Atiq Ahmed: Aliyekuwa mwanasiasa wa India na kakake wapigwa risasi wakiwa mubashara kwenye Runinga

Atiq Ahmed: Aliyekuwa mwanasiasa wa India na kakake wapigwa risasi wakiwa mubashara kwenye Runinga

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
RISASI.JPG

Mwanasiasa wa zamani wa India aliyepatikana na hatia ya utekaji nyara ameuawa kwa kupigwa risasi moja kwa moja kwenye TV pamoja na kaka yake.

Atiq Ahmed, ambaye alikuwa chini ya usalama wa maafisa wa polisi, alikuwa akizungumza na waandishi wa habari wakati bunduki ilipotolewa karibu na kichwa chake huko Prayagraj, eneo pia linalojulikana kama Allahabad.

Baada ya risasi hizo kufyatuliwa Jumamosi usiku, wanaume watatu waliokuwa wakijifanya wanahabari walijisalimisha haraka na kuwekwa chini ya ulinzi.

Mtoto wa kijana wa Ahmed aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi siku zilizopita.

Makumi ya kesi, ikiwa ni pamoja na utekaji nyara, mauaji na unyang'anyi, zilisajiliwa dhidi ya Atiq Ahmed katika kipindi cha miongo miwili iliyopita. Mahakama ya eneo hilo ilimhukumu yeye na wengine wawili kifungo cha maisha Machi mwaka huu katika kesi ya utekaji nyara.

Ahmed alikuwa amedai hapo awali kulikuwa na tishio kwa maisha yake kutoka kwa polisi.

Video ilionyesha Ahmed na kaka yake, Ashraf, wote wakiwa na pingu, wakizungumza na waandishi wa habari wakiwa njiani kwenda kuchunguzwa afya zao hospitalini sekunde chache kabla ya wote wawili kupigwa risasi.

Katika video hiyo, iliyosambazwa sana kwenye mitandao ya kijamii na vituo vya televisheni, Ahmed anaulizwa ikiwa alihudhuria mazishi ya mwanawe.

Maneno yake ya mwisho kwa kamera ni: "Hawakutuchukua, kwa hivyo hatukuenda."

Washukiwa watatu wa uhalifu walikuwa wamefika eneo hilo kwa pikipiki, polisi walisema. Polisi na mwandishi wa habari pia walijeruhiwa katika eneo la tukio.

Kufuatia tukio la Jumamosi usiku, Waziri Mkuu Yogi Adityanath aliamuru uchunguzi wa mahakama kuhusu mauaji hayo na kupiga marufuku mikusanyiko mikubwa katika wilaya za jimbo la Uttar Pradesh ili kuhakikisha amani.

Wataalamu wameibua maswali kuhusu jinsi mtu anaweza kuuawa mbele ya vyombo vya habari na polisi. Mwandishi wa BBC Hindu Anant Zanane aliripoti kutoka Prayagraj kwamba jiji hilo lillikuwalimewekwa katika hali kutotoka nje.
 
Bila shaka hao wauaji watakuwa ni ndugu au wanafamilia wa hao ambao walitekwa na kuuawa na huyo aliyekuwa kiongozi ambaye sasa alikuwa jela.

Kuna wakati mwanadamu kutokana na kupoteza wapendwa wake hufikia hali ya kuona hata maisha yake hayana thamani tena.

Ni kama yule aliyemwua Gadafi. Gadafi akiwa madarakani alimwua kaka yake, yeye akajiunga na wapigaji wengine kuudondosha utawala wa Gadafi. Wote wakakubaliana Gadafi akamatwe na afikishwe mahakamani, lakini yeye aliamua kumtandika risasi. Alishtakiwa, alipohojiwa alikiri kumwua Gadafi. Alipoulizwa kwa nini alifanya hivyo, akasema hakuona sababu ya Gadafi kufikishwa mahakamani kwa sababu yeye Gadafi hakumfikisha Kaka yake mahakamani. Na alipohukumiwa kifo, akasema ana faraja kubwa sana kwa sababu amelipiza kisasi kwa Gadafi dhidi ya mauaji ya Kaka yake.
 
Bila shaka hao wauaji watakuwa ni ndugu au wanafamilia wa hao ambao walitekwa na kuuawa na huyo aliyekuwa kiongozi ambaye sasa alikuwa jela.

Kuna wakati mwanadamu kutokana na kupoteza wapendwa wake hufikia hali ya kuona hata maisha yake hayana thamani tena.

Ni kama yule aliyemwua Gadafi. Gadafi akiwa madarakani alimwua kaka yake, yeye akajiunga na wapigaji wengine kuudondosha utawala wa Gadafi. Wote wakakubaliana Gadafi akamatwe na afikishwe mahakamani, lakini yeye aliamua kumtandika risasi. Alishtakiwa, alipohojiwa alikiri kumwua Gadafi. Alipoulizwa kwa nini alifanya hivyo, akasema hakuona sababu ya Gadafi kufikishwa mahakamani kwa sababu yeye Gadafi hakumfikisha Kaka yake mahakamani. Na alipohukumiwa kifo, akasema ana faraja kubwa sana kwa sababu amelipiza kisasi kwa Gadafi dhidi ya mauaji ya Kaka yake.
Yule jamaa alishtakiwa kumbe..
 
Back
Top Bottom