Asubuhi Moja Kigamboni na Bi. Mwajame bint Dossa Aziz

Asubuhi Moja Kigamboni na Bi. Mwajame bint Dossa Aziz

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Akituelekeza namna ya kufika nyumbani kwake Kigamboni leo asubuhi Bi. Mwajame bint Dossa Aziz akamaliza kwa kusema, "Ukifika hapo utaona kibao kimeandikwa "Mwajame Street."

Mpwa wangu Yusuf aliyekuwa ananiendesha akashtuka na kuzungumza na Bi. Mwajame akasema "Mjomba Mtaa una jina lake!"

Hakika hata mimi nilishtuka.

Bi. Mwajame ni mtoto wa Dossa Aziz.

Dossa Aziz ni katika wazalendo 17 waliounda TANU mwaka wa 1954 na kati ya wafadhili wakubwa wanne wa chama hicho: John Rupia, Dossa Aziz na ndugu wawili Abdul na Ally Sykes.

Nimeshtuka kwa sababu juu ya makubwa ambayo baba yake kafanya katika kupigania uhuru wa Tanganyika hajatunukiwa mtaa si nyumbani kwao Gerezani wala popote pale.

Iweje mwanae apewe mtaa?

Yusuf Makamba kapewa mtaa jirani na alipozaliwa Dossa Mtaa wa Mbaruku na Congo na waliotoa mtaa huo kumpa Makamba ni kama vile hawamjui Dossa Aziz wala hawajapata kumsikia.

Wewe nani umtangulie Dossa kupata mtaa?

Dossa Aziz katika siku za mwanzo kabisa za kupigania uhuru alitoa gari yake kumpa Mwalimu Nyerere imsaidie katika kufanikisha majukumu yake kama President wa TANU.

Kasahaulika!

Hana mtaa wala chochote cha kuonyesha kutoka nchini kwake na kutoka chama alichokiunda na kukifadhili. Dossa hakupewa hata mtaa. Mwanae Mwajame kapewa mtaa Kigamboni.

Hakika nilistaajabu sana. Haya mambo yakoje?

Wakati wake Dossa walimpa lakabu wakimwita "The Bank."

Huendi benki ukaambiwa fedha zimekwisha njoo kesho.

Hana mtaa kwao Gerezani.

Nimeshuka kwenye gari na Shariff Yusuf mpwa wangu akanipiga picha kwenye kibao hicho chenye jina la dada yangu Mwajame.

Mwajame bint Dossa ana mtaa Kigamboni. Da Mwajame anasema mtaa ule hakuupata kwa kutumia mgongo wa baba yake.

"Mimi nilipigiwa simu na Mwenyekiti wa Mtaa kuelezwa kuwa jina langu limepewa mtaa ninaokaa kwa kuwa mimi ni mkazi wa zamani kupita wote.

Baada ya kupewa mtaa ndipo niliposikia wakimtaja baba yangu kuwa alikuwa mfadhili wa TANU na rafiki wa Nyerere."

Bi. Mwajame anakumbuka maasi ya Tanganyika Rifles mwaka 1964 na simanzi iliyomfika baba yake wakati huo Dossa akiishi shambani kwake Ruvu.

"Baba kaja nyumbani Mtoni kwa Aziz Ali na mkewe Bi. Nagla anaendesha Land-rover akamweleza bibi kuwa kumetokea maasi ya wanajeshi na Nyerere kapotea hajulikani alipo.

Baba akasema kuwa anamwacha mkewe hapo yeye anakwenda kumtafuta Nyerere.

Kwanza Bi. Nagla akasema yeye hakubali Dossa aende peke yake lazima awe na yeye. Bibi akamuuliza baba, "Dossa utampata wapi Nyerere na vurugu hili?"

Baba akawa anabishana na mama anamwambia, "Nagla utaniponza tukamatwe sote, wanajeshi wanakamata Wahindi na Waarabu." Bi. Nagla alikuwa kachanganya damu.

"Mwishowe baba na mama wote wakaondoka. Siku nzima nyumba nzima ilikuwa na simanzi wakihofia maisha ya Nyerere na ya baba aliyekwenda kumtafuta rafiki yake.

"Usiku baba alirudi nyumbani peke yake hoi kachoka, akamweleza bibi kuwa Nyerere yuko salama."

"Yuko salama wapi?" Bibi anataka kujua.

"Baba hakumwambia yeye kashikilia tu kuwa Nyerere mzima yuko salama.

"Baba alisimamishwa mara mbili na wanajeshi wakati anatoka Mtoni.

"Alisimamishwa makutano ya Pugu Road na Msimbazi karibu na ofisi za mabasi ya DMT yaani Dar-es-Salaam Motor Transport na makutano ya Msimbazi na Kitchwele.

"Kote aliachiwa kupita bila matatizo wale wanajeshi wakisema, Dossa huyo mwacheni apite."

Hakuna ambae hakuwa anajua uhusiano na Dossa Aziz na Nyerere.

Lakini baba anasema aliona magari mengi pembeni ya barabara yametobolewa matairi.

Ilikuwa wazi wanajeshi hawakutaka kuona magari barabarani.

Nyerere wakati wa kupigania uhuru hata kazi ya ualimu hajaacha alikuwa akija nyumbani Mtaa wa Mbaruku na Congo na Abdul na Ally Sykes wakati mwingine akilala pale.

Kama atalala nyumbani chumba chake.kilikuwa cha kaka yangu Ali Aziz na Ali atakwenda kulala kwengine kwani alikuwa mtoto bado yuko shule.

Nilikuja kujua baadae kuwa baba katika fikra zake alikuwa anadhani Nyerere kwa kuwa hayuko Government House atakuwa kenda kujificha Ruvu shambani kwake ambako wakati wa kupigania uhuru walijenga handaki endapo itabidi kujificha.

Nimemuuliza baba mara nyingi wapi Nyerere alijificha wakati wa maasi lakini baba alikataa kuniambia.

Nikimghasi kutaka aniambie akisema, "Mwajame una maswali kama askari."

Mwajame baada ya kumaliza masomo alijiunga na jeshi la polisi.

Muhimu wanahistoria wafanye utafiti kujua hili handaki shambani kwa Dossa liko wapi kwani ni sehemu muhimu ya historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Bi. Mwajame anasema baba yake alipata kumweleza kuwa ile nyumba ya baba yake Ruvu walikuwa wakiitumia wakati mwingine kama sehemu yao moja ya kutafuta faragha TANU inapokuwa na jambo lake lililohitaji kujadiliwa kwa utulivu.

Lakini anasema lile handaki ilikuwa siri kubwa.

Yeye alikuja kulisikia kwa mfanyakazi wao mmoja wa shamba.

Huyu ndiye aliyemfahamisha miaka mingi baadae kuwa katika moja ya mashamba ya Dossa Aziz palijengwa handaki.

Historia ya Nyerere alitoka vipi Government House wakati wa maasi niliyosikia kutoka kwa Kitwana Kondo inatofautiana kidogo na historia aliyoandika Peter Mbwimbo katika kitabu chake, ''Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere,'' (2015).

Bi. Mwajame ana mengi katika udugu na urafiki baina ya baba yake na Nyerere ambae anasema baba yake akipenda kumwita, "Kambarage."

"Nilikwenda kwa baba kumuomba mtaji nifuge kuku."

Baba akaniambia, "Nenda kwa Kambarage." Nilikuwa naogopa lakini yeye akanishikilia niende.

Nilikwenda Msasani.

Foleni ya kuonana na Mwalimu ndefu mpaka naingia kumuona jua limekuchwa. Mwalimu alikuwa kanisahau. Nikamweleza shida yangu.

Mwalimu akataka kujua mahitaji yangu. "Mwalimu nitapokea chochote utakachonipa."

Mwalimu akaweka oda nipewe vifaranga 500 pamoja na chakula na madawa.

Mwalimu alipojua kuwa naendesha scooter akaagiza nipelekwe na "escort" hadi nyumbani.

Baada ya siku mbili vifaranga na kila kitu changu vikaletwa nyumbani Mtoni.

Kuku wangu walipokua nikachukua kuku 20 nikawachinja nikampelekea Mwalimu.

Wasaidizi wa Mwalimu waliponiona walikuwa sasa wananifahamu wananiita Mtoto wa Dossa.

Wakanipeleka kwa Mama Maria. Mama Maria alinishangaa, "Mwajame umekuwa mkubwa kiasi hiki!"

Mwanahistoria mkubwa wa historia ya Tanganyika John Iliffe alipata kusema kuwa historia nyingi ya TANU ipo mikononi mwa watu binafsi.

Mimi nakubaliana na yeye kwani mimi kila ninapopata nafasi ya kuzungumza na wale waliokuwapo nyakati zile za kupigania uhuru hukutana na historia ambayo kamwe sijapata kuisikia popote.

Hasa ninapokutana na watoto wa wapigania uhuru hawa huwa na historia za kusisimua.

Mimi sikujua kuwa ile nyumba aliyotafutiwa Nyerere na TANU Maduka Sita Magomeni, mdogo wake Dossa Ramadhani Aziz yeye alikuwa pale kabla akiendesha duka lake.

Kiasi mtu unapata picha kama vile marafiki wa Nyerere hawakutaka Mwalimu awe popote pale peke yake bila ya wao kuwa na mtu wao jirani yake.

335904245_1002789804033572_3379634127741146721_n.jpg
335610495_949185239420011_4143322468447407316_n.jpg

335378713_883118926107405_5420298323028283869_n.jpg

images-jpeg.1405451

Dossa Aziz
 
Umenikumbusha Nyumbani Tunduru those days kulikuwa na mtaa pale Tunduru mjini unaitwa Kwa Dosa Azizi sijui kama upo bado.
 
Mbona huwa inasemwa mwalimu aliwatosa waliomsaidia.
Kumbe Hadi watoto wao walipewa mtaji wa kuku!!

Kule yalipo majengo ya Avic town karibu na kimbiji Kuna maeneo makubwa Sana ,wenyeji walinambia ni ya Azizi Ali.
Ana unasaba na hawa kina Dosa?
 
Pole yake Kwa kuzidiwa akili,mjini mipango

Halafu siku zote wageni ndiyo huleta maendeleo
 
Mbona huwa inasemwa mwalimu aliwatosa waliomsaidia.
Kumbe Hadi watoto wao walipewa mtaji wa kuku!!

Kule yalipo majengo ya Avic town karibu na kimbiji Kuna maeneo makubwa Sana ,wenyeji walinambia ni ya Azizi Ali.
Ana unasaba na hawa kina Dosa?
Deo...
Aziz Ali ni baba yao.
 
Mbona huwa inasemwa mwalimu aliwatosa waliomsaidia.
Kumbe Hadi watoto wao walipewa mtaji wa kuku!!

Kule yalipo majengo ya Avic town karibu na kimbiji Kuna maeneo makubwa Sana ,wenyeji walinambia ni ya Azizi Ali.
Ana unasaba na hawa kina Dosa?
Deo...
Iko siku niko Mtaa wa Sokoine karibu na train station natupa jicho barabarani namuona Dossa Aziz anaendesha pickup ya njano.

Katika mazungumzo nikamweleza Ally Sykes.

Kumbe Ally Sykes alikuwanazo taarifa akaniambia kuwa Nyerere amemnunilia Dossa gari ile.
 
ile historia tuliyofundishwa shuleni ukweli wake una mashaka sana
 
ASUBUHI MOJA KIGAMBONI NA BI. MWAJAME BINT DOSSA AZIZ

Akituelekeza namna ya kufika nyumbani kwake Kigamboni leo asubuhi Bi. Mwajame bint Dossa Aziz akamaliza kwa kusema, "Ukifika hapo utaona kibao kimeandikwa "Mwajame Street."

Mpwa wangu Yusuf aliyekuwa ananiendesha akashtuka na kuzungumza na Bi. Mwajame akasema "Mjomba Mtaa una jina lake!"

Hakika hata mimi nilishtuka.

Bi. Mwajame ni mtoto wa Dossa Aziz.

Dossa Aziz ni katika wazalendo 17 waliounda TANU mwaka wa 1954 na kati ya wafadhili wakubwa wanne wa chama hicho: John Rupia, Dossa Aziz na ndugu wawili Abdul na Ally Sykes.

Nimeshtuka kwa sababu juu ya makubwa ambayo baba yake kafanya katika kupigania uhuru wa Tanganyika hajatunukiwa mtaa si nyumbani kwao Gerezani wala popote pale.

Iweje mwanae apewe mtaa?

Yusuf Makamba kapewa mtaa jirani na alipozaliwa Dossa Mtaa wa Mbaruku na Congo na waliotoa mtaa huo kumpa Makamba ni kama vile hawamjui Dossa Aziz wala hawajapata kumsikia.

Wewe nani umtangulie Dossa kupata mtaa?

Dossa Aziz katika siku za mwanzo kabisa za kupigania uhuru katoa gari yake kumpa Mwalimu Nyerere imsaidie katika kufanikisha majukumu yake kama President wa TANU.

Kasahauliwa.

Hana mtaa wala chochote cha kuonyesha kutoka nchini kwake na kutoka chama alichokiunda na kukifadhili.

Dossa hakupewa hata mtaa.
Mwanae Mwajame kapewa mtaa Kigamboni.

Hakika nilistaajabu sana.
Haya mambo yakoje?

Wakati wake Dossa walimpa lakabu wakimwita "The Bank."

Huendi benki ukaambiwa fedha zimekwisha njoo kesho.

Hana mtaa kwao Gerezani.

Nimeshuka kwenye gari na Shariff Yusuf mpwa wangu akanipiga picha kwenye kibao hicho chenye jina la dada yangu Mwajame.

Mwajame bint Dossa ana mtaa Kigamboni.

Da Mwajame anasema mtaa ule hakuupata kwa kutumia mgongo wa baba yake.

"Mimi nilipigiwa simu na Mwenyekiti wa Mtaa kuelezwa kuwa jina langu limepewa mtaa ninaokaa kwa kuwa mimi ni mkazi wa zamani kupita wote.

Baada ya kupewa mtaa ndipo niliposikia wakimtaja baba yangu kuwa alikuwa mfadhili wa TANU na rafiki wa Nyerere."

Bi. Mwajame anakumbuka maasi ya Tanganyika Rifles mwaka 1964 na simanzi iliyomfika baba yake.

Wakati huo Dossa akiishi shambani kwake Ruvu.

"Baba kaja nyumbani Mtoni kwa Aziz Ali na mkewe Bi. Nagla anaendesha Land-rover akamweleza bibi kuwa kumetokea maasi ya wanajeshi na Nyerere kapotea hajulikani alipo.

Baba akasema kuwa anamwacha mkewe hapo yeye anakwenda kumtafuta Nyerere.

Kwanza Bi. Nagla akasema yeye hakubali Dossa aende peke yake lazima awe na yeye.

Bibi akamuuliza baba, "Dossa utampata wapi Nyerere na vurugu hili?"

Baba akawa anabishana na mama anamwambia, "Nagla utaniponza tukamatwe sote wanajeshi wanakamata Wahindi na Waarabu."

(Bi. Nagla alikuwa kachanganya damu).

"Mwishowe baba na mama wote wakaondoka.
Siku nzima nyumba nzima ilikuwa na simanzi wakihofia maisha ya Nyerere na ya baba aliyekwenda kumtafuta rafiki yake.

Usiku baba alirudi nyumbani peke yake hoi kachoka akamweleza bibi kuwa Nyerere yuko salama."

"Yuko salama wapi?" Bibi anataka kujua.

"Baba hakumwambia yeye kashikilia tu kuwa Nyerere mzima yuko salama.

Baba alisimamishwa mara mbili na wanajeshi wakati anatoka Mtoni.

Alisimamishwa makutano ya Pugu Road na Msimbazi karibu na ofisi za mabasi ya DMT yaani Dar-es-Salaam Motor Transport na makutano ya Msimbazi na Kitchwele.

Kote aliachiwa kupita bila matatizo wale wanajeshi wakisema, "Dossa huyo mwacheni apite."

Hakuna ambae hakuwa anajua uhusiano na Dossa Aziz na Nyerere.

Lakini baba anasema aliona magari mengi pembeni ya barabara yametobolewa matairi.

Ilikuwa wazi wanajeshi hawakutaka kuona magari barabarani.

Nyerere wakati wa kupigania uhuru hata kazi ya ualimu hajaacha alikuwa akija nyumbani Mtaa wa Mbaruku na Congo na Abdul na Ally Sykes wakati mwingine akilala pale.

Kama atalala nyumbani chumba chake.kilikuwa cha kaka yangu Ali Aziz na Ali atakwenda kulala kwengine kwani alikuwa mtoto bado yuko shule.

Nilikuja kujua baadae kuwa baba katika fikra zake alikuwa anadhani Nyerere kwa kuwa hayuko Government House atakuwa kenda kujificha Ruvu shambani kwake ambako wakati wa kupigania uhuru walijenga handaki endapo itabidi kujificha.

Nimemuuliza baba mara nyingi wapi Nyerere alijificha wakati wa maasi lakini baba alikataa kuniambia.

Nikimghasi kutaka aniambie akisema, "Mwajame una maswali kama askari."

Mwajame baada ya kumaliza masomo alijiunga na jeshi la polisi.

Muhimu wanahistoria wafanye utafiti kujua hili handaki shambani kwa Dossa liko wapi kwani ni sehemu muhimu ya historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Bi. Mwajame anasema baba yake alipata kumweleza kuwa ile nyumba ya baba yake Ruvu walikuwa wakiitumia wakati mwingine kama sehemu yao moja ya kutafuta faragha TANU inapokuwa na jambo lake lililohitaji kujadiliwa kwa utulivu.

Lakini anasema lile handaki ilikuwa siri kubwa.

Yeye alikuja kulisikia kwa mfanyakazi wao mmoja wa shamba.

Huyu ndiye aliyemfahamisha miaka mingi baadae kuwa katika moja ya mashamba ya Dossa Aziz palijengwa handaki.

Historia ya Nyerere alitoka vipi Government House wakati wa maasi niliyosikia kutoka kwa Kitwana Kondo inatofautiana kidogo na historia aliyoandika Peter Mbwimbo katika kitabu chake, ''Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere,'' (2015).

Bi. Mwajame ana mengi katika udugu na urafiki baina ya baba yake na Nyerere ambae anasema baba yake akipenda kumwita, "Kambarage."

"Nilikwenda kwa baba kumuomba mtaji nifuge kuku."

Baba akaniambia, "Nenda kwa Kambarage."
Nilikuwa naogopa lakini yeye akanishikilia niende.

Nilikwenda Msasani.

Foleni ya kuonana na Mwalimu ndefu mpaka naingia kumuona jua limekuchwa.

Mwalimu alikuwa kanisahau.
Nikamweleza shida yangu.

Mwalimu akataka kujua mahitaji yangu.
"Mwalimu nitapokea chochote utakachonipa.

Mwalimu akaweka oda nipewe vifaranga 500 pamoja na chakula na madawa.

Mwalimu alipojua kuwa naendesha scooter akaagiza nipelekwe na "escort" hadi nyumbani.

Baada ya siku mbili vifaranga na kila kitu changu vikaletwa nyumbani Mtoni.

Kuku wangu walipokua nikachukua kuku 20 nikawachinja nikampelekea Mwalimu.

Wasaidizi wa Mwalimu waliponiona walikuwa sasa wananifahamu wananiita Mtoto wa Dossa.

Wakanipeleka kwa Mama Maria.
Mama Maria alinishangaa, "Mwajame umekuwa mkubwa kiasi hiki."

Mwanahistoria mkubwa wa historia ya Tanganyika John Iliffe alipata kusema kuwa historia nyingi ya TANU ipo mikononi mwa watu binafsi.

Mimi nakubaliana na yeye kwani mimi kila ninapopata nafasi ya kuzungumza na wale waliokuwapo nyakati zile za kupigania uhuru hukutana na historia ambayo kamwe sijapata kuisikia popote.

Hasa ninapokutana na watoto wa wapigania uhuru hawa huwa na historia za kusisimua.

Mimi sikujua kuwa ile nyumba aliyotafutiwa Nyerere na TANU Maduka Sita Magomeni, mdogo wake Dossa Ramadhani Aziz yeye alikuwa pale kabla akiendesha duka lake.

Kiasi mtu unapata picha kama vile marafiki wa Nyerere hawakutaka Mwalimu awe popote pale peke yake bila ya wao kuwa na mtu wao jirani yake.

335904245_1002789804033572_3379634127741146721_n.jpg
335610495_949185239420011_4143322468447407316_n.jpg

335378713_883118926107405_5420298323028283869_n.jpg

images-jpeg.1405451

Dossa Aziz
Bwana Mohamed kuna jambo lilinistua kidogo nikajisemeza huku si kumsuta Mohamed Said katika interview ya mtangazaji Jaffary Mponda na bi Mwajama kupitia stesheni ya UTV kipindi chaitwa zumari kuna nukta lilinistua, kwamba bi Mwajama kwanza akimsifia mwalimu kama baba kwake na Rafiki wa baba yake, lakini ziada akisimulia namna mwalimu alivyompa mtaji wa biashara, kwakweli nilistaajabu vipi mwalimu anashambulia kumtelekeza Aziz na mwanae anatusimulia kinyume? Kwakweli "you shall know Truth and The Truth will set you free"
 
Bwana Mohamed kuna jambo lilinistua kidogo nikajisemeza huku si kumsuta Mohamed Said katika interview ya mtangazaji Jaffary Mponda na bi Mwajama kupitia stesheni ya UTV kipindi chaitwa zumari kuna nukta lilinistua, kwamba bi Mwajama kwanza akimsifia mwalimu kama baba kwake na Rafiki wa baba yake, lakini ziada akisimulia namna mwalimu alivyompa mtaji wa biashara, kwakweli nilistaajabu vipi mwalimu anashambulia kumtelekeza Aziz na mwanae anatusimulia kinyume? Kwakweli "you shall know Truth and The Truth will set you free"
Shukuru...
Ikiwa Mwalimu kumpa Mwajame mtaji wa kufuga kuku kunaondoa ukweli wa
historia ya Dossa tuachie hapo.
 
Shukuru...
Ikiwa Mwalimu kumpa Mwajame mtaji wa kufuga kuku kunaondoa ukweli wa
historia ya Dossa tuachie hapo.
Si historia, bali unaeleza ni kwa namna gani madai yako hayakuwa ya kweli hasa mara kadhaa unaposimulia kisa cha medals🥉, lakini hata bi Mwajame ukimsikia katika maelezo yake Anaeleza namna alivyonufaika/alivyopata upendeleo wa kazi benki kuu kwa kule kuwa yeye ni mtoto wa mpigania uhuru
 
Si historia, bali unaeleza ni kwa namna gani madai yako hayakuwa ya kweli hasa mara kadhaa unaposimulia kisa cha medals🥉, lakini hata bi Mwajame ukimsikia katika maelezo yake Anaeleza namna alivyonufaika/alivyopata upendeleo wa kazi benki kuu kwa kule kuwa yeye ni mtoto wa mpigania uhuru
Shukuru...
Hakuna tatizo.
Una uhuru wa kumjua Dossa upendavyo.
 
Si historia, bali unaeleza ni kwa namna gani madai yako hayakuwa ya kweli hasa mara kadhaa unaposimulia kisa cha medals🥉, lakini hata bi Mwajame ukimsikia katika maelezo yake Anaeleza namna alivyonufaika/alivyopata upendeleo wa kazi benki kuu kwa kule kuwa yeye ni mtoto wa mpigania uhuru
Shukuru...
Ikiwa wewe unaona hayo ndiyo malipo ya ihsani ya Dossa kwa mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika sawa hakuna shida.
 
Shukuru...
Ikiwa wewe unaona hayo ndiyo malipo ya ihsani ya Dossa kwa mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika sawa hakuna shida.
Sikweli kwamba naona hivyo, bali nimeweka kumbukumbu sawa kiasi wakati uandikapo kwa hisia usiusahau wema wa mwl walau kwa uchache
 
Sikweli kwamba naona hivyo, bali nimeweka kumbukumbu sawa kiasi wakati uandikapo kwa hisia usiusahau wema wa mwl walau kwa uchache
Shukuru...
Kwani ninapoeleza historia ya kweli na pengine kupunguza sifa ambazo hazimstahiki Mwalimu wewe unahisi mimi ni mtovu wa shukurani?
 
Sikweli kwamba naona hivyo, bali nimeweka kumbukumbu sawa kiasi wakati uandikapo kwa hisia usiusahau wema wa mwl walau kwa uchache
Umeeleza vizuri. Mwajame kaeleza vizuri. Inaonyesha Wazee wetu walifanyiana hisani nyingi ila kwa sababu ya adabu zao wakawa hawatangazi.

Ashakum si matusi ila Mzee MS Inaonyesha ni Mtu ambaye akikusaidia atakusimanga mpaka kaburini. Na kuna wakati unaweza kuona anaeleza habari zako kumbe 'simango'. Tuliozaliwa Pwani tunajua hayo.

Atakwambia mpaka alichokuwa Mwalimu anakula kwa Sykes.
 
Back
Top Bottom