ibanezafrica
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,261
- 6,553
Watanzania tubadilike, Kocha hajafungwa mchezo wowote katika ligi anakimbilia michezo 50 sasa, leo hii linatokea kundi la watu wakijiaminisha kabisa ati kocha hafai!
Majuzi hapa kocha wa Azam naye alikaribia kupindua meza kwa kucheza vizuri bahati mbaya refa naye aliwaangusha lakini walishinda mchezo, kwa bahati mbaya anakuja kupoteza mchezo mmoja tu katika ligi basi ameonekana hafai! Ihefu anasua sua na leo tena kapigwa na Singida, lakini kwao husikii presha ya mwalimu kufukuzwa!
Watanzania tujirekebishe tusiwe wakurupukaji, kuna mahali hatuko sawa. Tuwe na subira na tujifunze na tujijue tupo ngazi gani ya kiwango cha soka duniani. Tujiulize wachezaji wetu ni wa viwango vya thamani ipi?
Majuzi tumesikia tetesi za Kocha Svern kishingo kutajwa kuwa anaweza kurudi Simba! Unajiuliza kwanini aliondoshwa? Mgunda huyo ameonyesha rekodi nzuri toka ajiunge hapo Simba lakini leo anaonekana hafai!
Tunajielewa kweli? Hata Pep akitua hapa Tanzania naamini atafurushwa tu.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Majuzi hapa kocha wa Azam naye alikaribia kupindua meza kwa kucheza vizuri bahati mbaya refa naye aliwaangusha lakini walishinda mchezo, kwa bahati mbaya anakuja kupoteza mchezo mmoja tu katika ligi basi ameonekana hafai! Ihefu anasua sua na leo tena kapigwa na Singida, lakini kwao husikii presha ya mwalimu kufukuzwa!
Watanzania tujirekebishe tusiwe wakurupukaji, kuna mahali hatuko sawa. Tuwe na subira na tujifunze na tujijue tupo ngazi gani ya kiwango cha soka duniani. Tujiulize wachezaji wetu ni wa viwango vya thamani ipi?
Majuzi tumesikia tetesi za Kocha Svern kishingo kutajwa kuwa anaweza kurudi Simba! Unajiuliza kwanini aliondoshwa? Mgunda huyo ameonyesha rekodi nzuri toka ajiunge hapo Simba lakini leo anaonekana hafai!
Tunajielewa kweli? Hata Pep akitua hapa Tanzania naamini atafurushwa tu.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app