Asota jela miaka 9 baada ya rafiki yake aliyemuazimisha geto kumuua mpenzi wake. Kisa simu iliyopokea SMS ya mapenzi

Asota jela miaka 9 baada ya rafiki yake aliyemuazimisha geto kumuua mpenzi wake. Kisa simu iliyopokea SMS ya mapenzi

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Tumaini Mabula miaka 9 iliyopita alifika rafiki yake Justine Peter nyumbani kwake akiwa na mpenzi, rafiki yake alimuomba chumba chake alichopanga Mwananyamala akiwa na rafiki yake wa kike kwasababu yeye alikuwa anakaa kwa shemeji anayeishi na dada yake.

Tumaini alimpa maelekezo wakimaliza aache funguo kwa Mangi dukani lakini aliporudi mangi alikana kupewa funguo. Alipofika chumbani alikuta mwanamke(shemeji yake kwa Justine) akiwa amelala na macho yasiyofumba. Mwanzo alidhani ameamua 'kujirudisha' lakini alipofikika mwenyekiti wa mtaa akamwambia mwanamke husika amefariki.

Walipofika Polisi walimbeba Tumaini na safari yake ya kusota ikaanza rasmi, polisi walichukua alama za vidole zilizokuwa kwenye mwili wa marehemu zikiwemo za Justine na Tumaini alizoacha wakati anamuamsha. Justine alikimbia na walipofika kwa shemeji alipokuwa anaishi wakakuta nyumba nzima wameshahama na kuhamisha vitu usiku mmoja kabla yake.

Justine aliamua kwenda kuishi mpakani akiukimbia mji na kuogopa kukamatwa akiuza samaki wa Tanzania nchini Burundi. Siku moja alikumbana na askari wa uhamiaji na alipoulizwa ni raia wa nchi gani alisema Burundi lakini lafudhi nzuri ya Kiswahili chake iliwapa hofu maafisa uhamiaji wakaamua kuscan vidole vyake.

Alama zake za vidole zilijitokeza kuwa alikuwa anatafutwa kwa kesi ya mauaji, alama zilizochukuliwa wakati wa uchunguzi wa mwili wa marehemu.

Mwanzo Justine alijitetea kwamba hakujua marehemu alifariki na alimpiga bahati mbaya kisogoni baada ya mchumba wake kupigiwa simu mfululizo bila kupokea na baadae kutumiwa SMS mhusika akimlalamikia kutofika kwake wakati ameegesha mlango wazi akimsubiri yeye.

Changamoto aliyoipata Justine ni kukimbilia mpakani pamoja dada na shemeji yake kuhama usiku wa manane kama alijua hakufanya kitu.

Kwa hisani ya Millard
 
Hope's hii ni true story na ndio maana tunahitaji katiba mpya, maana katiba hii itatupa uwezo wa all suspects kuwa na haki zote hadi mahakama itoe hukumu, makosa yote yatakuwa yanapata dhamana, huu ni uonevu maana sidhani police waliweza to link mwenye chumba na crime scene, na pia sex ilifanyika why foresinc phothology report kuhusu mwili wa marehemu haikutumika hapo? Ndio maana magereza yetu yamejaa innocent guy's ndani mle, inahuzunisha sana.
 
Wacha hyo Kuna mchizi alikuwa anaishi na demu bila kumuoa demu alikuja kumfia kwa magonjwa yake yake ya tangu utotoni.

Wacha aisee wazazi wa demu walitaka kumfunga ila demu alijulikana kafa kwa ugonjwa wake wa matatizo ya kupumua jamaa kasota miaka 3 pia alifukuzwa kazi
 
Hata wenye nyumba wanaopangisha vijana wasio na wake wanatakiwa kuwaambia waziwazi kwamba ni marufuku kumwachia mtu na mpenzi wake kutumia chumba chake kwa sababu linaweza tokea tukio kama hilo na yeye akakimbia na kumwachia msala mwenye nyumba.
 
Wacha hyo Kuna mchizi alikuwa anaishi na demu bila kumuoa demu alikuja kumfia kwa magonjwa yake yake ya tangu utotoni .... Wacha aisee wazazi wa demu walitaka kumfunga ila demu alijulikana kafa kwa ugonjwa wake wa matatizo ya kupumua jamaa kasota miaka 3 pia alifukuzwa kazi
Yoooo nimesahau tunaishi in a shithole country!,again kwani ripoti ya kifo kutoka kwa phothologist haikusema sababu ya kifo!

opppps nimesahau kumbe toka afariki Professor Shaba(rip),nchi haijapata mwingine, nchi imejazaa MA na GPs
 
Huyo kamla Dem wa rafki yake,aache janja janja
 
Inasikitisha sana mtu hujaskiliza story nzima unakuja unaandika nonsense.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Mkuu,

Ulicholeta siyo story nzima
Bali Ni story ya upande mmoja
(Hatujaskia pia upande wa huyo unayemtuhumu kaua)

Kwaiyo
Unapoleta Uzi wako jf, Usitufunge wote ktk mawazo yako,yaan sote tufikiri unachofikiri wewe.

Na Hii Ndo maana Halisi ya HOME OF GREAT THINKERS
 
Kwan lazima mtu atumie geto lako gest zipo kibao had zingine shot time 2000 ukampe geto tatzo kutothamini mazingira yako unayoishi jitu lije na demu wake huko nilipe chumba ushenzi mkubwa huo.
 
Back
Top Bottom