Atlanta: Mchungaji na Mkewe wakamatwa kwa kuwafungia Walemavu ndani ya nyumba yao

Atlanta: Mchungaji na Mkewe wakamatwa kwa kuwafungia Walemavu ndani ya nyumba yao

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1642746786253.png

Picha: Mchungaji Curtis Keith Bankston

Mchungaji mmoja na mkewe wamekamatwa kwa madai ya kuwafungia walemavu katika eneo la chini la nyumba yao.

Maafisa wa polisi wanasema Curtis Keith Bankston , 55, na mkewe walikuwa wakiendesha kituo cha kuwaangalia walemvu bila kibali , katika eneo la Griffin , karibu na jimbo la Atlanta Georgia. wawili hao walidhibiti fedha za waathiriwa na mara nyengine kuficha matibabu yao.

Maafisa hao walipata walemavu wanane wenye changamoto ya akili walio na umri kati ya 25 na 65 ambao walikuwa mara nyengine wakifungiwa na bwana Bankston na mkewe Sophia Simm Bankston.

Uchunguzi ulibaini wanandoa hao walikuwa wakikodisha nyumba hiyo kwa miezi 14 na kuitumia kama nyumba ya kuwatunza watu hao ambao polisi inasema walikuwa wamefungiwa kinyume na matakwa yao.

Wakati huohuo, maafisa walisema kwamba waligundua kwamba Curtis Bankston alikuwa akitumia nyumba hiyo kwa kisingizo cha kuwa kanisa na kudai kwamba yeye ni mchungaji.

Yeye na mkewe bi Sim Bankston wameshtakiwa kwa kuwafungia watu kinyume na matakwa yao.

Chanzo: BBC Swahili.
 
Mchungaji mmoja na mkewe wamekamatwa kwa madai ya kuwafungia walemavu katika eneo la chini la nyumba yao.

Maafisa wa polisi wanasema kwamba Curtis Keith Bankston , 55, na mkewe walikuwa wakiendesha kituo cha kuwaangalia walemvu bila kibali , katika eneo la Griffin , karibu na jimbo la Atlanta Georgia.

Wachunguzi wanasema kwamba wawili hao walidhibiti fedha za waathiriwa na mara nyengine kuficha matibabu yao.
Madaktari waliitikia wito wa ripoti kwamba kulikuwa na mgonjwa ambaye alikuwa na mshtuko wa moyo tarehe 13 Januari.

Baada ya kubaini mlango uliokuwa ukielekea katika sehemu hiyo ya chini ya nyumba , maafisa wa masuala ya dharura waliarifu polisi , ilisema taarifa ya polisi.

Maafisa walisema kwamba , waliwapata walemavu wanane wenye akili tahira walio na umri kati ya 25 na 65 ambao walikuwa mara nyengine wakifungiwa na bwana Bankston na mkewe Sophia Simm Bankston.

Uchunguzi ulibaini wanandoa hao walikuwa wakikodisha nyumba hiyo kwa miezi 14 na kuitumia kama nyumba ya kuwatunza watu hao ambao polisi inasema walikuwa wamefungiwa kinyume na matakwa yao.

Wakati huohuo, maafisa walisema kwamba waligundua kwamba Curtis Bankston alikuwa akitumia nyumba hiyo kwa kisingizo cha kuwa kanisa na kudai kwamba yeye ni mchungaji.

Yeye na mkewe bi Sim Bankston wameshtakiwa kwa kuwafungia watu kinyume na matakwa yao.

Idara ya huduma za watu walio na umri mkubwa iliitwa na kuwaweka watu hao katika mazingira mazuri ya kuwatunza , ilisema taarifa hiyo.

Maafisa wa polisi wanatafuta haabari kutoka kwa wakazi wengine ambao huenda walikuwa na wapendwa wao katika nyumba hiyo.

Taarifa ya wakili wa Curtis Bankston iliotolewa kwa mshirika wa BBC, CBS ilisema kwamba alikana madai hayo dhidi yake na kudai kwamba zilitokana na habari zisizo za kweli zilizotolewa na polisi .

Taarifa ilidai kwamba kituo hicho hakikukuwa kundi la nyumba za kuwatunza walemavu , na badala yake kanisa ambalo limekuwa likitoa malazi kwa watu wasio na malazi .
 
KUMBE HATA HUKO KUNA WACHUNGAJI WA MCHONGO? Sura yake yenyewe janja janja
 
Maaskari wamejuaje hao walemavu wa akili wamefungiwa kinyume na matakwa yao
Unakuwa na uwezo wa kuamua chochote kuhusu maisha yako mpaka pale itakapothibitishwa huna uwezo huo na pia ikithibitika kuna watakao fanya maamuzi kwa faida yako. Inaelekea yote hayo hayakutendeka.
 
Tukio kama ilo lilishawai kufanywa na yule mangi wa Manzese,ila yeye alikua anawaruhusu asubuhi wanatoka kukusanya noti.
 
Back
Top Bottom