mungu ni fundi sana na amerekebisha alivyoona inafaa.
 
Kina Lema na wafuasi wao wanashangilia kama mazuzu bila kujua kama bunge ndio limepigwa nyundo mazima!

[emoji23][emoji23][emoji23]Nchi hii mataahira yapo kila kona
Tafakari hoja namba 9 naye amefurahi yaliyo mpata Ndugai na kuonesha aibu na ubovu wa katiba yetu. Ungana nasi kudai katiba.
 
Nani katumbukia?

Limetumbukia bunge siyo Ndugai
Mbona lilikuwa tayari lipo shimoni, kuondoka kwa Ndugai ndiko kunatupa nafasi na ari ya kuhalalisha madai ya katiba mpya. Ooh acha tufurahi Kisha tuungane kuanza kutekeleza madai ya katiba mpya.
 
Kina Lema na wafuasi wao wanashangilia kama mazuzu bila kujua kama bunge ndio limepigwa nyundo mazima!

[emoji23][emoji23][emoji23]Nchi hii mataahira yapo kila kona
Bunge lilijipinga nyundo lenyewe siku nyingi sana.ya Leo ni matokeo ya maamuzi yaliyofanywa na bunge lenyewe kwa kufunga ndoa na serikali badala yakuwa msimamizi na mshauri wa serikali.atake asitake tutamuongezea muda tu.ulitegemea Pana bunge hapo?
 
Nafasi ya Spika na naibu wake iwe ya kuajiriwa, vigezo viwekwe watu watume CV interview ya wazi tena mubashara kwenye tv (wakenya wanafanya hili wanapomtafuta jaji mkuu na msaidizi wake).

Kwa utaratibu huu hata chama tawala kikiwa Ada Tadea, yaliyotokea yatatokea tu. Kuna watu sehemu walikua wanasema Job angekaza mbona Nancy Pelosi alichana speech ya Trump, kitu wanachosahau Pelosi alichana Speech ya Rais M-republican haiwezi kuchana ya Biden.
 
Back
Top Bottom