Asubuhi ni muda wa kujadili masuala ya kitaifa/kimataifa kwenye vyombo vya habari (media), sio burudani

Asubuhi ni muda wa kujadili masuala ya kitaifa/kimataifa kwenye vyombo vya habari (media), sio burudani

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Kumekucha tena.

Hili siala limeshajadiliwa sana sehemu mbalimbali. Hivi kwa taifa hili changa tunajivunia nini kuanza kujadili michezo redioni na kwenye televisheni saa 2 asubuhi? Kweli?

Najua wapo watawala wana hofu kuhusu wenye nchi kuwa na uelewa wa mambo yanayowahusu na hatimaye kuchukua hatua stahiki. Najua pia vipo vyombo vya habari vyenye hofu hiyo ya kuonekana kinzani. Najua pia vipo vyombo vya habari vyenye hofu ya kupoteza wateja na matangazo kwa sababu hizo.

Watanzania wanapaswa kujengwa katika namna ambayo itawainua kifikra. Media leo inataka kuheshimiwa wakati 24/7 ni mpira na matangazo ya kamari tu? Leo ukiuliza nusu ya watanzania bajeti iliyopitishwa juzi ni ya thamani gani hawajui.

Ifike pahala media zione tija katika kuwapa maarifa wananchi kuhusu hatima zao kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiteknolojia, na kiburudani pia.
 
Watu wanapenda haya mambo

Mpira simba na Yanga. Ngono. Shock news au break news -ha bar I zilizovunjika - nani amefariki , ajari nani kauliwa n.k

So kinachoendelea ni kuwalisha watu wanachopenda.

Hivyo mtoa mada Kama ambavyo unachambua maharage kabla haujayapika ndivyo unabidi kuchambua habari gani inafaa kuilisha AKILI yako.
 
Kumekucha tena
Hili siala limeshajadiliwa sana sehemu mbalimbali. Hivi kwa taifa hili changa tunajivunia nini kuanza kujadili michezo redioni na kwenye televisheni saa 2 asubuhi? Kweli?

MODS naomba muiweke hii mada kama sticky kama ilivyo kwa mada zingine muhimu. Majadiliano yawepo kwa ajili ya kujenga kizazi chenye kujielewa na chenye utambuzi
Najua wapo watawala wana hofu kuhusu wenye nchi kuwa na uelewa wa mambo yanayowahusu na hatimaye kuchukua hatua stahiki. Najua pia vipo vyombo vya habari vyenye hofu hiyo ya kuonekana kinzani. Najua pia vipo vyombo vya habari vyenye hofu ya kupoteza wateja na matangazo kwa sababu hizo.
Watanzania wanapaswa kujengwa katika namna ambayo itawainua kifikra. Media leo inataka kuheshimiwa wakati 24/7 ni mpira na matangazo ya kamari tu? Leo ukiuliza nusu ya watanzania bajeti iliyopitishwa juzi ni ya thamani gani hawajui
Ifike pahala media zione tija katika kuwapa maarifa wananchi kuhusu hatima zao kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiteknolojia, na kiburudani pia
Kunatakiwa kuwe na media nyingi, kila mtu achague anayotaka.

Anayetaka michezo achague ya michezo, anayetaka siasa achague ya siasa.

Ukiona kuna mapungufu, hata wewe una haki ya kuanzisha media yako.

Mambo mengine unayoona muhimu wewe, wengine wanaona hayana umuhimu hivyo.
 
Power Breakfast /Joto la asubuhi
Sports Arena/Sports Round Up
Mashamsham/Leo tena
The Switch /Planet Bongo
Jahazi /Mgahawani
Amplifaya
Lavidavi / Singeli michano

Yaani ni vururu vururu tu.
Na hapo kwenye mitandao watu wanashinda tiktok kuangalia vibonzo tu. Aisee Taifa linadumazwa sana na hizi media na social media
 
Watu wanapenda haya mambo

Mpira simba na yanga
Ngono
Shock news au break news -ha bar I zilizovunjika - nani amefariki , ajari nani kauliwa n.k

So kinachoendelea ni kuwalisha watu wanachopenda.

Hivyo mtoa mada Kama ambavyo unachambua maharage kabla haujayapika ndivyo unabidi kuchambua habari gani inafaa kuilisha AKILI yako.
Kwa habari ya maslahi ya kitaifa, hakuna namna. Taarifa za kimaendeleo ziwe kama dozi. Utake usitake. Yani kijana anasikioiza michezo redioni akiwa anachokonoa meno na stiki toka china, mtumba toka Taiwan, sandals toka china, saa na simu imported. Redio yenyewe toka Malaysia, Mafuta ya kujipaka toka Kenya. Pakistani hapo watu wako na viwanda barabarani kama wamachinga wanazalisha vitu hatari. Tumebakia kusema wacha tusikilize tunachopenda
 
Power Breakfast /Joto la asubuhi
Sports Arena/Sports Round Up
Mashamsham/Leo tena
The Switch /Planet Bongo
Jahazi /Mgahawani
Amplifaya
Lavidavi / Singeli michano

Yaani ni vururu vururu tu.
Na hapo kwenye mitandao watu wanashinda tiktok kuangalia vibonzo tu. Aisee Taifa linadumazwa sana na hizi media na social media
Umenena mkuu
 
Kwa beki Mwamnyeto akiamka asubuhi unataka ajadili nini yeye? Hujui kama burudani ndio kazi yake na ndio jambo lake la kitaifa?
 
Kunatak8wa kuwe na media nyingi, kila mtu achague anayotaka.

Anayetaka michezo achague ya michezo, anayetaka siasa achague ya siasa.

Ukiona kuna mapungufu, hata wewe una haki ya kuanzisha media yako.
Hivi kwa uncle Sam nako asubuhi na mapema unaweza kuta watu wanazijadili LA Clippers, Lakers na kina LeBron James, Stephen Curry, Kevin Durrant halafu mchana, jioni na usiku hivyo hivyo?
 
Hivi kwa uncle Sam nako asubuhi na mapema unaweza kuta watu wanazijadili LA Clippers, Lakers na kina LeBron James, Stephen Curry, Kevin Durrant halafu mchana, jioni na usiku hivyo hivyo?
Kuna channel zinazungumza mambo hayo masaa 24 siku 7 za kila wiki.

Na pia kuna channel zinazungumza uchumi hivyo hivyo.
 
Kunatakiwa kuwe na media nyingi, kila mtu achague anayotaka.

Anayetaka michezo achague ya michezo, anayetaka siasa achague ya siasa.

Ukiona kuna mapungufu, hata wewe una haki ya kuanzisha media yako.

Mambo mengine unayoona muhinu wewe, wengine wanaona hayana umuhimu hivyo.
Ni kweli kabisa. Lakini kwa hali ya sasa inahitaji juhudi za ziada kuhakikisha kwanza huu mtazamo wa sasa unaondoka. Kwamba hata wanaoanzisha media wanaona soko lipo katika burudani. regulations ziwepo kwanza. Muda wa burudani unaweza kuwa kuanzia saa 9 alasiri hadi saa 1 usiku. Muda mwingne ni wa kuwajenga wananchi kifikra.
Pengine pia sina uwezo wa kuanzisha media. natoa mawazo yangu kama hivi ili wenye nguvu wakiona fursa waitumie.
 
Kuna channel zinazungumza mambo hayo masaa 24 siku 7 za kila wiki.

Na pia kuna channel zinazungumza uchumi hivyo hivyo.
Sisi itakuwa bado tuko kwenye hybrid labda ndio maana baadhi ya watu wanachanganywa, hatujafikia level ya kuwa na redio au TV channels za hard news pekee zilizojitofautisha na zile za burudani na anasa kama yaliyo magazeti.
 
Kumekucha tena.

Hili siala limeshajadiliwa sana sehemu mbalimbali. Hivi kwa taifa hili changa tunajivunia nini kuanza kujadili michezo redioni na kwenye televisheni saa 2 asubuhi? Kweli?

Najua wapo watawala wana hofu kuhusu wenye nchi kuwa na uelewa wa mambo yanayowahusu na hatimaye kuchukua hatua stahiki. Najua pia vipo vyombo vya habari vyenye hofu hiyo ya kuonekana kinzani. Najua pia vipo vyombo vya habari vyenye hofu ya kupoteza wateja na matangazo kwa sababu hizo.

Watanzania wanapaswa kujengwa katika namna ambayo itawainua kifikra. Media leo inataka kuheshimiwa wakati 24/7 ni mpira na matangazo ya kamari tu? Leo ukiuliza nusu ya watanzania bajeti iliyopitishwa juzi ni ya thamani gani hawajui.

Ifike pahala media zione tija katika kuwapa maarifa wananchi kuhusu hatima zao kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiteknolojia, na kiburudani pia.
Umeeleza vyema sana. Kwakweli hii imedumaza akili za Watanzania.
 
Ni kweli kabisa. Lakini kwa hali ya sasa inahitaji juhudi za ziada kuhakikisha kwanza huu mtazamo wa sasa unaondoka. Kwamba hata wanaoanzisha media wanaona soko lipo katika burudani. regulations ziwepo kwanza. Muda wa burudani unaweza kuwa kuanzia saa 9 alasiri hadi saa 1 usiku. Muda mwingne ni wa kuwajenga wananchi kifikra.
Pengine pia sina uwezo wa kuanzisha media. natoa mawazo yangu kama hivi ili wenye nguvu wakiona fursa waitumie.
Unataka kufanya social engineering jamii iwe unavyotaka wewe, wakati jamii yenyewe kwa kiasi kikubwa haitaki kuwa hivyo.

Unaliangalia tatizo kutoka upande mbaya, unaanzia juu kuja chini badala ya kuanzia chini kwenda juu.

Watu wengi wakipata elimu na kuelewa vipaumbele ni vipi, wafanyabiashara wenyewe watabadili priority kwenda na market demand.

Sasa hivi market inataka kusikiliza habari za Diamond na mpira, kwa sababu hapo ndipo utashi wa watu ulipo.

Ukiwalaumu wafanyabiashara kwa kuwapa watu wanachotaka unakuwa hujawatendea haki hao wafanyabiashara wala hao watu.
 
Kwani hauna Choice, dunia ya leo ni Information on demand kama haujui wapi pa kupata information unayohitaji basi ni huenda Bwana Robert alimaanisha wewe

In Abundance of Water a Fool is Thirsty.....; Angalia hili jambo kwa perspective nyingine people need burudani na sehemu ya ku vent their problems huenda hio michezo inasaidia sana watu kupunguza stress
 
Back
Top Bottom