Askofu Benson Bagonza: Viongozi wana nguvu sana katika vyama kuliko wanachama. Dola inatumika kuingilia chaguzi ndani za vyama vya siasa!

Mbangaizaji wa Taifa

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
493
Reaction score
844
Anaandika Rev Dkt BENSON BAGONZA

"Tatizo kubwa la hivi vyama vyetu vya upinzani vikianzishwa hugeuzwa kuwa vyama vya watu badala ya kuwa vyama vya wanachama.

Viongozi hufikia hatua ya kuviita vyama vyao.

Wanachama wanapaswa kuwa makini na kusimamia wajibu wao wa kutoruhusu mamlaka yao ya kutoa maamuzi ya mwisho kwenye chama yasipokwe na viongozi"-BBagonza

https://www.facebook.com/
View: https://www.facebook.com/share/v/19epb6kYUi/
 

maoni yenye mtazamo huo aliwahi kuyatoa pia dhidi ya kanisa lake, baada ya Askofu Dr.Alex Malalusa kurejea uongozini, yeke akibaki anakodoa macho na makasiriko yake, bila hata walau kupendekezwa kushika nafasi au wadhifa wa ukuu wa kanisa.

Nadhani Askofu Bagonza na Tundu Lisu wanashabihiana katika hulka ya chuki, uadui, uhasama, mdomo na makelele dhidi ya waandamizi wenzao wengine ndani ya taasisi walizomo ndio maana hukataliwa tangu hatua za mwanzo kabisaa kwenye chaguzi za taasisi zao 🐒
 
Bagonza wewe unaondka lini kwenye Uaskofu?
 
Kanisani kwako waumini wana mamlaka gani juu yako? Wewe ni Aloha na Omega...wanakuwa na mamlaka ya kutoa sadaka, wakishaitoa mamlaka yao yamekwisha sawa na vyama vya siasa, in a different version
 
Bangonza alivyoambiwa aachane na siasa kipindi JPM yeye aliamua kutafuta cheap popularity na sifa za kijinga za bavichaa ona Sasa machawa wa mbowe wanavyomuana kavu na kumdharilisha baada ya kutofautiana mtazamo
 
Kanisani kwako waumini wana mamlaka gani juu yako? Wewe ni Aloha na Omega...wanakuwa na mamlaka ya kutoa sadaka, wakishaitoa mamlaka yao yamekwisha sawa na vyama vya siasa, in a different version
Chadema wanshukia kama mwewe mtume wao baada ya kutofautiana mtizamo
 
Siasa ni nyoko ndo maana kama hunufaiki nayo basi achana nayo maana Tanzania hakuna wanasiasa Bali kunawajasiliasiasa na machawa kazaa
 
Hakuna mtu yoyote mwenye akili ataelewa eti Mbowe anasema hadi afikishe miaka 68 ndio astaafu, hoja ya hovyo kabisa kuwahi kutolewa na mtu.

Mbowe hana hoja ya kuendelea kuiongoza chadema, hana mipango mipya, hana mikakati, hana sera mpya, hana chochote kipya watu watakachopata baada ya miaka yake 21 ya uongozi.

Mbaya zaidi serikali inampigania Mbowe abaki madarakani, aendelee kuongoza chama, hapa ndip unapata harufu ya mzoga wa mbwa uliooza, harufu mbaya sana na wala huhitaji hata D 2, unahitaji kua ulifika darasa la nne tu unatosha kunusa hiyo harufu.

Ccm wanamtega mbowe kisha mwakani wammalize, hapa wanajifanya kumpenda, mwakani baada ya uchaguzi wanamgeuka, chadema itakua na legitimacy ipi ya kutaka mabadiliko ya kimfumo hapa nchini kama mwenyekiti wao anang'ang'ania madaraka, watawezaje kuisema ccm imeng'ang'ania madaraka miaka 65?

Chadema, it was good to know you sir, rest in peace.
 
Bagonza wewe unaondka lini kwenye Uaskofu?
Katiba ya uaskofu inasema umri wa kustaafu ni miaka 75 kama hakuna changamoto za kiàfya.
Katiba ya Mbowe inasema ni miaka 68 kàma baba mkwe.
 
Askofu hakuandika, alizungumza katika mahojiano.
Hakuzungumzia upinzani tu bali vyama vyote ikiwemo CCM (nimesikiliza ulichoweka mwenyewe).
 
Ukiachana na hulka ya Askofu, una mtazamo gani juu ya maoni na ushauri wake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…