#COVID19 Askofu Gwajima Kaathiriwa na Filamu za Hollywood "Fiction movies" Pamoja na Mambo dhahania

#COVID19 Askofu Gwajima Kaathiriwa na Filamu za Hollywood "Fiction movies" Pamoja na Mambo dhahania

Na kaswali kamoja tu ivi kwanini hamjibu hoja zake?


Hii nchi inachekesha Sana.
Sasa hoja ya Gwajima ni ipi ili ijibiwe?

Mtu anaongea porojo zake ambazo hazina MANTIKI alafu unategemea apewe hoja zenye MANTIKI. Wewe uliona wapi mambo ya hivyo??

Yaani mtu aangalie Filamu ya Hulk, au Batman alafu akuambie inawezekana mtu akawa vile, utamjibu nini Kama sio akili za kitoto.

Gwajima Hana hoja isipokuwa anatumia haki yake kutoa maoni yake ya Filamu za Hollywood
 
Ni chizi pekee anayeweza msikiliza na kuamini wasemacho dk Gwajima na dk Molleli ambao miezi kitatu tu waliuaminisha umma kwamba kuvaa barakoa na kupata chanjo ni hatari kwa maisha na ustawi wa watanzania.

Wakahamasisha watu wajifukize na kula maliamao na matango. Shubamiti!!!
Viongozi wangapi walipingana na Jiwe? ... ilibaki tu kila mtu akilinda ngozi yake ... ili familia yake iendelee kumuona!
 
Hii nchi inachekesha Sana.
Sasa hoja ya Gwajima ni ipi ili ijibiwe?

Mtu anaongea porojo zake ambazo hazina MANTIKI alafu unategemea apewe hoja zenye MANTIKI. Wewe uliona wapi mambo ya hivyo??

Yaani mtu aangalie Filamu ya Hulk, au Batman alafu akuambie inawezekana mtu akawa vile, utamjibu nini Kama sio akili za kitoto.

Gwajima Hana hoja isipokuwa anatumia haki yake kutoa maoni yake ya Filamu za Hollywood

nini umuhimu wa chanjo kama mtu akichanja bado anaweza kuambukizwa, chanjo inamana gani kama mtu akichanjwa bado inambidi asikae kwenye mikusanyiko? nini maana ya chanjo kama nikichanja bado naendelea kuvaa barakoa? chanjo inaulazima gani kama nikichanja bado naweza kuumwa corona na nikafa kabisa, nini tofauti kati ya aliye chanjwa na asie chanjwa? gwajiboy ana hoja na inabidi zijibiwe na kama kupinga chanjo ayo mataifa mnayo yaabudu hata wao raia wao wanawasiwasi na hizo chanjo na juzi tu kulikuwa na maandamano ufaransa marekani wametoa adi ofa ya dolla mia kwa kila raia atakae chanjwa, kuna kitu nyuma ya chanjo ila usiniulize ni nini?
 
We sema tu unatetea ugali huna lolote. Hao wazungu wanaosambaza clip za madhara ya hiyo chanjo kuhusu kutumika kwa nano technology unawazungumziaje au nao ni mafala na mbona wao huko kwao ambako ndo kitovu cha hiyo biashara hatujasikia wakikamatwa.

Bwana dalali ebu tupeleke polepole
... hiyo nanotechnology anayoongelea Gwajima ni 'pure science fiction' ukilinganisha na nanotechnology halisi ambayo bado ipo kwenye mapambazuko yake ... yaani Gwajiboy anaongelea njozi za NANOTECHNOLOGY!
NB: Naotechnology ikifikia level za Gwajiboy basi hata Robots zitakuwa 'self aware' na ataweza kuzihubiri GOSPEL!
 
Tangu aseme ule mkono sio wake ni wa baunsa sina ham nae tena yan
Nashaangaa sana watu wanaomtazama kwa jicho la uaskofu..mshenz,mzinzi,muongo kimacho macho[emoji15] hivi unamuogopaje huyo mtu!!!
 
nini umuhimu wa chanjo kama mtu akichanja bado anaweza kuambukizwa, chanjo inamana gani kama mtu akichanjwa bado inambidi asikae kwenye mikusanyiko? nini maana ya chanjo kama nikichanja bado naendelea kuvaa barakoa? chanjo inaulazima gani kama nikichanja bado naweza kuumwa corona na nikafa kabisa, nini tofauti kati ya aliye chanjwa na asie chanjwa? gwajiboy ana hoja na inabidi zijibiwe na kama kupinga chanjo ayo mataifa mnayo yaabudu hata wao raia wao wanawasiwasi na hizo chanjo na juzi tu kulikuwa na maandamano ufaransa marekani wametoa adi ofa ya dolla mia kwa kila raia atakae chanjwa, kuna kitu nyuma ya chanjo ila usiniulize ni nini?


Hayo yote uliyoyauliza mbona yameshaelezewa hata humu JF.
 
Hayo yote uliyoyauliza mbona yameshaelezewa hata humu JF.

mkuu tunaomba uyajibu tafadhali itapendeza sana kama yakijibiwa ili tumuaibishe gwajiboy aache kutuchonganisha na serikali yetu pendwa sana
 
Sasa Kama mtu hujawahi kupande Ndege na huna mpango wa kwenda nchi za mbali unafikiri hili la Chanjo linakuhusu Mkuu?

Binafsi siiogopi hiyo Chanjo, yaani niogope kisa nimemsikia muangalia Filamu za kizombi akinitisha 😃😃😃
Nakushauri uingie kwenye tovuti ya CDC ujionee mwenyewe mambo ya zombie preparedness sio tu mnakimbilia kumhuku Gwaji boy
 
Sasa Kama mtu hujawahi kupande Ndege na huna mpango wa kwenda nchi za mbali unafikiri hili la Chanjo linakuhusu Mkuu?

Binafsi siiogopi hiyo Chanjo, yaani niogope kisa nimemsikia muangalia Filamu za kizombi akinitisha 😃😃😃
😂😂😂 ndege
Unaenda wapi na hizo ndege mkuu?
 
Nakushauri uingie kwenye tovuti ya CDC ujionee mwenyewe mambo ya zombie preparedness sio tu mnakimbilia kumhuku Gwaji boy


Nilitegemea ungenambia niende sehemu Fulani hapa duniani nitaonana na hao mazombi sasa wewe unanieleza kwenye Tovuti zenye Fiksi Mkuu.

Kuna Fiction stories, MOVIES, na hizo websites
 
mkuu tunaomba uyajibu tafadhali itapendeza sana kama yakijibiwa ili tumuaibishe gwajiboy aache kutuchonganisha na serikali yetu pendwa sana


Huwezi muaibisha mtu Kama Gwajima, mtu anayeishi kidhahania huwezi muaibisha kabisa.
 
Nilitegemea ungenambia niende sehemu Fulani hapa duniani nitaonana na hao mazombi sasa wewe unanieleza kwenye Tovuti zenye Fiksi Mkuu.

Kuna Fiction stories, MOVIES, na hizo websites
Kama walichokiandika CDC ni fix kwa mjibu wako basi hata product wanazozitoa pia ni fix. Au huelewi CDC ni akina nani hapa duniani.

Yani kifupi WHO ni tawi tu ambalo liko attached na shina liitwalo CDC

Na kuhusu uzombie mbona wamefanikiwa sana kuwatengeneza. Angalia jamii inayokuzunguka hapo hujaona mazombie kweli. Hivi kwa akili ya kawaida mwanamke unaweza tembea uchi balabalani tena mchana kweupe kweli? Labda hujanielewa namaanisha uvaaji wa nguo za kulalia ambazo kama si kuonyesha laivu maumbile ya siri basi yatachorwa bila kificho, huo si uzombi ni nini.

Uvaaji wa nywele za maiti wa kizungu ili tu afanane na mzungu(kujikana nafsi) mpaka wengine zinatoa harufu ya panya aliekuafa kichwani si uzombie ni nini

Mtoto wa kiume kupaka makeup na kutoboa masikio sasa wengine wanapaka mpaka lip shine hujaona uzombie hapo

Watoto wetu siku hizi hawafundishiki yani ni vilaza hatari mpaka imepelekea serikali kupanua goli ili angalau ionekane wamefalu wengi huo si uzombie pia?

Hiyo ni mifano michache sana ya zombie praredness
Eb ww nambie uzombi unautarajia ni upi
 
Kama walichokiandika CDC ni fix kwa mjibu wako basi hata product wanazozitoa pia ni fix. Au huelewi CDC ni akina nani hapa duniani.

Yani kifupi WHO ni tawi tu ambalo liko attached na shina liitwalo CDC

Na kuhusu uzombie mbona wamefanikiwa sana kuwatengeneza. Angalia jamii inayokuzunguka hapo hujaona mazombie kweli. Hivi kwa akili ya kawaida mwanamke unaweza tembea uchi balabalani tena mchana kweupe kweli? Labda hujanielewa namaanisha uvaaji wa nguo za kulalia ambazo kama si kuonyesha laivu maumbile ya siri basi yatachorwa bila kificho, huo si uzombi ni nini.

Uvaaji wa nywele za maiti wa kizungu ili tu afanane na mzungu(kujikana nafsi) mpaka wengine zinatoa harufu ya panya aliekuafa kichwani si uzombie ni nini

Mtoto wa kiume kupaka makeup na kutoboa masikio sasa wengine wanapaka mpaka lip shine hujaona uzombie hapo

Watoto wetu siku hizi hawafundishiki yani ni vilaza hatari mpaka imepelekea serikali kupanua goli ili angalau ionekane wamefalu wengi huo si uzombie pia?

Hiyo ni mifano michache sana ya zombie praredness
Eb ww nambie uzombi unautarajia ni upi


Wewe unazungumzia ishu za kimaadili, mabadiliko ya kiutamaduni, NK.

Hapa tunazungumzia ishu kibaiolojia
 
Hivi Kwa Teknolojia iliyopo Kwa akili yako unaamini kabisa maneno anayoongea Gwajima na watu wa Aina zake??

Mimi ni mtunzi wa stori, nafahamu mambo mengi anayopendelea kuyasema Gwajima yamejikita katika fictions Stories or movies ambazo wengi WA Watanzania hawazijui.

Gwajima Hana tofauti kubwa na ndugu yangu Mshana Jr kwenye mambo ya stori za kubuni tuu
Shia sio Gwajima, tatizo hili walilianza wenyewe wataalamu, wamebadili gear angani ghafla bin vu bila maelezo ya kutosha.

Hawa ndiyo waliotupoteza wala siyo Askofu Gwajima.
 
Shia sio Gwajima, tatizo hili walilianza wenyewe wataalamu, wamebadili gear angani ghafla bin vu bila maelezo ya kutosha.

Hawa ndiyo waliotupoteza wala siyo Askofu Gwajima.



Ni kweli kabisa.

Basi hoja ya Gwajima ilipaswa iwe Kwa nini hao Viongozi wamebadilisha Gear angani, na sio hizo hadithi zake anazozitolea kwenye Hollywood
 
GWAJIMA AMEATHIRIWA NA FILAMU ZA HOLLYWOOD "FICTION MOVIES" PAMOJA NA MAMBO DHAHANIA.

Na, Robert Heriel.

Gwajima anaonekana ni muumini mkubwa wa filamu za kimarekani "Hollywood", hasa zile fiction movies, adventure movies na Horror movies.
Ukimsikiliza Kwa umakini mkubwa Ndugu Gwajima utakuungana na Mimi kuwa, tayari anaathari mbaya ya Filamu hizo.
Mbali na athari za Filamu za Hollywood lakini pia AMEATHIRIWA na mambo DHAHANIA, mambo ya kusadikika, mambo ya kufikirika ambayo kimsingi hayawezekaniki.

Sio ajabu Gwajima, ukimsikia akijitapa kuwa yeye ananguvu mpaka za kufufua wafu, kurejesha misukule. Mtu yeyote wa namna hiyo AMEATHIRIWA kisaikolojia na Kiroho.

Ukikaa na watu Kama kina Gwajima sio ajabu kwenye Stori zao ukiwasikia wakisema wanaouwezo wa kupaa angani Kama Spiderman au Batman, wenyewe watakuambia wanaouwezo wa kuruka juu kupitia nguvu za Yule wamwitaye Yesu.

Gwajima Hana tofauti kubwa na wala unga "madawa ya kulevya", ambao mawazo Yao mengi ni Kama wapo ndotoni, sio ajabu wakajiona wapo Marekani ilhali kiuhalisia wapo Buza Kwa mpalange huko.

Gwajima na watu wote wa dizaini yake, sio ajabu akakupa kikombe cha chai ya Kahawa alafu akakuambia ukinywa utapona UKIMWI, au gonjwa lolote kubwa.

Kumuamini Gwajima au watu dizaini yake itakupasa uwe na akili na mtazamo Kama wake, aidha uwe imeathiriwa na Filamu za Hollywood au unapenda mambo dhahania ambayo ni fiksi tuu.

Gwajima ni Aina ya watu Kama kinjektile Ngwale, Mzee wa maji maji. Yaani Wazee wa fiksi fiksi tuu. Gwajima ni Aina Ile Ile ya watu Kama kina Kibwetere.

Kumsikiliza Gwajima labda iwe Kwa kujifurahisha, kujiburudisha, au Comedy tuu.

Ingawaje kuna wakati anaweza kuongea mambo ya msingi lakini mara nyingi akiongea mambo asiyo na utaalamu nayo hujikuta akipata athari za Filamu za Hollywood na mambo ya dhahania.

Juzi nilimsikiliza nikacheka Sana, yaani Gwajima anatafuta istilahi ya kitaalamu ngumu ngumu ambayo waumini wake hawaijui kisha huilezea kuipa nguvu hoja zake.

Jambo moja la hakika na ambalo Gwajima anaweza kujivunia ni uwezo wa kujieleza na kushawishi watu hasa WAVIVU WA KUFIKIRI,
Watu dizaini ya Gwajima wengi wao wamejaliwa Ushawishi na uwezo mkubwa wa kujieleza. Kwenye biashara Kama za Mtandaoni Kama Qnet,Aim Global, Rifaro na biashara za namna hiyo watu Kama Gwajima ni wamoto, yaani wakija kukushawishi ujue umekwisha.

Watu Kama Gwajima wanaposhikilia msimamo hasa kwenye ishu wasizo na utaalamu nazo, huwa na Agenda ZIFUATAZO

1. Kuvumisha jina lake.
Watu mashuhuri wa dizaini ya kina Gwajima, wakiona jina limepoa Kwa kitambo, hutafuta kitu cha kuinuka nacho.
Gwajima anajua baada ya kuwa opposite na Serikali na kuipinga basi lazima atakutwa na misuko suko ambayo itamuimarisha zaidi kuliko kumfifisha.
Gwajima hata akiwekwa ndani Leo hii, kwake ni faida. Maana lengo lake litakuwa limetimia.

2. Kurejesha Imani ya waumini wake.
Mbali na Gwajima kujitetea baada ya video ya ngono iliyovuja yenye Sura yake lakini bado waumini wengi Imani zao zilishuka. Baadhi yao waliacha hata kwenda kanisani kwake.
Hivyo Kitendo cha Gwajima kushikilia msimamo wake kuhusu Chanjo ya Corona kutarejesha Imani ya waliorudi nyuma na ikiwezekana kupata waumini wapya.

Zingatia, Watanzania wengi wameathiriwa na mambo dhahania zaidi kuliko halisia. Watu Kama Gwajima hupendwa zaidi kwenye jamii Kama ya kitanzania.

3. Kuitikisa SERIKALI.
Gwajima hakuwahi kwenda kinyume na serikali ya awamu ya tano licha ya kuwa na mapungufu mengi. Gwajima nilishawahi kumsikia wakati wa Kikwete akiishambulia serikali, lakini awamu ya tano hakuwahi kuthubutu kuleta vyokovyoko zake.

Kuingia Kwa Samia Suluhu, Gwajima kaanza tena kujifaraguza Kama mtu mwenye kusimamia ukweli(kile akionacho ni ukweli) Gwajima ningekuwa upande wake Kama angekuwa msema ukweli pasipo hofu wakati awamu ya tano, lakini ukimya wake kipindi kile na zaidi alikuwa akipongeza pekeake kunanipa mashaka.

Wapo Maaskofu Kama kina Mwingira, Kakobe, Mwamakula, Fredrick Shoo, na Yule wa Bukoba hawa walishajipambanua kuwa ni wasema ukweli ingawaje ukweli wao unaigusa tuu serikali ya CCM na mara nyingi hawakosoi Vyama pinzani. Hata hivyo nikitaka kuwatetea naweza sema kuwa, siku zote Mdogo anatetewa, na mkubwa ndiye anayelaumiwa.

Gwajima Hana tofauti na Wale wanaokupigia hesabu za kilimo cha Tikitiki wakati hawajawahi kulima tikiti, ni watu wa nadharia na mambo dhahania.

Gwajima hafai kwenye mambo Sirius kwani anaweza ingiza hadithi Kwa ishu halisi.

Gwajima ni Wale wanaokuambia hadithi za 666 sijui Freemason, vitu ambavyo Kwa lugha rahisi ni matokeo ya Utandawazi.

Vitu Kama Passport (Hati za kusafiria), Vitambulisho vya NIDA, Tin number, Kadi za Benk ni Teknolojia ya namna ya kupata Huduma tuu havina uhusiano wowote na mambo ya kiroho.
Hivyo sio ajabu miaka ijayo kadiri Teknolojia inavyokuwa hiyo 666 ikawa ni sehemu Teknolojia ya kumrahisishia kupata Huduma.

Kuliko kutembea na makarabrasha mengi kwenye mkoba, ni Bora upigwe chapa moja sehemu yoyote ya mwili kurahisisha upewaji wa Huduma mbalimbali.

Watu Kama kina Gwajima hupenda kutisha watu ili nafasi Yao nao iwepo.

Ndio maana wao kila kitu huweza kukitumia kutisha watu, sababu ni Ile ile, nayo ni ili nafasi Yao nayo ionekane, nao wazingatiwe.

Sio ajabu watu dizaini ya Gwajima, ukiwasikia wakizungumza ishu za kulogwa, sijui uchawi, sijui majini, yaani wao mambo Yao Kwa 90% huyachukulia kidhahania dhahania.

Wakati mambo dhahania kwenye maisha ya binadamu hayazidi hata Asilimia 10%.

Mwisho, Gwajima Hana makosa. Jamii bado ndiyo yenye makosa Kwa sababu IPO katika Giza la Ujinga.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Morogoro
gwajiboy ni wa mirembe tu
 
Back
Top Bottom