Askofu Munga, aadhimisha ibada(Albadir) ya kulaani waliomvamia Tundu Lissu

Askofu Munga, aadhimisha ibada(Albadir) ya kulaani waliomvamia Tundu Lissu

Bandiko lako limenigusa sana! Na kunihuzunisha kwa yanayoendelea,Tena kwenye hiyo kauli mbiu yao waliyoigundua sasa hivi"WAPOTEZWE WAMEZIDI".mungu ibariki tanzania
Ndivyo ilivyo ndugu yangu, tuko njia panda, lakini yana mwisho , tujikaze kiume madhalimu yasitumeze!!!
 
Mleta mada acha kupotosha .
Hakuna mahali ambapo Baba Askofu amesoma Albadiri .

Kilichofanyika ni Dua Maalum juu ya hali ya nchi na mambo ,matukio mbalimbali yanayoendelea yanayochangia kuondoa amani yetu na siyo Issue ya Lisuu pekee .!

Kibibilia Dua ni Maombi maalumu ambayo yanayofanywa kupitia Jina la Yesu Kristo Mungu aliye hai ili kuomba
Rehema juu ya uovu unaoendelea.

Katika dua hakuna laana au kuwaombea watu wapatwe na mabaya bali waache njia mbaya .

Dua ni rehema tofauti na Albadiri ambayo ni
..........
 
Mleta mgawanyiko mkubwa hapa nchini ni yule anayedai kuwa yeye ndiye "Mzalendo" na wengine wote wenye mawazo tofauti na mtazamo wake ni "Wasaliti"
Mvurugaji wa amani yetu ni yule anayewafukuza watu wengine kazi wakiwa na taaluma zao kwa kisingizio cha kukosa vyeti vya Form IV, huku wapambe wanaotumika kuvuruga amani wanasifiwa hata kama majina yao ya elimu ni feki.
Nenda kwenye Mkutano wowote wa kitaifa ujionee, hasa wa kiserikali jinsi ubaguzi ulivyotamalaki. Ukiwa upinzani hata kama una haki ya kutambulishwa watajifanya vipofu ilimradi jina lako lisisike.
Imejitokeza nadharia ya kishetani kwamba kuna kitu kinaitwa "Vita ya Uchumi" ambayo usipofikiri kama wao basi umekaribisha "Watu wasiojulikana" mlangoni.
Kwamba sasa "Watu wasiojulikana" ndio wamekuwa watetezi wakubwa wa serikali ya Chama cha Mapinduzi ni jambo lililo bayana. Ukiwauripoti Polisi unaona dhahiri jinsi Polisi wanavyowagwaya.
Leo hii inasikitisha na kutia kinyaa unapokutana na kada wa CCM anayetamba bila lepe la aibu kuwa: "Apotezwe tu naye amezidi" Yaani CCM iliyokuwa tayari kujikosoa na kukosolewa, leo imekuwa chama kinacholea ukatili dhidi ya walio na hoja kinzani.
Chama kilicholeta kauli mbiu ya "Kushindana bila kupigana," leo kimeishiwa hoja na kubakiza vitisho vinavyotumiwa na magenge ya "Wapotezaji"
Kwa hakika CCM IMEIVURUGA MAMA TANZANIA KWA SIASA ZA CHUKI NA VISASI!!!
Mhe. Askofu ombeni sana, maana tumeingiliwa, si na joka tu, bali pia na "Wakana Mungu" wenye kiu ya damu za raia wenzao!!!!!!!
Mkuu umelenga mule mule..
 
Aksante baba ubarikiwe sana kwa ukweli huo. Bado tunajidai kuwa tunapendwa kwa mabaya yote haya! Mungu tusamehe!
 
KKKT hakika mnajitahidi sana kupiga kichwani hawa viongozi wetu tofauti sana na madhehebu mengine yaliyopo nchini.
 
Nimeondoka na hili,
HAKUNA UZALENDO BILA UMOJA
Amina.
Nadhani dhana nzima ya mahubiri ya askofu imelala hapo. Kujifanya Mzalendo huku ukihubiri utengano huna tofauti na joka analokisema baba Askofu.
 
Mleta mgawanyiko mkubwa hapa nchini ni yule anayedai kuwa yeye ndiye "Mzalendo" na wengine wote wenye mawazo tofauti na mtazamo wake ni "Wasaliti"
Mvurugaji wa amani yetu ni yule anayewafukuza watu wengine kazi wakiwa na taaluma zao kwa kisingizio cha kukosa vyeti vya Form IV, huku wapambe wanaotumika kuvuruga amani wanasifiwa hata kama majina yao ya elimu ni feki.
Nenda kwenye Mkutano wowote wa kitaifa ujionee, hasa wa kiserikali jinsi ubaguzi ulivyotamalaki. Ukiwa upinzani hata kama una haki ya kutambulishwa watajifanya vipofu ilimradi jina lako lisisike.
Imejitokeza nadharia ya kishetani kwamba kuna kitu kinaitwa "Vita ya Uchumi" ambayo usipofikiri kama wao basi umekaribisha "Watu wasiojulikana" mlangoni.
Kwamba sasa "Watu wasiojulikana" ndio wamekuwa watetezi wakubwa wa serikali ya Chama cha Mapinduzi ni jambo lililo bayana. Ukiwauripoti Polisi unaona dhahiri jinsi Polisi wanavyowagwaya.
Leo hii inasikitisha na kutia kinyaa unapokutana na kada wa CCM anayetamba bila lepe la aibu kuwa: "Apotezwe tu naye amezidi" Yaani CCM iliyokuwa tayari kujikosoa na kukosolewa, leo imekuwa chama kinacholea ukatili dhidi ya walio na hoja kinzani.
Chama kilicholeta kauli mbiu ya "Kushindana bila kupigana," leo kimeishiwa hoja na kubakiza vitisho vinavyotumiwa na magenge ya "Wapotezaji"
Kwa hakika CCM IMEIVURUGA MAMA TANZANIA KWA SIASA ZA CHUKI NA VISASI!!!
Mhe. Askofu ombeni sana, maana tumeingiliwa, si na joka tu, bali pia na "Wakana Mungu" wenye kiu ya damu za raia wenzao!!!!!!!
Unajing'ata nini mkuu sema Magufuli na sio yule ambaye sijui anajifanya mzalendo
 
Back
Top Bottom