Auawa kikatili kisa wizi wa mihogo Ruangwa Lindi

Auawa kikatili kisa wizi wa mihogo Ruangwa Lindi

Friday Malafyale

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2017
Posts
1,811
Reaction score
2,916
Raia mmoja ambaye hajatambulika kwa haraka amekutwa amekufa kwa kuuliwa na kuchomwa moto hadi kufa. Kwa mujibu wa mtoa taarifa hii, tukio hili limetokea kijiji cha Luchelegwa Ruangwa Lindi njia inayoelekea Nachingwea kuna mwizi ameuawa na kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali usiku wa kuamkia leo asubuhi ambapo chanzo inadaiwa ni wizi wa mihogo.

Inadaiwa pia mmiliki wa shamba la mihogo alikuwa akilalamika mara kadhaa kuibiwa shambani mwake, hadi akaamua kuvizia wezi wa mihogo ndipo ikatokea mpambano mkubwa kati ya mwizi na mwenye shamba, ambapo mwenye shamba amejeruhiwa vibaya. Lakini pia mwizi ameuawa na kuchomwa moto.

Chanzo mwenyeji wa Luchelegwa Ruangwa Lindi.
 
Updates.....
Mwizi ametambuliwa na inaonekana ni mkaazi wa kijiji cha Chinongo mbele ya Luchelegwa, na ndugu zake wamepigiwa simu na ametambuliwa. REST IN HELL TO HIM
 
Inabidi tuwawinde waliokula pesa za kodi.
Tufuate ile ripoti ya CAG
 
Bongo kuua wezi imeshakuwa jambo la kawaida siku hizi.

Wezi wa mihogo wanachomwa Moto,Ila wezi wa mabilioni wanaachwq wanazurula mitaani na ma-V8.
 
Kuna watu wanajifanya hawapaoni panaposema "...palitokea mpambano mkali Kati ya mwizi na mwenye shamba na kupelekea mwenye shamba kujerehiwa vibaya.." lakini kila mtu anasitikia kifo Cha mwizi aliyeuawa. Ndiyo yaleyale ya Helen Kijo Bi Simba, polisi aliuawa anakaa kimya utadhani hamna kilichotokea lakini akiuawa jambazi atatoa tamko na mishipa imemjaa kichwan
 
Ibaaa mamilion kwa mabilion hutauliwa

Ova
 
Yaani mihogo ameiba! Na bado akaanzisha tifu kwa mwenye shamba, marehemu mwizi inaonekana alikuwa m'babe sana.
 
Back
Top Bottom