Askofu Shoo atoa neno kuhusu kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe

Askofu Shoo atoa neno kuhusu kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
%22_Dkt._Lilian_Mbowe_tunajua_mme_wako_mpendwa_ndugu_yetu_@freemanmbowetz_hajaweza_kuhuzuria_m...jpg


Akizungumza kwenye Ibada ya mazishi ya marehemu Johara Mtei , ambaye ni Mama Mkwe wa Freeman Mbowe , Aliyeko gerezani kutokana na kesi ya uzushi ya Ugaidi , amesema hata kama siasa ni mchezo mchafu lakini walio kwenye madaraka wajaribu kutenda haki badala ya kutenda mambo yanayovuka mipaka ya utu maana hayana mwisho mwema .

DR Shoo ametoboa siri kwamba yeye na maaskofu wenzake ndio waliomuita na ndio waliomshauri Mbowe kusitisha operesheni UKUTA ili kuepusha mauaji ya Raia wasio na hatia na akatii na kusitisha maandamano yale , Bila kumung'unya maneno Askofu Shoo amesikitishwa sana na kitendo cha Mbowe kusingiziwa Ugaidi , na Amemuomba Dr Lilian ambaye ni Mke wa Mbowe kuwa na uvumilivu

 
Raia kuandamana ni haki yao kisheria, na Mbowe kuwataka waandamane kwenye hiyo operation UKUTA alikuwa akitimiza/tekeleza haki yake kisheria.

Lakini Askofu kwa kujua unyama wa polisi wetu, akaona bora amtake Mbowe aache kuwahimiza raia waandamane ili kuwaepushe na majanga ambayo yangeweza kumkuta yeye pamoja na raia.

Hapa najifunza kitu, hii nchi sasa haiongozwi tena kwa kufuata sheria, wala na chama cha siasa, inaongozwa na vyombo vya dola, hawa jamaa wanalitumia jeshi la polisi kwa manufaa yao kisiasa.

Hali hii ikiachwa iendelee itasababisha huko mbele ya safari raia wawe sugu nao watafute njia ya kujilinda na madhila ya polisi, tukifika hapo CCM watavuna walichopanda.
 
Operation ukuta walimuita wakamkataza, kwanini Operation hii wakamuacha? Wameyataka wenyewe
 
Ugaidi siyo tangazo kwamba kila mtu ajue ni siri ya gaidi na gaidi tu!

Wakati mwingine kwenye familia unaweza kustukia mapolisi yamekuja kumshika mwanao kwa tuhuma za ujambazi bila ya mzazi kufahamu iwapo mwanaye alikuwa jambazi, sembuse na mbunge usiye kaaa naye kabisa
 
View attachment 1906402

Akizungumza kwenye Ibada ya mazishi ya marehemu Johara Mtei , ambaye ni Mama Mkwe wa Freeman Mbowe , Aliyeko gerezani kutokana na kesi ya uzushi ya Ugaidi , amesema hata kama siasa ni mchezo mchafu lakini walio kwenye madaraka wajaribu kutenda haki badala ya kutenda mambo yanayovuka mipaka ya utu maana hayana mwisho mwema .

DR Shoo ametoboa siri kwamba yeye na maaskofu wenzake ndio waliomuita na ndio waliomshauri Mbowe kusitisha operesheni UKUTA ili kuepusha mauaji ya Raia wasio na hatia na akatii na kusitisha maandamano yale , Bila kumung'unya maneno Askofu Shoo amesikitishwa sana na kitendo cha Mbowe kusingiziwa Ugaidi , na Amemuomba Dr Lilian ambaye ni Mke wa Mbowe kuwa na uvumilivu .
Askofu Shoo ni mmoja wa Viongozi wa Kidini wapenda HAKI na huwa hamungunyi maneno kama baadhi ya Viongozi wa kidini walio wanafiki!!
 
Ma kwenye hili la Mbowe, namwona huyu Mama ni shetani mwingine kwa umbile la mwanadamu wa jinsia ya kike.

Afanye lolote, hata liwe jema kiasi gani, kwa huu ushetani alioufanya, watu wote wenye hekima, akili, wakweli wa nafsi na matendo, wanaothamini utu, haki, uhuru na demokrasia wamemweka katika thamani ya uchafu.

Kwa mara nyingine, tena tupo chini ya utawala wa shetani.
 
Back
Top Bottom