Athari Tatu za Kuondoka kwa Lewis Hamilton Kutoka Mercedes

Athari Tatu za Kuondoka kwa Lewis Hamilton Kutoka Mercedes

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Mercedes Benz ilimpa Lewis dola milioni 100 kwa miaka miwili na akakataa offa yao. Mercedes Benz, ikagoma katukatu kumpa Sir Lewis Hamilton nafasi ya ubalozi. BONGE LA MISTAKE!
1737799299574.jpg


Ferrari haikumpa dola milioni 100, lakini iliwekeza dola milioni 446 kwa Sir Lewis Hamilton na taasisi zake za kijamii, kama vile mradi wa Mission44 & CRUCIALLY huku pia wakimpa nafasi ya ubalozi.
1737799299574.jpg


Baada ya Sir Lewis Hamilton kusainiwa, hisa ya Ferrari iliongezeka kwa 10% ambayo iliongeza dola zaidi ya bilioni 10 kwenye soko la Ferrari. Ukisikia kupishana na gari la mshahara ndio huku, Mercedes Benz mmekula za uso.
 
Mercedes Benz ilimpa Lewis dola milioni 100 kwa miaka miwili na akakataa offa yao. Mercedes Benz, ikagoma katukatu kumpa Sir Lewis Hamilton nafasi ya ubalozi. BONGE LA MISTAKE!
View attachment 3213553

Ferrari haikumpa dola milioni 100, lakini iliwekeza dola milioni 446 kwa Sir Lewis Hamilton na taasisi zake za kijamii, kama vile mradi wa Mission44 & CRUCIALLY huku pia wakimpa nafasi ya ubalozi.
View attachment 3213553

Baada ya Sir Lewis Hamilton kusainiwa, hisa ya Ferrari iliongezeka kwa 10% ambayo iliongeza dola zaidi ya bilioni 10 kwenye soko la Ferrari. Ukisikia kupishana na gari la mshahara ndio huku, Mercedes Benz mmekula za uso.
Daaah kweli kila mada na watu wake.....
Ngoja waje wenye mada yao.. Maana Sijaelewa kitu...


Ni Hayo Tu!!
 
Mercedes Benz hawana jipya saiv na huyo Hamilton ni suala la muda tu atapotea.

Red Bull all the way ♦️♦️♦️
 
yaani umesema ferrari wamewekeza kwa jamaa dola milllion 446 alafu baada ya kusaini hisa za ferrari zikapanda thamani hadi kufikia dola billion 10.! mbona kama jamaa ndio kawafaidisha parefu zaidi ya alichopewa yeye..au mtoa mada ndio umekosea kuandika hizo tarakimu za dola
 
Habari za kuondoka kwa Lewis Hamilton kutoka Mercedes zimetikisa ulimwengu wa Formula One. Baada ya miaka 11 ya ushirikiano wenye mafanikio makubwa, ambapo wametwaa mataji sita ya ubingwa wa dunia, pande hizi mbili zinatengana rasmi.
1737799299574.jpg


Ingawa ni changamoto mpya kwa pande zote mbili, kuondoka kwa Hamilton kutaacha athari tatu muhimu kwa Mercedes na ushiriki wao katika mbio za baadaye za Formula One.

Athari ya Kwanza: Kuporomoka kwa Umaarufu na Uuzaji wa bidhaa zake.
lewis-hamilton-mercedes.jpg


Hamilton ni miongoni mwa wanariadha maarufu zaidi duniani. Uwepo wake katika timu ya Mercedes umevutia mashabiki na wapenzi wengi, na kuongeza thamani ya kibiashara kwa kampuni hiyo. Kuondoka kwake kunaweza kusababisha kuporomoka kwa umaarufu wa timu hiyo, na kupunguza maslahi ya mashabiki na wawekezaji. Hii inaweza kuwa pigo kubwa kwa mapato ya Mercedes kutoka kwa uuzaji wa bidhaa na udhamini.

Athari ya Pili: Uhitaji wa Kupata Mbadala Anayefaa.
images (86).jpeg


Kupata mbadala anayefaa kwa Hamilton sio kazi rahisi. Hamilton ni mmoja wa madereva bora zaidi katika historia ya F1 na duniani. Mbadala wake atahitaji kuwa na uwezo wa kuendana na viwango vya juu vya timu hiyo, na pia kuvutia mashabiki na wawekezaji. Kazi ya kutafuta mbadala anayefaa itakuwa changamoto kubwa kwa Mercedes.
images (85).jpeg


Lewis Hamilton pamoja na George Russell walitengeneza timu bora sana ya Mercedes-AMG Petronas na hii binafsi Mercedes-AMG Petronas ndo timu yangu bora ya muda wote ndani ya Formula One. Mercedes wanaumiza kichwa ni nani ataunda timu pamoja na George Russell.

Athari ya Tatu: Mabadiliko ya Mwelekeo pamoja na falsafa ya Timu.
images (87).jpeg


Kuondoka kwa Hamilton kunaweza pia kusababisha mabadiliko ya mwelekeo pamoja na falsafa ya timu. Mercedes inaweza kuamua kubadili mbinu zao za uendeshaji, huku wakizingatia zaidi maendeleo ya teknolojia na ubunifu. Hii inaweza kuwa fursa kwa timu hiyo kujitengenezea utambulisho mpya na kuvutia kizazi kipya cha mashabiki.
lewis-hamilton-mercedes.jpg


Jambo muhimu ni kuwa Mercedes ni timu yenye historia ndefu ya mafanikio. Wameonyesha uwezo wao wa kukabiliana na changamoto na kubaki kuwa miongoni mwa timu bora zaidi katika F1. Ingawa kuondoka kwa Hamilton ni pigo kubwa, Mercedes ina uwezo wa kuendelea kushinda na kubaki kuwa miongoni mwa timu zinazoheshimika zaidi katika mbio za magari duniani.
images (85).jpeg


Kwa sasa wanapaswa kujiandaa kisaikolojia kwani washindani wao kama, Haas, AlphaTauri, McLaren, Alfa Romeo, Alpine, Aston Martin wameshapata nafasi ya kuona ushindi upo mara baada ya msumbufu kuondoka.

Kila lenye kheri Mercedes na mafanikio mema kwa timu Mercedes-AMG Petronas.
 
yaani umesema ferrari wamewekeza kwa jamaa dola milllion 446 alafu baada ya kusaini hisa za ferrari zikapanda thamani hadi kufikia dola billion 10.! mbona kama jamaa ndio kawafaidisha parefu zaidi ya alichopewa yeye..au mtoa mada ndio umekosea kuandika hizo tarakimu za dola
Ulichokiandika ndiyo hasa lengo la uzi.Haujatofautiana naye.
 
Tunasubiri tuone comb yake na Charles itakuwa vp, kitambo sana Ferrari hatujaonja ubingwa, ninatamani iwe ndio mwanzo wa kuchukua ubingwa.
Haiwezekani kila msimu ni bahati mbaya tu, ama team imepambana, ni wakati sasa wa kuondoka na Ubingwa wenyewe.
 
Watu na vipaji vyao Dunia nzima ni wewe tu check jamaa anaona sehemu Gani!? Kuna noti ndo anaenda
 
yaani umesema ferrari wamewekeza kwa jamaa dola milllion 446 alafu baada ya kusaini hisa za ferrari zikapanda thamani hadi kufikia dola billion 10.! mbona kama jamaa ndio kawafaidisha parefu zaidi ya alichopewa yeye..au mtoa mada ndio umekosea kuandika hizo tarakimu za dola
Hili ndio LENGO LA UZI.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Back
Top Bottom