#COVID19 Askofu Gwajima: Chanjo ya Corona ni hatari, ni chapa ya mpinga Kristo, Mataifa kututenga kwa sababu hatujachanjwa ni mwanzo wa Uchumi wetu kukua

Kwani serikali imeshakataa hizi chanjo? Hivi tumefikaje hadi na kuwa na watu kama hawa. Nilikuwa nina matumaini kuwa miaka inavizidi kwenda uelewa unaongezeka kumbe ni kinyume chake!
 
Siyo kweli, this is just a naked lie, kugiribu watu wachache akili! Chajo ziko za aina tofauti na kutoka nchi tofauti(India ambayo ndo nzuri zaidi, China, Russia, UK, USA etc), should we assume kuwa hata chanjo ya surua, pepopunda, flu ni ya kishetani? Endeleeni kukusanya sadaka tu.
 
Gwajima ameongea point Sana lakini watu msio jielewa mnanwabwaja tu fanyeni utafiti kuhusu hii chanjo mme kaa kwenye kibodi tu hapo mnaandika vitu msivyo vijua
Ngwajima kawa Daktari lini!, We unafikiri upatikanaji wa dawa zote unazotumia au maarifa mengi ya kimaisha pamoja na technologia tumevipata bila ya upendo wa Muumba wetu.Watu walogundua Computer unayotumia kuweka maoni yako ,gari unalotumia,na umeme Tanesco wanaokukatiaga,wengi hata huyu mungu hawakumwamini.Lakini Muumba kavileta kupitia kwao,na akawabariki na utaalamu na ujuzi,leo wewe mwamini Mungu unajimwambafai hapa jf.

Ngwajima kuwa na kanisa hakumpi yeye uwezo wa kujua vitu vya kitaalam,kwa maneno mengine,kuamini Mungu hakuna maana unajua kila kitu cha kidunia,vitu vya kitaalam vinahitaji mawazo ya kitaamu sio porojo.

Ili ujue mambo ya madawa lazima uende shule na usomee,Elimu imeletqa na muumba na kuijua kunasaidia binadam kutatua matatizo yetu ya kimaisha,dini zinatuweka sawa ili tuitumie elimu vizuri.Chanjo zipo miaka na miaka na kuna magonjwa yamepotea sababu ya upatikanaji na chanjo,mfano mzuri ni Polio.

Enzi za mikate kuanguka toka angani zimepita,enzi hizi Muumba wetu katubariki na elimu ya kulima ngano,kutengeneza moto,na kuoka mkate,kinachohitajika ni kutumia akili na kuacha uvivu ili tule mkate,na hii ndo baraka ya zama zetu.
 
Mwenye masikio na asikie, hivi hua hamjiulizi kwanini kipindi flan corona ilislow down ila baada ya chanjo kuanza kurollout ghafla tukaambiwa kuna strain mpya ya hizo virus? mbaya zaidi sasa tunaambiwa moja ya hizo new variant zimepatikana kwa watu kutoka TZ?

Kama unaamua kua mbishi ni ruksa kwàni maisha ni yako na mwamuzi wa maisha yako ni wewe mwenyewe... Personally nasimama na GWAJIMA ila kama nabugi step Mungu aniongoze In Sha Allah...
 
Gwajima ameongea point Sana lakini watu msio jielewa mnanwabwaja tu fanyeni utafiti kuhusu hii chanjo mme kaa kwenye kibodi tu hapo mnaandika vitu msivyo vijua
Mkuu wewe uliyefanya utafiti kuhusu hii chanjo tujuze tusichokijua.
 
Hivi wabongo mmelogwa na nani ?
 
Kwani Askofu anatumia cha Arusha??

Anavyoongea ni kama Mwanakijiji ambaye hajui a wala b

Sijaelewa chanjo inahusiana nini na Uchumi wetu.

Nawasikitikia waumini wake ambao wametoka majumbani kwao kwenda kula chakula cha roho alafu badala yake wanaambiwa hayo

Poor him
 
Kauli kama hizi ni bora kama mtu akikaa nazo binafsi
 
Maswala ya Afya ya Watanzania tuiachie wizara ya afya, Pia masuala ya uchumiwetu wa leo na ule wa kesho tuwaachie watalamu wa Uchumi!
Ni jambo la hatari sana kuingiza siasa kwenye masuala ya afya au uchumi! Wanasiasa siku zote ni watu wanaoongea tu bila kuwa na kipimo au data, wala scale ya jambo husika, hivyo kuna uwezekano mkubwa mkandanganywa uwongo mkavu na mkajikuta mnaumia wenyewe na vizazi vyenu!
Nashauri hili kanisa kama lina mkuu mwingine zaid ya huyu Gwajima lingempiga marufuku ya kufanya shuguli za kiroho abakie akitumikia siasa kwanza kwa miaka 5 ya ubunge wake!
 
huyu mpuuzi ni tapeli
Nilianza kuwa na mashaka naye alipohaidi kununua Train kwa ajili ya SGR sijakaa sawa mwaka jana anatoa ahadi ya kuwapeleka wapiga kura wake Marekani akichaguliwa.

Ukipiga hesabu ya Wakazi wa Kawe X nauli ya USA kwenda na kurudi + Expenses za kula na hotel nikaoa hapa anatapeli watu tu 😂
 
Wazungu wangetaka kutuumiza wangekuwa washatumaliza tangia zamani,kumbuka chanjo zote za watoto zinatoka kwao!! Huo Ukimwi wameleta kondomu na ARV,tatizo wabongo wanapenda ngono sana bila kujikinga ndio maana tunapukutika!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…