Askofu Mkombo(Ktoka DRC) amevunja Duka Usiku wa Kuamukia Leo!!!!

Amia kwa Nabii Flora, hana matatizo
Huyo mie ndio namtaka maana hawa Manabii wa kiume wote wamejaa ulaghai na kuchuma mali za waumini wao labda haka ka kike katakuwa na huruma.
Hizi DINI zinazoibuka siku hizi zimejaa kelele na kutisha km hapo huyo Papaa anavyomtisha huyo Mama Abeid kwanini haonekani tena (mm km ni Mke wangu ningemkunja huyo Nabii na nimeshindwa mpigia simu kwani tumepewa Mwenye duka ( Mama Abeid) (0715 448519)
Labda cha kumwambia
Asome Biblia Isaya 42 : 1-4 Hatalia wala kupiga kelele wala kupaza sauti barabarani Na wakimbishia awsomee Mathayo 12: 19-21 Hatakuwa na Ubishi wala kupiga kelele
Huyu Papaa ni pepo la Ngono linamsumbua tu baada ya kumuona Mama wa watu keshamshtukia anaanza mambo Ya
Kibwetere wa Uganda au Johannes wa Guyana kutumia Principle ya kuwateketeza Wafuasi wake wote
 
Huyu askofu ana skendo nyingi sana hapa Tanzania tangu alipokuwa Mbeya!! Sijui kama usalama wa taifa unafanya kazi kwa namna gani katika nchi hii!! Naamini kuna ma informer wanapita hapa!! Hebu fanyieni kazi kutafiti kazi halisi za hawa wanaojiita maskofu, manabii, mitume hasa toka nchi za nje!! Nchi iko hatarini!! Kuna mengi yanayoendelea kwa askofu mkombo kupitia kivuli cha huduma ya kanisa!!
 
umeandika vzr na umejitahidi kufikisha ujumbe wako kwa mujibu wa ufahamu wako,lkn pia nami ktk kupitia maelezo yako,napenda kuchangia kama ifuatavyo, usijipe unyonge kwa kuunganisha habari tofauti, mhalifu ni mhalifu tu, awe mkristo au muislamu, yule mchungaji wa kutoka nigeria aliyekamatwa na madawa ya kulevya kesi iko mahakama kuu, na mtuhumiwa yuko mahabusu akiendekea na kesi yake, kama unavyojua kesi za mahakama kuu huchukua muda mrefu,huyo askofu kama kweli kavunja duka la mpangaji wake basi ni jukumu la huyo mwenye duka kufungua kesi ili sheria ichukue mkondo wake, lkn jiulize walikuwa na mkataba wa upangaji au walipangishana kienyejienyeji, ndugu yangu kumbuka mhalifu ni mhalifu.
 
Binadamu tunatakiwa tutulie mtu umezaliwa lutheran au katoliki iweje anajitokeza mtu anaanzisha kanisa lake unamfua kwani yeye ana mungu wa tofauti.

kiongozi watakwambia wanafwata miujiza. maana siku hizi mchungaji akimdondosha mtu hata kwa kumsukuma watu wanamiminika hao ohh anatoa mapepo. wapi ujanja mwingi siku hizi watu wabaki katika makanisa yao ya asili hawa saint fulani saint nanii , saint duniani nani kasema.
 
Naona hata hujielewi...

Kweli nyani haoni makalio yake hapa msikiti wa mtambani huwa wanatimuana ndani kwa bakora, halafu ponda anayemtetea alikuwa mfanyabiashara za magendo Kongo to Kigoma, Burundi to Kigoma.
 
Nayaona haya kuja kutokea ktk familia yangu.mama yangu kagawa nusu ya kiwanja kwa wapumbavu wajenge kanisa,hapa najipanga kwenda kuwatimua

ahahahahaaaaaaaaaa....pambana na udhalimu huu bila uoga mkuu
 
Sijuhi-sijui. Uhamuzi-uamuzi, sasa wewe unamuuliza mwenzio ana elimu ya kiwango gani, na wewe tukuulize shule uliyosoma ilikuwa haina somo la kiswahili?

Ilikuwa haina, hilo alikunikwaza kwenda vyuo vikuu, back to the point mada hii has nothing to do with masterly of swahili language, tunazungumzia hatari ya kuingiza mambo ya udini katika incidents za kawaida kama ili la Askofu kutoelewana na mpangaji wake.

Labda nikuhulize swali: Nikisema c-u -2-morrow ubongo wako utajazilizia nini kinacho kosekana! Basi binadamu Mungu ametuhumba ubongo wetu una uwezo mkubwa wa kusahihisha automatically kasoro bila ya kupoteza meaning, kiswahili kama kilivyo kingereza maneno mengi ni redundant, kama unaona nilicho andika akieleweki just ignore and move on, lakini ili la kupoteza muda ukijaribu kusahihisha grammar au spelling za wachangiaji kinaonyesha una an inbuilt trait ya complex ya aina fulani.

Labda nikukumbushe kwamba we didn't join JF kuandika white paper, hii si mara yako ya kwanza ku-pick up vitu vidogo vidogo na kujaribu ku-derail mada kwa kunitafuta mimi binafsi, unajaribu kutumia IDs tofauti - huna unacho changia kazi yako kujaribu ku "dot the i's and cross the t's basi.

Angekuwa KING COBRA ndiye kakwazika kwa majibu yangu ningemuelewa, sina shaka ailijuwa nilicho kuwa namaanisha sikuwa na nia mbaya naye.
 
Habari imekaa ki-upande mmoja zaidi! (mama Abedi) na isitoshe habari inasema kuna kundi lilikuja kuvunja usiku, je mama Abed ana uhakika gani kama lilitumwa na ASKOFU?
Contract ya kupangisha eneo la kanisa inasemaje, je alilipa kodi! je muda wake wa kupanga haukuwa umekwisha? mbona mama abedi haelezi hatua gani za mwanzo zilizochukuliwa na askofu kuikia kufunga duka?
"MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU"
 

Mkuu umenikumbusha kisanga cha GUYANA - hata mimi nilikuwa na wasi wasi sana na Manabii/Mitume hawa, wamewateka waumini wao kisaikolojia sana. Siku moja nilikumbuka tragedy ya GUYANA baada ya kuona waumini wa hapa BONGO walivyo kuwa hawana kauli mbele za MITUME/manabii WA SIKU HIZI - sijawahi kusikia mitume/manabii kwenye dini za kikristo i.e Katoriki, Luteli au Aglicana.

Nili wahi kufikilia hivi siku moja manabii hawa wakiwakusanya waumini wao na kuwapeleka camp fulani, alafu baadae wakawambia kunyweni Juice au Mvinyo iliyo changanywa na Cynide au Potassium Iodide labda na valium kwa kuamini kwamba kwa kufanya hivyo watakwenda peponi moja kwa moja. Je, wanaweza kuwa na ubavu wa kuwakatalia?
 
Sio jambo la kufurahiya jamani....Mungu atusaidie sana. ila ndugu usi question imani za watu khs utume na unabii muache Mungu mwenyewe ahukumu cha msingi if you are happy where you are ..well and good..waache wanaotafuta kushiba chakula cha kiroho zaidi as long as kuna amani..but it is more than enough mtu kwenda kwenye hayo makanisa akawa na peace of mind than doing nasty things.... imagine akina dada wasingekuwa wanahudhuria kwenye hizo ibada wakahamia kwenye majumba ya starehe kungekuwaje? kusingekalika hata kidogo...mmoja aki bugi step tumuombee arudi kundini otherwise God knows..Oh dear
 

Mungu akubariki na akutie katika kundi la waamuzi manake hukumu zimekuwa nyingi humu ndani mpaka tumekuwa wabaya kuliko hata Askofu mwenyewe
 

Raisi Muislamu, jaji mkuu muislamu, makamu wa raisi muislamu, Mkuu wa usalama wa taifa muislamu, mkuu wa polisi ni muialsmu lakini bado unalalamika ? kila kitu udini hatua hazijachukuliwa umeanza kulalamika ? kwanza inaelekea hujasoma uzi na kuulewa huyo aliyekamatwa si padri ila ni askofu rudia kusoma uzi, pili huyo mkongo anahaki kufungua kanisa TZ kama ilivyokuwa kwa Waarabu toka Arabuni kuuleta Uislamu Afrika, au Wazungu toka Ulaya kuleta Ukristo Afrika. Cha msingi hapa tatizo ni kuvunja sheria basi ? kuvunja sheria hakuna udini kama Ponda ameonewa nenda kawe shahidi wake.
 

Safi sana kwa kuupasua mfumo kristo
 
Kitoabu acha kuongelea na kulinganisha mambo usiyoyajua, na ambayo wala hayastahili kulinganishwa. Huo mnaouita "mfumo kristo" upo vichwani mwenu tu nyie ambao mnaota kutengeneza dola ya Kiislam chini ya Sharia.

Usiishie kusoma elimu akhera tu, soma na sheria za nchi ujue nchi inaendeshwaje, na haki inapatikana vipi. Nchi haiendeshwi kwa Biblia wala Quran, sasa sijui "mfumo kristo" au "mfumo Islam" unatoka wapi?

Mtu kama Ponda anafanya vurugu kwa kisingizio cha kutetea haki za Waislam. Hataki kutafuta haki kwa taratibu zilizowekwa. Pili anapingana na BAKWATA, kwani BAKWATA ni nani? Si ni Waislam kama yeye pia? Wakipingana naye anaingia mtaani kusambaza fitna na kujenga chuki kwamba kuna "mfumo kristo". Sasa sijui hiyo BAKWATA kuna Wakristo mle?

Kama anataka kufanya siasa ni bora afanye siasa rasmi. Siasa za kidini hazina mwisho mzuri. We jione kama Mtanzania kwanza, kisha Muislam. Ila ukiendekeza kuona Muislam kwanza halafu ndo Mtanzania basi kila siku utaona unaonewa.
 
Last edited by a moderator:

Unge relax ungekuwa umeandika kitu cha maana
 
Mimi nasema wanaowafuata maaskofu dizaini hiyo vichwani mwao watakuwa sinwazima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…