Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 60
Watu wameomba mkopo wala siyo msaada, halafu wakapewa Watanganyika, Wanzanzibari wakanyima, hii haingii akilini kabisa! Kama ndivyo ilivyotokea na hakuna maelezo ya kuridhisha toka wizarani basi tutakuwa na kila sababu ya kuamini ubaguzi umefanyika; kama ndivyo tujiulize huko wizarani wanatoa wapi kiburi hiki?
Unaenda mbali Mkuu katika kuandika mada hii mawazo yangu hayakuwa huko kwenye udini au ukabila - bahati mbaya hunijui lakini katika vitu ambavyo vinanichefua moyo ni ubaguzi uwe wa aina yeyote, hukutani na mimi nikakuuliza kwenu wapi au dini yako gani?
Nimeeleza mwanzoni kuwa itakuwa vigumu kutoa ushahidi "physical" kwani hela zimepelekwa ubalozini China na waliopewa ni wanaotoka Bara tu, kwa vile sina orodha ya malipo ya wanafunzi walopewa hiyo hela ni vigumu, lakini kama kweli mfatiliaji wasiliana na mimi kwa email: zakyjason@hotmail.com na nitakupa jina la mtu wa kuwasiliana naye huko China na atakuhakikishia haya niliyoandika.
Marehmu Baba wa Taifa alisema kuwa ubaguzi ukianza mwisho mtakulana wenyewe kwa wenyewe na hili limeanza kuonekana kwani katika hao walionyimwa ni WTZ Bara waliohamia Znz kwa kazi tu lakini Mabwana wakubwa hawakujua waliloangalia ni huyu kapata nafasi hii kwa kutokea Zanzibar "stop" TUSIMPE MKOPO huu.
Hivi mtu apige kelele hadi koo limtoke!? Tulipopiga kelele kuhusu bodi ya mikopo mwaka mzima wa jana tukasema imeoza, inanuka rushwa, ina upendeleo, na haijalishi ni mzanzibari, mbara, mtumbatu, au mmakua, wao wanachojali ni nani atawahakikishia fedha! Mbona hatukusikika.
Kati ya wale vijana 29 waliokwama Ukraine unajua kati yao walikuwemo Wazanzibari? Kama walishaweza kufanya ubaguzi wao kwa kuangalia fedha (siyo mahali kama mnavyotutaka tuamini) kwanini mnafikiri wamebadilika wakati watu ni wale wale? Hadi pale bodi hiyo itakapofumuliwa kabisa na kuundwa upya kama Mamlaka ya Mikopo ya Elimu ya Juu mtaendelea kuwa na matatizo yale yale!.
Hao wanafunzi kama wapo waniandikie: mwanakijiji@klhnews.com
Hao maafisa wa ubalozi hapo china ni kina nani... majina ni muhimu sana. Elimu ya juu kumeoza na kama itakumbuka ile petition ya kumtoa Msolla ilikuwa inalenga mambo mengi likiwemo hili... majina ni muhimu.....
Maafisa wa Ubalozi China siwajui na hasa huyo mwambata wa Elimu lakini najua Balozi ni Omar Mapuri kama hajaondolewa. Mwafrika wa Kike unataka majina gani?, kama ni ya wanafunzi nitamuandikia alonipa habari hizi ili hayo majina yapatikane.
Wenye ushahidi wa kadhia hiyo na waumbwage hadharani kabla ya kutoa hukumu. Isije ikawa tunajadili kitu ambacho hakipo, Ama kila upande wa serikali ya Muungano na ya SMZ zina majukumu yake katika kuchangia elimu, iwe ya juu ama ya kawaida. Km ni hivyo iwapo upande mmoja kwa sababu moja ama nyingine imeshindwa kutekeleza majukumu yake na wakati huo huo upande mwingine umetekeleza wa kulaumiwa atajulikana.
Mwanakijiji nakubaliana na wewe kuwa Bodi ya Mikopo imeoza lakini hili suala ni tafauti kidogo kwani pale unapofanyika utumbo kwa vigezo vyengine inakuwa mnalaumu utaratibu wote kwa pamoja lakini inapotokea walengwa ni kundi fulani tu katika jamii inabidi ni lazima tuseme "sasa tunaenda mbali zaidi na ni dosari nyengine katika Muungano ambao unalegalega katika kamba ya Buibui".
Bikirembwe, ninachokataa ni kutaka kuona suala hili ni la "uzanzibari" na "ubara". Siamini hivyo, bila taarifa za kina ni vigumu kufikia hitimisho ilo unless tunaweza kuona clear cut WOTE waliokosa mikopo hiyo wanatoka visiwani na WOTE waliopata mikopo hiyo wanatoka bara. Vinginevyo kwangu mimi naona ni suala la Uzembe na ufisadi wa bodi ya mikopo.
Lakini hata hivyo ni lazima tuangalie pia kuwa je suala la mikopo ya elimu ya juu ni suala la muungano? kama walipewa mikopo ya kusoma huko basi wana haki naamini ya kupewa hiyo mikopo mingine, huwezi kumpa mchezaji jezi halafu umnyime viatu!
Jamani ni vizuri kuuliza na kufatilia kwa makini haya mambo kabla ya kuyashadadia.Mwaka 2003 kama sikosei kulitokea tetemeko algeria na wanafunzi wote wa kigeni walirudishwa makwao.Watanzania walipotuma taarifa bongo zikatumwa tiketi za wazanzibari tu.Amini usiamini wa visiwani warirudi ila wa bara walibaki huku kukiwa na hatari ya tetemeko lingine na ilibidi mikoa mingine walale nje(kwenye mahema)wakihofia majengo kushuka.Wizara ilituma mtu kutoka bara huyu anaitwa mama Kibaya muulize mtu yeyote aliyepata skolashipu na serikali anamjua huyu mama ndiye msimamizi mkuu.Huyu mama alilia hali aliyoikuta huko ukizingatia wengine walikwisha ondoka na kuacha wenzao kwenye hofu kuu.Wa bara nao wakapewa tiketi na kurudi ila hawajawahi kulalamika.Hebu fuatilieni hizo pesa zinatoka wapi na utaratibu wa kuomba ulikuwa vipi ndio muanze kupiga makelele.Halafu uliza uambiwe hasa wewe mwanakijiji,Waziri wa elimu ya juu alipokuja Algeria mwaka jana kuna watu waliomba wapewe pesa za usafirishaji wa mizigo,unajua walijibiwa nini?Waziri alisema huko mmeenda kusoma na sio kufanya biashara sasa mizigo mingi mmetoa wapi?Tukakaa kimyaaa!Ulikuwa ubaguzi huu?Mwanakijiji kwa taarifa yako tu na wala sitapoteza muda kuelezea haya mambo yashapitwa na wakati,baada ya kuropoka bila kufatilia mambo kwenye ile ishu ya watu kupata mikopo mara mbili hivi navyokuambia watu wanapata shida mpaka navyozungumza.Kwa kifupi hakuna mtu aliyepata mkopo mara mbili Algeria kama ulivyotolea mifano zaidi zaidi umeleta msiba huku watu wameuchuna tu!Naomba hili lifatilie kwa makini usije ukatibua mambo ya watu katika harakati zako za kutafuta misifa.Merci;
Jamani ni vizuri kuuliza na kufatilia kwa makini haya mambo kabla ya kuyashadadia.Mwaka 2003 kama sikosei kulitokea tetemeko algeria na wanafunzi wote wa kigeni walirudishwa makwao.Watanzania walipotuma taarifa bongo zikatumwa tiketi za wazanzibari tu.Amini usiamini wa visiwani warirudi ila wa bara walibaki huku kukiwa na hatari ya tetemeko lingine na ilibidi mikoa mingine walale nje(kwenye mahema)wakihofia majengo kushuka.Wizara ilituma mtu kutoka bara huyu anaitwa mama Kibaya muulize mtu yeyote aliyepata skolashipu na serikali anamjua huyu mama ndiye msimamizi mkuu.Huyu mama alilia hali aliyoikuta huko ukizingatia wengine walikwisha ondoka na kuacha wenzao kwenye hofu kuu.Wa bara nao wakapewa tiketi na kurudi ila hawajawahi kulalamika.Hebu fuatilieni hizo pesa zinatoka wapi na utaratibu wa kuomba ulikuwa vipi ndio muanze kupiga makelele.Halafu uliza uambiwe hasa wewe mwanakijiji,Waziri wa elimu ya juu alipokuja Algeria mwaka jana kuna watu waliomba wapewe pesa za usafirishaji wa mizigo,unajua walijibiwa nini?Waziri alisema huko mmeenda kusoma na sio kufanya biashara sasa mizigo mingi mmetoa wapi?Tukakaa kimyaaa!Ulikuwa ubaguzi huu?Mwanakijiji kwa taarifa yako tu na wala sitapoteza muda kuelezea haya mambo yashapitwa na wakati,baada ya kuropoka bila kufatilia mambo kwenye ile ishu ya watu kupata mikopo mara mbili hivi navyokuambia watu wanapata shida mpaka navyozungumza.Kwa kifupi hakuna mtu aliyepata mkopo mara mbili Algeria kama ulivyotolea mifano zaidi zaidi umeleta msiba huku watu wameuchuna tu!Naomba hili lifatilie kwa makini usije ukatibua mambo ya watu katika harakati zako za kutafuta misifa.Merci;
Unaenda mbali Mkuu katika kuandika mada hii mawazo yangu hayakuwa huko kwenye udini au ukabila - bahati mbaya hunijui lakini katika vitu ambavyo vinanichefua moyo ni ubaguzi uwe wa aina yeyote, hukutani na mimi nikakuuliza kwenu wapi au dini yako gani?
Nimeeleza mwanzoni kuwa itakuwa vigumu kutoa ushahidi "physical" kwani hela zimepelekwa ubalozini China na waliopewa ni wanaotoka Bara tu, kwa vile sina orodha ya malipo ya wanafunzi walopewa hiyo hela ni vigumu, lakini kama kweli mfatiliaji wasiliana na mimi kwa email: zakyjason@hotmail.com na nitakupa jina la mtu wa kuwasiliana naye huko China na atakuhakikishia haya niliyoandika.
Marehmu Baba wa Taifa alisema kuwa ubaguzi ukianza mwisho mtakulana wenyewe kwa wenyewe na hili limeanza kuonekana kwani katika hao walionyimwa ni WTZ Bara waliohamia Znz kwa kazi tu lakini Mabwana wakubwa hawakujua waliloangalia ni huyu kapata nafasi hii kwa kutokea Zanzibar "stop" TUSIMPE MKOPO huu.
Mwanakijiji nakubaliana na wewe kuwa Bodi ya Mikopo imeoza lakini hili suala ni tafauti kidogo kwani pale unapofanyika utumbo kwa vigezo vyengine inakuwa mnalaumu utaratibu wote kwa pamoja lakini inapotokea walengwa ni kundi fulani tu katika jamii inabidi ni lazima tuseme "sasa tunaenda mbali zaidi na ni dosari nyengine katika Muungano ambao unalegalega katika kamba ya Buibui".
Kwa signature ya maandiko yako wewe ni Mzanzibari.Hakuna Mbara anayeweza kkuandika neno Vyengine akiwa na maana ya vingine au neno nyengine akiwa nyingine.
Kwanza nakupa pole kwa vijana wetu kubaguliwa wakiwa ni Watanzania damu kutoka Zanzibar ambayo ni sehemu ya Tanzania.
Pili naomba kusema hivi;
Ndugu yangu unakosea sana kusema suala hili ni tofauti kidogo tu kwa sababu kwa sababu sasa hivi waliobaguliwa ni Wanzanzibar.
Mimi nilikuwa mmoja wa wana JF aliyepiga kelele nyingi kupinga vitendo viovu vya Bodi ya mikopo bila kujari ni watu wangapi wanaunga mokono na bila kujari watu hao ni wa bara au ni wa visiwani.
Ubaguzi ni Ubaguzi uwe wa rangi dini kabila utaifa hali au mwonekano wa sura. Ubaguzi ni Ubaguzi.
Ndiyo maana Wasomali wanapigana mpaka leo wakati dini yao ni moja Uislamu kabila laoni moja wote wasomali na rangi yao ni moja wote weusi.
Vita ya wasomali ni ya koo, ukoo mmoja unalamba risasi koo nyingine.
Ndugu yangu kitendo chako cha kulitenga tukio hili na kulifanya ni tofauti na tukio la wanafunzi 29 kinanipa hofu kwamba wewe ni mpiganaji tu pale wa kwenu akiwa matatani.
Kitendo cha kuwanyima mikopo wanafunzi 29 wa Ukraine na hiki cha kuwanyima mikopo wanafunzi wa Kizanzibari vyote ni vitendo vya ubaguzi.
Kwa hiyo kama unapenda wote tuingie katika mapambano ni vema ukubali kwanza hiki ni kitendocha ubaguzi sawa na vitendo vya ubaguzi vilivyowahi kufanywa hapo awali.
Hatahivyo, kama wewe unaona tendo hili la ubaguzi linabeba uzito mkubwa kwa sababu safari hii kigezo cha kubagua siyo Rushwa ila ni Uzanzibari na hivyo ni kizito zaidi. Mimi nitakuwa wa kwanza kuweka manyanga zangu chini kwa kitendo chako cha kupingana na ubaguzi kibaguzi.
Bikirembwe, ninachokataa ni kutaka kuona suala hili ni la "uzanzibari" na "ubara". Siamini hivyo, bila taarifa za kina ni vigumu kufikia hitimisho ilo unless tunaweza kuona clear cut WOTE waliokosa mikopo hiyo wanatoka visiwani na WOTE waliopata mikopo hiyo wanatoka bara. Vinginevyo kwangu mimi naona ni suala la Uzembe na ufisadi wa bodi ya mikopo.
Lakini hata hivyo ni lazima tuangalie pia kuwa je suala la mikopo ya elimu ya juu ni suala la muungano? kama walipewa mikopo ya kusoma huko basi wana haki naamini ya kupewa hiyo mikopo mingine, huwezi kumpa mchezaji jezi halafu umnyime viatu!