Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
Baadhi ya Wachungaji wa Makanisa kutoka katika Kaunti ya Taita Taveta wamelalamika maisha yao kuzorota baada ya kukosa sadaka na fungu la 10 kutoka kwa Waumuni kufuatia kufungwa kwa Makanisa ikiwa ni njia ya kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo
Mmoja wa Wachungaji hao amsema, “Hili janga la #Corona limetuathiri sana kwa nyumba ya Mungu kufungwa. Sisi ni Wachungaji tunategemea sadaka na fungu la 10. Kuna watu wanaficha kwamba hawategemei sadaka. Ila mimi nasema ukweli nimeitwa na Mungu na ninachotegemea ni sadaka na fungu la 10 kutoka kwa Waumini”
Huku Wachungaji hao wakiwa wameomba msaada wa chakula kutoka kwa Wahisani, Mchungaji mmoja amasema kuwa “Kwa kipindi hiki maisha yamekuwa magumu kweli, kuna Wachungaji hatujalima hatujafanya chochote tulitegemeq sadaka na fungu la 10”
Wachungaji hao wanasema #COVID19 imetikisa imani ya Wakristo kwa kiasi kikubwa na kuomba Serikali kufungua Makanisa kwa maana maombi ya madhabauni yana nguvu kuliko maombi ya nyumbani
Kutokana na hilo Gavana wa Taita Taveta, Granton Samboja amesikia kilio chao na kuwapatia Wachungaji hao chakula akitoa fedha zake mwenyewe mfukoni tukio ambalo limepigwa vikali na Wadau mbalimbali wakihoji, itakuwaje kwa wananchi waliopo vijijini ambao nao hawana chakula?
Mmoja wa Wachungaji hao amsema, “Hili janga la #Corona limetuathiri sana kwa nyumba ya Mungu kufungwa. Sisi ni Wachungaji tunategemea sadaka na fungu la 10. Kuna watu wanaficha kwamba hawategemei sadaka. Ila mimi nasema ukweli nimeitwa na Mungu na ninachotegemea ni sadaka na fungu la 10 kutoka kwa Waumini”
Huku Wachungaji hao wakiwa wameomba msaada wa chakula kutoka kwa Wahisani, Mchungaji mmoja amasema kuwa “Kwa kipindi hiki maisha yamekuwa magumu kweli, kuna Wachungaji hatujalima hatujafanya chochote tulitegemeq sadaka na fungu la 10”
Wachungaji hao wanasema #COVID19 imetikisa imani ya Wakristo kwa kiasi kikubwa na kuomba Serikali kufungua Makanisa kwa maana maombi ya madhabauni yana nguvu kuliko maombi ya nyumbani
Kutokana na hilo Gavana wa Taita Taveta, Granton Samboja amesikia kilio chao na kuwapatia Wachungaji hao chakula akitoa fedha zake mwenyewe mfukoni tukio ambalo limepigwa vikali na Wadau mbalimbali wakihoji, itakuwaje kwa wananchi waliopo vijijini ambao nao hawana chakula?