Leo nd'o leo.
Macho ya watanzania wengi wapenda michezo yataelekezwa katika jiji la Birmingham. Katika uwanja wa Villa Park unaomilikiwa na klabu ya Aston villa kutakuwa na mtanange wa nusu fainali ya pili kati ya Aston villa na Leicester city.
Katika mechi ya kwanza timu hizi zilitoka sare ya moja kwa moja. Hivyo mchezo wa leo ni muhimu sana kwakuwa mshindi atapata tiketi ya kucheza fainali.
Macho ya watanzania wapenda soka yatakuwa kwa kijana wao, nahodha wa timu ya taifa, Mbwana Ally Samatta.
Samatta anakuwa mchezaji wa kwanza mtanzania kucheza katika timu iliyopo katika ligi kuu ya uingereza.
Uzi huu ni maalum kwa ajili ya update za mechi hiyo kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Kama upo mbali ya runinga kaa hapa, utapata kila kitu kuhusu mechi hiyo.
Karibuni sana.
Naitwa Six Man.
Sent using
Jamii Forums mobile app