Askofu Mwamakula: Mwanafunzi wa kidato cha kwanza mwenye miaka 13 aswekwa Mahabusu kituo cha Polisi Kirumba

Askofu Mwamakula: Mwanafunzi wa kidato cha kwanza mwenye miaka 13 aswekwa Mahabusu kituo cha Polisi Kirumba

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
"Kati ya mahabusu wa kiume 48 waliokuwepo katika Kituo cha Kirumba, kuna mtoto mwenye umri wa miaka 13. Mtoto huyu, alimsogelea Askofu na kumueleza kwa masikitiko kisa chake. Kwamba siku moja aliamua kuchuma limao moja katika mlimao wa jirani yake ili aweke kwenye dagaa ili ale. Jirani yake ambaye ni mwanamke pamoja na watoto wake walimshukia kwa kipigo kizito mtoto yule wakimshambulia kuwa ni mwizi.

Mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina la Johnson Frank, anasoma Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari ya Ibungilo iliyoko Ilemela. Askofu anakumbuka kuwa mtoto yule alisema kuwa shuleni anajulikana kwa jina la Ibrahim Frank na kwamba anakaa na bibi yake kwani mama yake yupo Dar es Salaam. Bibi yake, Mama yake na hata Uongozi wa Shule yake hawajui kama yupo mahabusu. Lakini kwa umri kama ule mtoto kuchanganywa mahabusu na watu wazima ni jambo lililomuumiza sana Askofu.

Askofu anajiuliza kama Mwanza hakuna Mahabusu ya Watoto? Askofu anatoa wito kwa makundi ya kutetea haki za watoto kufika haraka sana katika Kituo cha Polisi Kirumba, Mwanza ili kuangalia namna ya kumsaida mtoto yule. Lakini pia mtoto yule anatakiwa kufanyiwa vipimo kwani alikuwa analalamika maumivu katika mkono wake wa kulia kutokana na kipigo alichokuwa ameshushiwa na mwenye mti wa mlimao. Mazingira hayakuruhusu kwa Askofu kupata picha ya mtoto yule." - Askofu Emmaus Mwamakula
 
Huko makanisani mwao wanapohubili huwa hawaulizi watu wenye shida ili wawasaidie kwa hizo sadaka na kufanya hao wenye shida kutoingia kwenye migogoro ya kisheria? Au mpaka wakutane mahabusu ndo waje kusimulia na kuona huruma kwa wenye shida?

Ni wajibu wa mwamakula kusaidia wenye shida kabla hawajaingia kwenye madhambi ya kujitafutia riziki.

Kwa kua ameamua kuwa mchungaji basi achunge na shida zao na sio kuwanyofoa kondoo sadaka bila kuwalisha kondoo wenye shida.
 
Huko makanisani mwao wanapohubili huwa hawaulizi watu wenye shida ili wawasaidie kwa hizo sadaka na kufanya hao wenye shida kutoingia kwenye migogoro ya kisheria?..
Kama kuna mtoto kwenu wa miaka 13, usingeandika hivyo. Mkuu hebu kaa upande wa kutetea watu, tetea wanao onewa. Mahubiri ya makanisani na kusaidia watoto(japo makanisa kweli yanasaidia watu), unaongeaje hivi ikiwa kweli unajali maumivu ya watu?

Unajipatia laana, na hautaiona itakapokupata, utaenda kuagua.

Waovu hawashindi.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Sawa inawezekana sio limao tu ......kwa umri wake inakuwa busara kuwa mahabusu moja na watu wazima..?
Jaribu kuwa Mzazi....je ingekuwa mtoto wako ndio kafiwa hivyo leo ungeandika haya..
Wewe na huyo askofu mwamakula mna uhakika huyo mtoto ana miaka 13? mumehakiki wapi?

pili mtoto huyo anasema shuleni anajulikana kama Ibrahim frank lakini mahabusu anajiita Johnson Frank kwa nini alibadili jina ghafla alipoingia mahabusu? akaandikisha jina tofauti kulikoni kama sio mhalifu mzoefu alikuwa anaficha nini? maana ASKOFU KASEMA HUYO MTOTO ALIJITAMBULISHA KWAKE KAMA JOHNSON FRANK wakati huko shule anajulikana kama Ibrahim FRank

Anaposema hakuna ajuaye yuko mahabusu watajuaje wakati kabadili jina alipoingia mahabusu
 
Wewe na huyo askofu mna uhakika huyo mtoto ana miaka 13? mumehakiki wapi?

pili mtoto huyo anasema shuleni anajulikana kama Ibrahim frank lakini mahabusu anajiita Johnson Frank kwa nini alibadili jina ghafla alipoingia mahabusu? akaandikisha jina tofauti kulikoni kama sio mhalifu mzoefu alikuwa anaficha nini?...
Hawa ni wale watoto walioshindikana mtaani. Inawezekana hata familia imeshamchoka wamemsusa.
 
Unadhani jela za watoto ziliundwa kwa ajili gani? Watoto wako shule huyo wenu veepe?
 
Back
Top Bottom