ATCL sasa kutumia Masaa Matatu kutoka Dar hadi Afrika Kusini, ni baada ya kurejesha safari zake

ATCL sasa kutumia Masaa Matatu kutoka Dar hadi Afrika Kusini, ni baada ya kurejesha safari zake

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
Shirika la Ndege nchini ATCL, limetangaza kurejesha safari za ndege zake kwenda nchini Afrika ya Kusini baada ya kusimama kwa muda

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa safari hiyo Leo Novemba 30, Waziri wa Uchukuzi Professa Makame Mbarawa amesema “kuimarika kwa diplomasia ya uchumi umerahisisha kurejesha kibali cha ATCL kwenda South Africa ikiwa ni hatua muhimu inayolenga kukuza biashara na ushirikiano kwa mataifa mengine”

Prof.Mbarawa ameeleza kuwa jitihada za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji inakuwa bora na inaongezeka ili kusaidia shughuli hizo na kuchangia kukuza uchumi wa taifa letu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Mhandisi Peter Ulanga amemshukuru Rais Samia kwa kumuamini na kumteua. Huku akisisitiza kilio cha watanzania wengi wataohitaji kwenda Afrika ya Kusini na kutoka Afrika ya Kusini kuja nchini sasa kimepata dawa.

Amesema sasa ndege ya ATCL itakuwa inatumia Miasaa matatu kutoka Dar Es Salaam Hadi Afrika Kusini. Amesema safari zitakuwa mara tano kwa yaani ndege ipo wiki nzima isipokuwa Jumanne na Alhamis tu.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa “kurejeshwa kwa safari hizi itakuwa nafasi ya kuimarisha biashara ya mizigo barani Afrika lakini pia kuboresha huduma kwa abiria wake” amesema Mhandisi Ulanga
 
Hiyo Route inalipa sana sijui kwa nini waliiacha ikachukuliwa.....
Wao kama wenyenyeji wakiingia na Business strategies nzuri, muhimu wasibadili ratiba/muda wa safari mara kwa mara ili tuwapige chini AirLink
Binafsi naipenda sana ATC hasa safari za nje, ni chaguo #1; Ndege ya nyumbani ukiwa na changamoto yoyote mnaongea kinyumbani.....
 
Ndege za shirika la air Tanzania zimeanza safari za kwenda OR Tambo International airport, Johannesburg, RSA, mizigo mpaka 69kgs kwa abiria wa daraja la economy.

NB: Tukitua Lagos na Accra basi tumeshaliteka soko la Afrika nzima.

**Tuwe wazalendo.
 
Ndege za shirika la air Tanzania zimeanza safari za kwenda OR Tambo International airport, Johannesburg, RSA, mizigo mpaka 69kgs kwa abiria wa daraja la economy.

NB: Tukitua Lagos na Accra basi tumeshaliteka soko la Afrika nzima.

**Tuwe wazalendo.
Kwa hizo nauli walizoanza nazo, wanaweza kujiona kama wana bahati mbaya, maana watu wanaweza kuendelea kupanda KQ licha ya huo mzunguko wao.

Ova
 
Lots of Bs, mnatakiwa mtueleze cost comparison, Service delivery, space, comfort, na hizo nyingine...

Kuish SA hakukufanyi frequent traveller...

Can we learn?
 
Shirika la Ndege nchini ATCL, limetangaza kurejesha safari za ndege zake kwenda nchini Afrika ya Kusini baada ya kusimama kwa muda

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa safari hiyo Leo Novemba 30, Waziri wa Uchukuzi Professa Makame Mbarawa amesema “kuimarika kwa diplomasia ya uchumi umerahisisha kurejesha kibali cha ATCL kwenda South Africa ikiwa ni hatua muhimu inayolenga kukuza biashara na ushirikiano kwa mataifa mengine”

Prof.Mbarawa ameeleza kuwa jitihada za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji inakuwa bora na inaongezeka ili kusaidia shughuli hizo na kuchangia kukuza uchumi wa taifa letu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Mhandisi Peter Ulanga amemshukuru Rais Samia kwa kumuamini na kumteua. Huku akisisitiza kilio cha watanzania wengi wataohitaji kwenda Afrika ya Kusini na kutoka Afrika ya Kusini kuja nchini sasa kimepata dawa.

Amesema sasa ndege ya ATCL itakuwa inatumia Miasaa matatu kutoka Dar Es Salaam Hadi Afrika Kusini. Amesema safari zitakuwa mara tano kwa yaani ndege ipo wiki nzima isipokuwa Jumanne na Alhamis tu.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa “kurejeshwa kwa safari hizi itakuwa nafasi ya kuimarisha biashara ya mizigo barani Afrika lakini pia kuboresha huduma kwa abiria wake” amesema Mhandisi Ulanga
Haisemwi 'masaa matatu' bali ni saa tatu'
 
Jambo zuri. Airlink South Africa ni ghali sana na wanakupa kilo 20 tu. Angalau sasa tutakuja na ndege yetu. Wale jamaa wa AIRlink mlionisumbua baada ya kuwa na kilo zaidi ya 20 kwaherini sasa hamtaniona tena na ndege yenu.
 
Yule Mzungu mkamata ndege ameshaondoka Joburg? Asije akaondkka na ndege yenu


🤣🤣🤣
Kumbe ndiye ambae walimkimbia ??!
Duuuh 🙆‍♂️🤦‍♀️ jamani nyie ! Kazi kweli kweli .
Umenikumbusha enzi zile aisee!
 
Kwa hizo nauli walizoanza nazo, wanaweza kujiona kama wana bahati mbaya, maana watu wanaweza kuendelea kupanda KQ licha ya huo mzunguko wao.

Ova


KQ na Air Malawi.
Air Malawi wameingia ushirika na Ethiopian Airline siku hizi.

Sema route hizo zinapoteza muda mwingi wakati wa safari masaa mengi kusubiri.
Hiyo Air Malawi yenyewe mkitoka SA pale Chileka Airport mtapoteza masaa chungu nzima kusubiri ndege itoke Lilongwe jioni mwende Bongo na kufika usiku.
 
Wekeni nauli rafiki sasa kama Malawi Air wana bei nzuri sana hao jamaa maana ninyi hamchelewi kuweka nauli ya Daslm kwenda Amsterdam kumbe safari ni ya Oliver Tambo tu hapo angalieni washindani wenu Rwanda, ET na Malawi.
Baggage allowance 69kgs tofauti na hao Malawian 46kgs. Nauli ATC imezidi kama 100USD kwa Malawian.
 
Baggage allowance 69kgs tofauti na hao Malawian 46kgs. Nauli ATC imezidi kama 100USD kwa Malawian.
OK hiyo sio mbaya ila waangalie kidogo maana direct flights zina gharama kidogo hata hao SA ndio balaa zaidi wanaanza January hizo 46 Kg kwa wabeba mizigo midogo midogo ipo vizuri sana hata kwa car accessories..
 
Sijui huko watatoa chakula cha kueleweka au ndio zile Korosho zao za chumvi na vijuisi vya Azam ??!
Yaani Korosho zikishawekwa chumvi siwezi kula hata kidogo 😌🤦‍♀️
Mungu kaweka radha ya asili Kwanini uweke chumvi ??
Kwanini zikaangwe ??

ni swą na kula mahindi ya kuchoma kwa chumvi au Maji ya safi kwa ndimu.
Yaani naonaga ni ujinga wa kuzidi .
 
Wenzao wa Malawi unapewa chakula kizuri tu si haba.
Na kutoka Malawi kwenda SA msosi pia.
Lakini ATCl ni Korosho na Azam kadogo Basi.
 
Shirika la Ndege nchini ATCL, limetangaza kurejesha safari za ndege zake kwenda nchini Afrika ya Kusini baada ya kusimama kwa muda

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa safari hiyo Leo Novemba 30, Waziri wa Uchukuzi Professa Makame Mbarawa amesema “kuimarika kwa diplomasia ya uchumi umerahisisha kurejesha kibali cha ATCL kwenda South Africa ikiwa ni hatua muhimu inayolenga kukuza biashara na ushirikiano kwa mataifa mengine”

Prof.Mbarawa ameeleza kuwa jitihada za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha miundombinu ya usafiri na usafirishaji inakuwa bora na inaongezeka ili kusaidia shughuli hizo na kuchangia kukuza uchumi wa taifa letu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Mhandisi Peter Ulanga amemshukuru Rais Samia kwa kumuamini na kumteua. Huku akisisitiza kilio cha watanzania wengi wataohitaji kwenda Afrika ya Kusini na kutoka Afrika ya Kusini kuja nchini sasa kimepata dawa.

Amesema sasa ndege ya ATCL itakuwa inatumia Miasaa matatu kutoka Dar Es Salaam Hadi Afrika Kusini. Amesema safari zitakuwa mara tano kwa yaani ndege ipo wiki nzima isipokuwa Jumanne na Alhamis tu.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa “kurejeshwa kwa safari hizi itakuwa nafasi ya kuimarisha biashara ya mizigo barani Afrika lakini pia kuboresha huduma kwa abiria wake” amesema Mhandisi Ulanga
Kama ccm inadaiwa wajiweke tayari kupaki huko. Maana sasa watakamata mpaka abiria kufidia madeni
 
Back
Top Bottom