Attention Bodi Ya Mikopo Ya Elimu Ya Juu Kwa Wanafuzi(HESLB)

Hapana, just wishing. Sidhani kama itavunjwa. Nyatega na wenzake hawawezi kuondolewa pale kuna maslahi ya watu wengi sana. So, ndio maana hata sikumuomba Rais afanye lolote, nimemuomba Santa; probably HE can do something about it.
 
sasa mzee hadi Santa akiwa kwenye kundi lao basi ndio tutakuwa tumefikia mwisho
 
Itakuwa ni zawadi kubwa ya Krismasi na mwaka mpya kwa maelfu ya wanafunzi wa elimu ya juu nchini. ! Dear Santa, I have not asked for anything lately but just this time please!!!

Mwanakijiji,

Unaweza kushangaa kwamba tatizo sio board ya mikopo, tatizo ni sisi watanzania. Huko nyuma wizara walikuwa wanashughulikia bado matatizo yalikuwa mengi tu.

Watanzania tusipoacha ubinafsi na fitina nyingi haya matatizo hata siku moja tusitegemee kuyamaliza. Watu wanaona wanaoteseka sio ndugu zao, sio marafiki zao, then why should they bother?

Labda dawa ni kubinafisha hiyo idara ya mikopo, waje Makaburu
kutufundisha kwamba mpende jirani yako kama unavyoipenda nafsi yako. Maana yangu ni kwamba kama watendaji ni hawa Watanzania wenzetu ambao wengine tunawajua, hata ubadilishe kitu gani, bado kutakuwa na matatizo kibao. Tunahitaji radical changes kwenye idara zetu na wala sio kubadili majina au kubadili kiongozi mmoja mmoja.
 
Mtanzania unachosema ni kweli kabisa. Kama kuna kitu kimenifundisha kuhusu ubabe wa serikali ni suala hili. Can you believe wametumia karibu shilingi milioni 30 kuwarudisha nyumbani, halafu kutumia kiasi kingine kama hicho kuwatafutia shule nyumbani na wengine kurudi Urusi? Cha kushangaza ni kuwa wale waliopata nafasi kwenye vyuo vya nyumbani wanalipa karibu kiasi kile kile kama Ukraine na ukiweka gharama za tiketi kurudi (ambayo ilikuwa ni mkopo) wanajikuta wanalipa zaidi kuliko kama wangeachwa Ukraine.

Chokala alipopata nafasi ya kuwatolea uvivu wanafunzi na kuwarudisha nyumbani aliwaambia wazi kuwa "serikali ingewasaidia lakini mmeenda kwenye vyombo vya habari" ndiyo maana serikali ikawatilia ngumu. Hata waliporudi nyumbani watu wa bodi wakawa wanadhihaki "mjanja nani sasa, huyo Mwanakijiji wenu yuko wapi". Prof. Msolla mwenyewe aliamua kuwacheleweshea hata hizo tiketi ili kuwakomoa halafu tiketi zikiwa tayari zimepatikana karibu mwezi mmoja kabla yake wao wakaenda kuwashtukiza wale vijana with a about 48 hours kuondoka.
 
Mwanakijiji,

Wanaoangalia maslahi ya taifa Tanzania ni wachache sana.

Mimi nikiwa TZ kwa likizo ya mwezi mmoja, huwa nakaribia kurusha ngumu zaidi ya mara 10. Course zote za anger management ambazo wazungu wanatufundisha huku Ulaya huwa hazifanyi kazi.

Unajua kuna watu wanakuonyesha ubabe mpaka unabaki kujiuliza kama hao watu wamewahi kuwa na shida hapa duniani?

Wizara wanafikiri wanawakomoa wanafunzi, kwao hiyo milioni ngapi sijui, haina maana, hiyo ni silaha tu ya kumnyanyasa mnyonge. Fahari wawili wapiganapo, ziumiazo ni nyasi, hiyo ilikuwa vita ya Mwanakijiji na serikali, nyasi zimekauka, tuombe mvua ziote tena.

Tunahitaji radical changes, wala hatutakiwa kuanzia mbali, tunatakiwa kuanzia hapa hapa JF. Je sisi tunatoa haki kwa wale
wanaokuja kutaka kutaka haki kwenye himaya zetu?
 
Duh hapo kwa kweli mi naona swala la Elimu ya Juu na mikopo ni la zamani kwelikweli.... Nakumbuka wakati BM-Waziri; Balali- Katibu Mkuu; Mahalu - Mkurugenzi..... Listi kamili hiyo hata ya Maximo haikaribii hapo mahali... Sasa jiulize wale tulitupwa India, Eastern Europe etc mwaka 1993/4, ilikuwa songombingo si mchezo especially wakati wa uchaguzi wa 1995. Point is uozo pale ndani ni jadi yake na wakati wa BM alishindwa kufanya kitu sababu na yeye alishatumia njia ya pale kutengeneza "Mkate wa kila siku" kimagendo, rushwa, undugunaizesheni nk.... Sasa JK lazima aangalie na kujisafisha manake kama ni kidonda, "LILE NI DONDA NDUGU" mwanangu.....

Yetu macho... au ndio maana kiswahili kinagombewa kuwa lugha chuo kikuu ili waseme "hamuhitaji kwenda nje, jilipieni hapahapa nyumbani" watoto na ndugu zao wapi - "huko maulaya mwanangu"
 
Msomaji wa mada hii, naandika mada hii nikirejea maoni ya wachangiaji wenzangu wa mada ya "UDSM ndio chanzo cha Mfubao wa Elimu Tanzania" kama ilivyowasilishwa na Mkamap. Kwa mrejeo wa kujua nini tulijadili, unaweza kupitia kiungo hiki: http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=140258#post140258.Ni kweli kwamba kiwango cha elimu ya juu (huenda na ya kati) Tanzania kinadidimia kila uchao.
1. Chanzo cha kudumaa huku kwa elimu ni nini?
2. Tufanyeje ili tunyanyue?
3. Nafasi yako ni ipi katika kuifanya elimu hii inyanyuke?

Tuendelee na mjadala.
Idimi
 

1) Chanzo cha kudumaa kwa elimu Tanzania ni nyerere.
2) Tukubali kuwa nyerere ndio katufisadi na tuondokane kabisa na mawazo yake mabovu.
3) Mwambie JK anifanye waziri wa elimu, uone mambo.
 

Idimi:

Kuna mambo mengi yanayochangia kudidimiza elimu ya juu. Kwanza ni uwekezaji wa resource za jamii kama vile pesa katika masuala ya elimu. Ingawaje waliomaliza UDSM watasema kuwa UDSM ni moja ya chuo bora Afrika, safari kwa wanafunzi wengi wa kitanzania kufika huko ni ngumu sana. Ukiangalia ni jinsi gani watanzania wanasoma shule za msingi, sekondari na high school utaona matatizo mengi yanaanzia huko. Wanafunzi wengi wako obsessed na kupata grade nzuri lakini ni juhudi ndogo zinachukuliwa na wanafunzi na walimu wao kufanya wahitimu wawe independent thinkers. Na hili tatizo liko kwa nchi nyingi za Kiafrika. Moja ya alama za Taifa kwa nchi huru za kiafrika ilikuwa ni kujenga vyuo vikuu ambavyo vilichukua elite lakini kilichosahaulika ni njia wa-elite hao kufika kwenye vyuo hivyo. Hii ni tofauti na nchi za Asia tiger, nchi hizi zina mitaala ya nguvu kwa shule za chini kama msingi. Hivyo resources za elimu ni lazima zitumike katika ngazi zote elimu.

Kitu kingine ambacho ningependa kuchangia ni kuwa ni lazima UDSM ikubali ushindani ili kutoa huduma kwa watanzania. Serikali au jamii kwa ujumla ni lazima ianzishe chuo kingine chenye nguvu na kutumia resource za nchi kama vile UDSM. Waliopitia UDSM wanaweza kulipinga hilo lakini nina sababu zifuatazo. UK isingeendele kielimu bila ya kuwepo vyuo vikubwa viwili Cambridge na Exford ambavyo kwa namna moja vinashindana. Na vile vile Yale, MIT, Harvard vina ushindani ambao unasaidia maendeleo ya kielimu na jamii nchini Marekani na Dunia. Monopoly ya UDSM haisaidii nchi katika fani zote.

Vilevile tenure za walimu katika nafasi za uongozi ziwe na muda wake. Watu wasikae katika nafasi za umakamu kwa zaidi ya miaka 6. Na nafasi nyingine kama mkuu wa idara au faculty au vice chancellor zitolewa kwa watu wote duniani na sio walimu waliohitimu katika vyuo hivyo peke yao.

Kwa leo ni hayo tu.
 
Habari nilizozipata ni kuwa wanafunzi wa KItanzania wanaomaliza masomo yao nchini China mwezi wa July mwaka huu, waliomba mkopo kutoka Elimu ya Juu ili kusafirisha mizigo yao - mnajua tena wanaosoma huko hukaa kwa muda mrefu na huwa na vitu vingi ambavyo hutaka kuvichukua kuja kuwasaidia kuanzia maisha Bongo. Mungu si Athumani maombi yao yakakubaliwa lakini ikawa ni neema kwa wengine na simanzi kwa wengine kwani WTZ wanaotoka Bara ndio waliopewa huo mkopo na wale wa Visiwani wamepigwa na chini. Na ninaongelea WTZ wenye vigezo vimoja kuwa wote walipata nafasi hizo kwa kupitia Elimu ya Juu na sio Wizara ya AFya Bara au Visiwani- kilichowatafautisha ni asili tu hawa wanatoka Bara na wengine Visiwani, tafadhali musinitake kuthibitisha habari hizi ni vigumu ila anayeweza kufatilia huko nyumbani afatilie.

Jee hapo hakuna dalli za ubaguzi na malalamiko haya Wazanzibari wanayasemea sana kwani hapo mwanzo Elimu ya Juu haikuwa katika yale mambo 11 yalokubaliwa katika Muungano iliingizwa tu kinyemela kama yalivyoingizwa Wizara ya Mambo ya nchi za Nje na/ mahusiano ya Kimataifa au Fedha.

Sasa hivi nakumbuka wazee walivyokuwa wanamnukuu Marehemu Karume kuwa Muungano mwisho Chumbe naona sasa ni zamu ya Upande wa pili kusema Muungano mwisho Msasani.
 
Ahsante sana Bikirembwe kwa kuleta hii. Huu nao ni mwiba na ni miongoni mwa dhulma dhidi ya Wazanzibari, na hivyo ni miongoni mwa kero kuu za Muungano. Vinara wa JF nalo hili liangalieni, na kwa nguvu, kasi na ari moja litoleeni maelezo kama vile mnavyofanya vizuri katika mada za mafisadi za Richmond na EPA. Kwani dhulma ni dhulma tu, na maonevu ni maonevu tu, na upendeleo ni upendeleo tu uwe wa ufisadi au wa kuwanyima haki hao watoto wakati wenzao wapewa- Abaa!!!
 



hii ni dhulma ya wazi.

inasikitisha sana
 
Watu wameomba mkopo wala siyo msaada, halafu wakapewa Watanganyika, Wanzanzibari wakanyima, hii haingii akilini kabisa! Kama ndivyo ilivyotokea na hakuna maelezo ya kuridhisha toka wizarani basi tutakuwa na kila sababu ya kuamini ubaguzi umefanyika; kama ndivyo tujiulize huko wizarani wanatoa wapi kiburi hiki?
 

akina mkjj na wengine mko wapi? watetezi wa nyonge mko wapi? au hawa wazenji kufanyiwa haya ni sawa?


au wazanzibari hawana haki kwenye elimu ya juu?

ubaguzi huu mpaka lini? kwa nn hasa wazanzibar wanafanyiwa haya???
 
akina mkjj na wengine mko wapi? watetezi wa nyonge mko wapi? au hawa wazenji kufanyiwa haya ni sawa?


au wazanzibari hawana haki kwenye elimu ya juu?

ubaguzi huu mpaka lini? kwa nn hasa wazanzibar wanafanyiwa haya???

Niko kidogo skeptical na habari hii .Inakuwa kama habari ya sisi Waislam kila siku kulalama tunabaguliwa lakini ukiangalia hali halisi ni mentality tu .Sasa na hili la ndugu zetu wao kila siku wanabaguliwa at the same time wanajiita wazanzibari na si Watanzania .Tunaomba ushahidi mlate hoja tuingie kazini .
 

Enhe Balahau. Wao wajiita Wazanzibari kwa vile Katiba inaruhusu wajiite hivyo. na wengine hawawezi kujiita Watanganyika kwa sababu katiba ya TZ hairuhusu wajiite hivyo. Jenga hoja za uchambuzi na usijaribu kunyofoa vijipengelepengele na kuweka visingizio. Mchambuzi mahiri huyachukua mambo kwa ujumla wake na siyo katika isolation. Wazanzibari wapo kwa vile kuna nchi iitwayo Zanzibar, kuna Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, Kuna Mahkama za Zanzibar, kuna na SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR. Na Watanzania (ukijumuisha na Wazanzibari - Watanzania wenye asili ya Zanzibar-)wapo kwa sababu kuna nchi inaitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kuna Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mahkama za Tanzania, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Watanganyika hawapo kwa sababu hakuna Nchi iitwayo Tanganyika (hivi sasa),hakuna Serikali ya Tanganyika, hakuna Bunge la Tanganyika na hakuna Mahkama za Tanganyika. Hivyo kwa ufupi tu yupo Mzanzibari ambaye ni lazima awe Mtanzania, na yupo Mtanzania ambaye halazimiki kuwa Mzanzibari. Hivyo hawa ndugu zetu wana haki popote pale kujinasibu kwa kujiita Wazanzibari.
 
akina mkjj na wengine mko wapi? watetezi wa nyonge mko wapi? au hawa wazenji kufanyiwa haya ni sawa?


au wazanzibari hawana haki kwenye elimu ya juu?

ubaguzi huu mpaka lini? kwa nn hasa wazanzibar wanafanyiwa haya???

Hivi mtu apige kelele hadi koo limtoke!? Tulipopiga kelele kuhusu bodi ya mikopo mwaka mzima wa jana tukasema imeoza, inanuka rushwa, ina upendeleo, na haijalishi ni mzanzibari, mbara, mtumbatu, au mmakua, wao wanachojali ni nani atawahakikishia fedha! Mbona hatukusikika.

Kati ya wale vijana 29 waliokwama Ukraine unajua kati yao walikuwemo Wazanzibari? Kama walishaweza kufanya ubaguzi wao kwa kuangalia fedha (siyo mahali kama mnavyotutaka tuamini) kwanini mnafikiri wamebadilika wakati watu ni wale wale? Hadi pale bodi hiyo itakapofumuliwa kabisa na kuundwa upya kama Mamlaka ya Mikopo ya Elimu ya Juu mtaendelea kuwa na matatizo yale yale!.

Hao wanafunzi kama wapo waniandikie: mwanakijiji@klhnews.com
 

Unaenda mbali Mkuu katika kuandika mada hii mawazo yangu hayakuwa huko kwenye udini au ukabila - bahati mbaya hunijui lakini katika vitu ambavyo vinanichefua moyo ni ubaguzi uwe wa aina yeyote, hukutani na mimi nikakuuliza kwenu wapi au dini yako gani?

Nimeeleza mwanzoni kuwa itakuwa vigumu kutoa ushahidi "physical" kwani hela zimepelekwa ubalozini China na waliopewa ni wanaotoka Bara tu, kwa vile sina orodha ya malipo ya wanafunzi walopewa hiyo hela ni vigumu, lakini kama kweli mfatiliaji wasiliana na mimi kwa email(PM) na nitakupa jina la mtu wa kuwasiliana naye huko China na atakuhakikishia haya niliyoandika.

Marehmu Baba wa Taifa alisema kuwa ubaguzi ukianza mwisho mtakulana wenyewe kwa wenyewe na hili limeanza kuonekana kwani katika hao walionyimwa ni WTZ Bara waliohamia Znz kwa kazi tu lakini Mabwana wakubwa hawakujua waliloangalia ni huyu kapata nafasi hii kwa kutokea Zanzibar "stop" TUSIMPE MKOPO huu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…