Askofu Mwamakula na matembezi ya hiyari

Askofu Mwamakula na matembezi ya hiyari

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
ASKOFU MWAMAKULA KUFANYA MIKUTANO JIJINI DAR ES SALAAM KABLA YA KWENDA MIKOANI!

Ndugu Watanzania na Jumuiya ya Kimataifa!

Ninapenda kuchukua nafasi hii kuwajulisha kuwa adhma yangu ya kuongoza "Matembezi ya Hiyari" kwa nchi nzima kwa lengo kuhamasisha umma kuhusu umuhimu na uhitaji wa Katiba Mpya iko palepale. Katika Mkoa wa Dar es Salaam ambao ndio tulipanga kuzindua Matembezi tarehe 16 Februari 2021, hatukufanya kwa kuwa mimi nilikamatwa na Jeshi la Polisi ambalo lilikuwa limejipanga kuvuruga Mpango wetu.

Kwa kuwa Jeshi la Polisi limenituhumu kuwa nilitaka kuchochea vurugu katika Mkoa wa Dar Es Salaam na kwa kuwa bado linaendelea na uchunguzi wake, kwa sababu hiyo, na ili kupisha uchunguzi wao, kutakuwa na mabadiliko kidogo katika ratiba na mpango wetu katika Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu namna ya kufanya Matembezi hayo. Hivyo, badala ya kufanya "Matembezi ya Hiyari" katika Mkoa wa Dar es Salaam tutakuwa tukifanya Mikutano ya Hadhara ya Hiyari" na "Mikutano ya Ndani ya Kumbi ya Hiyari". Mabadiliko hayo yanahusu mkoa wa Dar es Salaam tu.

Utaratibu huo unatarajia kuanza wakati wowote. Kabla ya kuanza kufanya, Wanasheria wangu watawasiliana na mamlaka husika na kuwapa taarifa kwa njia ya maandishi. Ratiba ya kufanya mikutano ya Hadhara na mikutano ya ndani katika Jiji la Dar es Salaam itatolewa wakati wo wote baadaye.

Hata hivyo, Mpango wa kufanya Matembezi katika Jiji la Dar es Salaam bado upo palepale. Nitashauriana na Wanasheria wangu kuhusu namna ya kufanya Matembezi hayo katika mazingira ambayo yatauhakikishia umma na dunia kwa ujumla kuwa yatakuwa ni "Matembezi ya Amani".

Tukimaliza hatua ya mikutano katika Jiji la Dar es Salaam tutaelekea mikoani ambako tutafanya "Matembezi ya Hiyari" au tutafanya Mikutano ya Hadhara au Mikutano ya Ndani au tutafanya vyote kulingana na mazingira ya kila Mkoa au Wilaya!

Washindi siku zote hawakati tamaa na wanaokata tamaa hawawezi kushinda (Quiters never win and winners never quit)! Hatuwezi sote kukaa chini na kuendelea kunung'unika chini kwa chini kama wanafiki badala ya kuchukua hatua! Dunia haijawahi kubadirishwa na kuboreshwa na waoga, wenye hofu na wavivu! Jiandae kuniunga mkono katika kampeni nzito za kiutu na kimaadili kuwahi kutokea katika nchi yetu.

Tamanio langu ni kuona Tanzania inaingia katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 ikiwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya! Tukiunganisha nguvu na tukiweka nia njema tutafanikiwa!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfutate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Awamu hii wachungaji wanapata taabu Sana ..... Kwani Yesu anasemaje au mchungaji ameamua kupambana mwenyewe
 
Watu wanawaza Corona na wengi wa wananchi wanapambania mlo wa kila siku.

Hivi kuna Mwananchi utamwambia aandamane kwa hiari eti kupigania katiba mpya nyakati hizi!?.. Hivi kuna mtu asiyejua Dunia nzima inaongelea Corona hadi Boko Haram na Al Shabaab wameenda likizo wakiogopa Corona, waweza kumshawishi mtu yeyote aandamane!?..

Mwenyewe ana msemo wake eti mwanakondoo ameshinda..
 
Tukiwaambia huyu Bishop wenu hazimtoshi kichwani hamuelewi. Watu wanawaza Corona na wengi wa wananchi wanapambania mlo wa kila siku. Hivi kuna Mwananchi utamwambia aandamane kwa hiari eti kupigania katiba mpya nyakati hizi!?.. Hivi kuna mtu asiyejua Dunia nzima inaongelea Corona hadi Boko Haram na Al Shabaab wameenda likizo wakiogopa Corona, waweza kumshawishi mtu yeyote aandamane!?.. Mwenyewe ana msemo wake eti mwanakondoo ameshinda..
Korona gani tena mkuu? Si tulisema Tz hatuna hii kitu? Si tulikubaliana tulishasaligi yakaisha? Sisi wala hatuwazi korona mkuu
 
Korona gani tena mkuu? Si tulisema Tz hatuna hii kitu? Si tulikubaliana tulishasaligi yakaisha? Sisi wala hatuwazi korona mkuu
Mlisema wewe na nani!?.. unajua hizi Siasa za Uccm na Ucdm zimeleta utapia mlo vichwani mwa vijana wengi. Uchangiaji wenu jamii forums umekaa kishambenga shambenga na unakuta ni wanaume na mna wake na watoto. Kwahiyo na wewe ukaamini hakuna Corona!??.. au unaongea mafumbo Kama waimba taarabu.
 
"Matembezi ya Hiyari kwa Amani".

Tamanio langu ni kuona Tanzania inaingia katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 ikiwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya! Tukiunganisha nguvu na tukiweka nia njema tutafanikiwa!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfutate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula

Tume huru na katiba mpya nchi Ni mahitaji ya haraka kwa raia...
 
Watu wanawaza Corona na wengi wa wananchi wanapambania mlo wa kila siku.

Hivi kuna Mwananchi utamwambia aandamane kwa hiari eti kupigania katiba mpya nyakati hizi!?.. Hivi kuna mtu asiyejua Dunia nzima inaongelea Corona hadi Boko Haram na Al Shabaab wameenda likizo wakiogopa Corona, waweza kumshawishi mtu yeyote aandamane!?..

Mwenyewe ana msemo wake eti mwanakondoo ameshinda..

Kama watu hawataandamana sio kwa hizo sababu unazosema, bali ni kwa hofu ya kutekwa, kuuwawa, ama kuhujumiwa kwenye shughuli zake za kuwaingizia kipato na huyu mlevi wa madaraka anayetaka kuendelea kukaa madarakani. Na sio kwamba hawataki katiba mpya, kwani watu wamechoka kuongozwa kwa shuruti.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mlisema wewe na nani!?.. unajua hizi Siasa za Uccm na Ucdm zimeleta utapia mlo vichwani mwa vijana wengi. Uchangiaji wenu jamii forums umekaa kishambenga shambenga na unakuta ni wanaume na mna wake na watoto. Kwahiyo na wewe ukaamini hakuna Corona!??.. au unaongea mafumbo Kama waimba taarabu.

Umelewa nini, hizo lugha za kutokuwa na Corona kila siku jiwe anazisema, hadi kusifiwa kuwa ameondoa corona.
 
Watu wanawaza Corona na wengi wa wananchi wanapambania mlo wa kila siku.

Hivi kuna Mwananchi utamwambia aandamane kwa hiari eti kupigania katiba mpya nyakati hizi!?.. Hivi kuna mtu asiyejua Dunia nzima inaongelea Corona hadi Boko Haram na Al Shabaab wameenda likizo wakiogopa Corona, waweza kumshawishi mtu yeyote aandamane!?..

Mwenyewe ana msemo wake eti mwanakondoo ameshinda..
kwa uchangiaji huu Sizani kama ww ni mwananch wa kawaida [emoji23][emoji23][emoji23] hakuna mwananchi asietaka Tume huru ya uchaguZ na Katiba mpya sizani kama ww ni Mtanzania wa kitaa kama Sisi


Nb: like bas hapaaa [emoji85][emoji85]
 
Watu wanawaza Corona na wengi wa wananchi wanapambania mlo wa kila siku.

Hivi kuna Mwananchi utamwambia aandamane kwa hiari eti kupigania katiba mpya nyakati hizi!?.. Hivi kuna mtu asiyejua Dunia nzima inaongelea Corona hadi Boko Haram na Al Shabaab wameenda likizo wakiogopa Corona, waweza kumshawishi mtu yeyote aandamane!?..

Mwenyewe ana msemo wake eti mwanakondoo ameshinda..

Alafu katika moja ya mbinu ya viongozi wa afrika nikufanya Maisha yawe magumu ili watawale.
 
Mungu mbariki mtumishi wako Askofu Mwamakula
Mjitokeze tu kwenye matembezi sio mumpige changa la macho kama mlivyofanya kwa akina Mange na Lisu.....watu wakaishia kutoa sapot kwenye keyboard tu
 
Mlisema wewe na nani!?.. unajua hizi Siasa za Uccm na Ucdm zimeleta utapia mlo vichwani mwa vijana wengi. Uchangiaji wenu jamii forums umekaa kishambenga shambenga na unakuta ni wanaume na mna wake na watoto. Kwahiyo na wewe ukaamini hakuna Corona!??.. au unaongea mafumbo Kama waimba taarabu.
Wewe na Mwigulu nchemba si ndo mlisema hamna corona? Akili za maccm
 
Mwanakondoo wa Mungu ameshinda!
Tumfuate.
Namuunga mkono Baba Askofu
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom