Askofu Cheyo aonya matumizi ya mitandao ya kijamii

Askofu Cheyo aonya matumizi ya mitandao ya kijamii

Besta Mlagila

Senior Member
Joined
May 29, 2018
Posts
101
Reaction score
191
Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi, Alinikisa Cheyo ameonya wale wote wanaotumia mitandao ya kijamii kuandika mambo machafu na kutukana wengine kuwa wanahatarisha amani ya nchi.

Askofu Cheyo amesema hayo, Jumatano Desemba 25,2019 wakati akitoa salamu za Krismasi katika ibada la Kanisa la Moravian Viwawa mjini Wilayani Mbozi mkoani Songwe kuwa amani na umoja wa nchi unapaswa kulindwa na kila mmoja ili watu waweze kufanya kazi ya kujiletea maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla.

Alisema "Wapo wenzetu ambao wanatumia vibaya elimu na uhuru wa habari kuharibu amani yetu, aidha kwa kutumika na watu wasioitakia mema nchi yetu na hao nawaambia nchi hii ndiyo tuliyopewa na Mungu tunapaswa kuilinda," amesema Askofu Cheyo.

Askofu Cheyo ametumia pia nafasi hiyo kutuma salamu za kumtakia heri Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa kazi njema ya kuliongoza Taifa hili
 
Mwambieni cheyo kuwa serikali ilisema haifanyikazi na maneno ya kwenye mitandao sasa imekuwaje leo wanahangaika na mitandao?
 
VWAWA na VIWAWA! Havina uhusiano kwani Vwawa iko Mbozi ila Viwawa bado haifahamiki iko wapi.
 
Inawezekana sadaka ya Krisimasi haikujaa kapu moja kwahiyo hasira zake akazirushia mitaani. Matusi, matusi, matusi mbona hatuyaoni mitandaoni! Usipounga mkono juhudi unaitwa unatukana!
 
Askofu wa Moravian anayejitambua ni mmoja tu - yule anayeitwa Askofu Mkuu Mwamakula.
 
Inawezekana sadaka ya Krisimasi haikujaa kapu moja kwahiyo hasira zake akazirushia mitaani. Matusi, matusi, matusi mbona hatuyaoni mitandaoni! Usipounga mkono juhudi unaitwa unatukana!

Budget ya sadaka imeamia kwenye bando.
 
Budget ya sadaka imeamia kwenye bando.
Baada ya sadaka kupungua wengine wao wameungana na kuanza kumshambulia Bulldozer kuwa anauza maji! ooh anauza mafuta! Wameanzisha mtindo ovu wa kuwataka waumini wao wapeleke picha zao kanisani! Ili kuwadhibiti wasiwakimbie na wameanzisha bahasha za michango! Wanahasira na bando kuwanyang'anya sadaka.
 
Back
Top Bottom