Uchaguzi 2020 Askofu Emmaus Mwamakula: OCD Bukoba na RPC Kagera, Tundu Lissu yuko salama kwa kiasi gani?

Uchaguzi 2020 Askofu Emmaus Mwamakula: OCD Bukoba na RPC Kagera, Tundu Lissu yuko salama kwa kiasi gani?

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
Anaandika Askofu EMMAUS BANDIKILE MWAMAKULA....

TUNDU LISSU YUKO SALAMA KWA KIASI GANI?

Nayaandika haya kama Askofu! Ndiyo! Askofu aliye katika Msafara wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Tundu Lissu.

Tarehe 23 Septemba 2020, Msafara wa Tundu Lissu uliwasili Bukoba. Ulipofika Jamhuri Road katika Ofisi ya CCM, mawe yalianza kuporomoshwa kutoka katika jengo la ghorofa ambalo lina Ofisi za CCM.

Warusha mawe walivaa sare za CCM wakiwa katika Ofisi za CCM. Chini ya jengo kulikuwa na watu wazima waliokuwa wamevalia sare za CCM. Kama hiyo haikutosha, pembeni kulikuwa na Askari Polisi ambao hawakuchukua hatua zozote!

Msafara wa Mheshimiwa Lissu ulikuwa unaongozwa na Gari Polisi ambalo kwa kuwa lilikuwa mbele zaidi huenda hawakuona (huenda hawa hawana hatia).

Tukio la jana limetupa maswali mengi sana. Ikiwa mambo kama haya yanaweza kufanywa mchana kweupe na watu wanaojulikana mbele ya macho ya Askari Polisi, iweje wakati wa usiku?

Hivi OCD wa Bukoba na RPC wa Kagera wamelichukuliaje tukio hilo? Wale Askari Polisi waliokuwa wanawatazama CCM wakimrushia mawe Lissu walikwenda kutoa ulinzi ili CCM watimize zoezi lile? Uongozi wa CCM Wilaya, Mkoa na Taifa, unalichukuliaje jambo hili?

Mawe yale yaliyokuwa yakilenga kichwa cha Lissu aliyekuwa akiwapungia mikono watu akiwa amesimama yaliishia katika mikono ya Wasaidizi wake waliokuwa wakipangua mawe yale.

Mimi kama Askofu, ninawatahadharisha Jeshi la Polisi na vyombo vya dola kwa ujumla kuongeza umakini na uwajibikaji katika eneo la ulinzi wa Wagombea wote wa Urais akiwemo Lissu.

Ninawaomba CCM walichunguze tukio la Bukoba na wachukue hatua na kuhakikisha kuwa Ofisi zao hazihifadhi watu wa vurugu.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
 
Wapenda amani hawalipizi, wanamwachia Mungu awapende zaidi, maana wanashindana na muujiza unaotembea
Kuna muda unamwomba Mungu alafu unaingia kwenye mapambano unawakumbuka Anti baraka.....
 
Viongozi wengine wa dini wanapaswa kutangaza Amani kwa wote na si kujificha wakiogopa dhihaka na pengine wanadhani kukaa kimya kwenye udhalimu kama huo uliotokea bukoba kwao ni kuonyesha wana Mungu wa kweli kumbe hata shetani anatumika kuwanyamazisha pasipo wao kujua.
 
Known by the republic , hao vijana walitumwa kwa maelekezo toka juu kwa Mhutu maana yeye ukiukaji wa Haki za binadamu na kuumiza watu ndio anapenda sadist wa kihutu . bipolar disorder .
 
Huyu kibaraka wenu Emma wenyewe mnamuita Askofu, kikiwaka hapa tunaanza naye mchochezi mkubwa, aulize Rwanda maaskofu wa hovyo hovyo kama huyu walifanywaje kwa uchochezi wao, yaani kwake yeye haki kutendeka mpaka aone Lissu anashinda sio???
But na wewe msikilize huyo askofu wako alichosema, siyo kumlaumu ana haki kumtia moyo kondoo wake but kashuhudia kondoo huyo huyo akivamiwa na mbwa mwitu wakitaka kumla..!
 
Huyu kibaraka wenu Emma wenyewe mnamuita Askofu, kikiwaka hapa tunaanza naye mchochezi mkubwa, aulize Rwanda maaskofu wa hovyo hovyo kama huyu walifanywaje kwa uchochezi wao, yaani kwake yeye haki kutendeka mpaka aone Lissu anashinda sio???
Mtu kurushiwa mawe, tena mgombea urais wa JMT ww unaona ni sawa?
Angerushiwa Pombe ungefurahi?
 
Askofu anaacha kuchunga kondoo anazunguka na wanasiasa huyu ana tofauti na gwajima wote ni walewale
 
Askofu anaacha kuchunga kondoo anazunguka na wanasiasa huyu ana tofauti na gwajima wote ni walewale
Anatimiza majukumu na wajibu wake kwa jamii.. kondoo wake wapo kati ya jamii. Siyo Kama wale wachumia tumbo wanaotetea kwa hila huu utawala wa kikoloni
 
Anatimiza majukumu na wajibu wake kwa jamii.. kondoo wake wapo kati ya jamii. Siyo Kama wale wachumia tumbo wanaotetea kwa hila huu utawala wa kikoloni
Anatafuta kick majukumu ya kwenye siasa wote na Gwajima ni matapeli wanaotumia dini
 
Mnaye kichaa mwenye faili mirembe anayedai yeye hataki maendeleo ya vitu, wakati huo huo leo nimeliona limo ndani ya basi la mwendokasi!! hivi nyie misukule mnadhani mgombea wenu ni mzima kiakili kweli??
Basi la mwendokasi ni la umma
 
Back
Top Bottom